Ushauri kwa Membe, Jitenge na Wanafiki

Ushauri kwa Membe, Jitenge na Wanafiki

Mwamakula tu ndiye anaweza ku discuss issue ya Msiba, maana alisimamia ukweli na haki. hawa wengine ni takataka.
Mwamakula anasema walimtumia mjumbe akamwambia aache kuimba mambo ya haki vinginevyo atapotea. Mtumishi wa Mungu akasema kama kuimba Haki mnataka kuniua basi kamwambie aliyekutuma aje aniue tu.

Mwamakula ni kama Meshaki, Abedenego na Shadrack kwa Nebkadineza.
 
Hapa huzungumzii msamaha tena, nakuona unazungumzia kisasi kwa sauti ya juu huku ukikipa jina la msamaha.

Unaonekana upo na mihemko ya kiwango cha juu sana, mpaka unafikia stage ya kumuita mwanadamu mwenzio shetani ukisahau tumeaswa tusihukumu ili nasi tusije kuhukumiwa.

Nawaona wengi wenu hii issue ya Musiba na Membe mnaichukulia kishabiki sana, mmeshindwa kabisa kutofautisha hisia zenu na uhalisia.
Jipe muda, uelewe maana ya kisasi.

Kwa ufupi ni kwamba, kwa mfano wewe ukaiba mali ya mtu, yule mtu akapata ushahidi kuwa ulimwibia, akaenda kukushtaki, nawe ukahukumiwa kwa lile kosa, hicho siyo kisasi. Umeadhibiwa kwa uovu ulioufanya.

Lakini kwa mfano wewe leo hii ukaenda ofisi ya kampuni fulani kutafuta kazi,, kwenye hiyo ofisi akawepo mwajiri ambaye kwa upendeleo tu kwa watu fulani, akakunyima ajira wakati sifa unazo. Baada ya miaka kupita, wewe ukapata kazi, na yule aliyekunyima ajra hapo kale naye akaja kumwacha mwajiri waje wa mwanzo, akaajiriwa kwenye kampuni ambayo wewe sasa upo, na wewe ukawa ndiye mkurugenzi mkuu wa kampuni. Huyo bwana akafanya kosa dogo lililostahili kupewa onyo lakini ukaamua kumfukuza kazi kwa sababu tu unakumbuka alivyokutenda hapo kale, hicho ndicho huitwa kisasi.
 
Kuna kelele nyingi za wanafiki kwako Mh. Membe. Lililo jema ni kwamba unaufahamu sana unafiki wao.

Manabii wa kweli wa Mungu, tangu historia, na tangu kale, wanafahamika kwa kusimama na kuusemea ukweli. Hawakujali nini kitawapata kwa kuwa wakweli. Walismama imara hata dhidi ya wafalme wenye nguvu na wenye mamlaka ya kutisha.

Tuwaulize viongozi wetu wa dini, wakati watu wakishambuliwa kwa risasi, wakiuawa, wakitekwa, wakiporwa mali zao, wakibambikiziwa kesi na kutupwa magerezani kwa uonevu, wao waliokuwa wapi? Walisimama upande upi? Walinena nini juu ya uovu ule?

Mungu aendelee kusimama na viongozi wa dini waliokemea na wanaoendelea kukemea uovu, wanaoutumikia ukweli, kwa sababu Mungu wetu ni Mungu wa ukweli, ni Mungu wa haki.

Ushauri wangu kwako Membe, ili usiendelee kusumbuliwa na watu wanafiki wanaojifanya wana hekima leo, lakini walijifanya vipofu na mabubu wakati uovu unatendeka, toa tamko kuwa iwe ni ofisini kwako, nyumbani kwako au mahali pengine popote, hutaki kutembelewa na mtu yeyote mnafiki ambaye anakuja eti kumwombea msamaha Musiba.

Ikikupendeza ruhusu tu kujadiliana na watu wenye hekima, watu ambao maisha yao yamejawa na kusimama katika ukweli bila ya kujali watawala watanena nini.

Lakini ufahamu kuwa ule uchafuzi wa haiba za watu, uhamasishaji wa watu kuuawa na kufungwa ulikuwa ni mradi uliohusisha watu wengi, mbele wakiwa wamemsimamisha Musiba, wao wakiwa nyuma yake. Hao waliokuwa nyuma yake, wengi wao ndio watakuja sasa na kujifanya washauri wa kukutaka umsamehe Musiba. Na wengine kwa vile hawawezi kukyfikia, wanawatumia viongozi wa dini wanaoamini wanaweza kuwatumia.

