Kichochoro
JF-Expert Member
- Jul 18, 2017
- 1,135
- 1,163
Wakuu ni rafiki yangu wa karibu sana mwaka wa tatu anaishi na mke wake ambaye yeye anadai alimuoa tu kutokana na kwamba akiwa single aliwahi kutoka na huyo binti na hatimaye akapata ujauzito.
Baada ya kupata ujauzito wazazi wa binti walileta hoja kwamba ni mwanafunzi na yeye ili kuua soo akaona akubali kumuoa ili kuepusha mambo mengi kama kupelekwa mahakama na polisi.
Lakini hakuna ndoa yoyote iliyofungwa walivutana tu kienyeji! Sasa rafiki yangu huyu amekuwa akiniita mara kwa mara nimshauri maana anasema huyo mwanamke hampendi kabisa toka moyoni Ila anaishi naye tu.
Sasa anataka kuachana na huyu dada lakini tangu aishi naye hakuna ugomvi wowote ulishawahi kutokea kati yake na yeye Ila kinachomuuma anaishi na mwanamke asiyempenda yaan kiufupi Hana furaha!
Nimeileta hoja hii humu ili niweze kupata mawazo mengine ambayo pengine ninaweza kumwelezea nayakamsaidia.
Baada ya kupata ujauzito wazazi wa binti walileta hoja kwamba ni mwanafunzi na yeye ili kuua soo akaona akubali kumuoa ili kuepusha mambo mengi kama kupelekwa mahakama na polisi.
Lakini hakuna ndoa yoyote iliyofungwa walivutana tu kienyeji! Sasa rafiki yangu huyu amekuwa akiniita mara kwa mara nimshauri maana anasema huyo mwanamke hampendi kabisa toka moyoni Ila anaishi naye tu.
Sasa anataka kuachana na huyu dada lakini tangu aishi naye hakuna ugomvi wowote ulishawahi kutokea kati yake na yeye Ila kinachomuuma anaishi na mwanamke asiyempenda yaan kiufupi Hana furaha!
Nimeileta hoja hii humu ili niweze kupata mawazo mengine ambayo pengine ninaweza kumwelezea nayakamsaidia.