Ukweli ni kwamba watu hawa hawaombi umsamehe Musiba kama mtu tu, bali umsamehe mwenzao ambaye walimweka mbele na wao wakiwa nyuma yake. Hawa wanataka kujitoa kwenye mazingira ya kulaumiwa na Musiba ambaye anawaona wamemsaliti kwa kutomsaidia nyakati hizi. Ukimwachia huyu mhalifu, hawa wahalifu wenzake watakwenda na kumwambia kuwa tumefanya kazi, tumekusaidia mpaka umekuwa huru sasa. Mbinu yao kubwa waliyoibuni kwa sasa ni kuwatumia viongozi wa dini ambao wwanawafahamu kuwa kwa namna fulani walikuwa nao katika katika hali ile ya kuulinda uovu.

Waliokuwa na Musiba, wamsaidie Musiba kulipia uovu wake, maana wao ni sehemu yake katika uovu wake. Na baadhi ya watu ambao sio waovu, na hawakuwahi kuwa waovu, wawe na hekima siyo kukubali maombi ya watu hovyo hovyo, hata wakaharibiwa heshima zao kutokana na kutumika na hao waovu wa kundi la Musiba.

Mpaka sasa si Musiba binafsi ndiye anayewaona viongozi wa dini kumwombea msamaha Musiba, bali ni watu wale wenzake na Musiba ndio wanaoenda kwa hao viongozi wa dini.

Mh. Membe, ujaliwe hekima katika hili.
Imani yangu wewe ni mmoja kati ya hilo kundi la wanafiki, ushauri wa hovyo sana huu uzungumzao
 
Imani yangu wewe ni mmoja kati ya hilo kundi la wanafiki, ushauri wa hovyo sana huu uzungumzao
Mjinga akikuambia wewe ni mjinga wakati siyo mjinga, hutakuwa mjinga kwa sababu kuna mjinga amesema wewe ni mjinga.
 
Jipe muda, uelewe maana ya kisasi.

Kwa ufupi ni kwamba, kwa mfano wewe ukaiba mali ya mtu, yule mtu akapata ushahidi kuwa ulimwibia, akaenda kukushtaki, nawe ukahukumiwa kwa lile kosa, hicho siyo kisasi. Umeadhibiwa kwa uovu ulioufanya.

Lakini kwa mfano wewe leo hii ukaenda ofisi ya kampuni fulani kutafuta kazi,, kwenye hiyo ofisi akawepo mwajiri ambaye kwa upendeleo tu kwa watu fulani, akakunyima ajira wakati sifa unazo. Baada ya miaka kupita, wewe ukapata kazi, na yule aliyekunyima ajra hapo kale naye akaja kumwacha mwajiri waje wa mwanzo, akaajiriwa kwenye kampuni ambayo wewe sasa upo, na wewe ukawa ndiye mkurugenzi mkuu wa kampuni. Huyo bwana akafanya kosa dogo lililostahili kupewa onyo lakini ukaamua kumfukuza kazi kwa sababu tu unakumbuka alivyokutenda hapo kale, hicho ndicho huitwa kisasi.
Nabaki hapo kwenye mfano wako wa mwajiri, then inakuje kama huyo jamaa akituma watu waje kukuomba msamaha kwa kosa alilokufanyia mwanzo hadi ukaenda kutafuta kazi sehemu nyingine, na baadae kupandishwa cheo, ukiukataa msamaha wake hicho sio kisasi?
 
Naona unauwekea msamaha mipaka mpaka kuanza kuwaita wale wanaotaka Musiba asamehewe ni wanafiki.

Msamaha ni msamaha tu, bila kujalisha unaombwa muda gani, na wakina nani, lakini sio kuwaita wale wanaokutaka usamehe wanafiki, kwangu huko ni kutafuta kisingizio tu cha kutosamehe.
Mbona misamaha mingine haiwi na publicity na trending kama huu?

Huu inabidi utafautishwe na hiyo mingine ya kawaida kwa sababu kila kitu chake pia sio cha kawaida.

Je Kabla ya Musiba uliwahi ona wapi mtu akitukana, kutisha, kuchafua, kufedhehesha watu namna ile, tena hadharani, kwenye mitandao na kwingineko??

Nampongeza Bw. Membe, kwani amewakilisha wahanga wengine wengi kumshughulikia yule mhuni.
 
Mkuu Bams, Inavyoonekana wewe ni mtu mzima atleast mtu wa makamo piga ua enye miaka 40-50 una elimu ya kutosha na ni mcha mungu una familia halafu unapenda haki na unaamini kuwa jinai haiozi, hupendi unafiki,unajali watu na huwa ni mtetezi wa wanyonge n.k n.k

Kitu ambacho sijaweza kudadavua hata kwa kukisia kisia huko juu ni Una asili ya Bara gani- Asili yako? Mwafrika Muarabu, Mzungu wa Ulaya, au MwaAshia n.k uniwie radhi na naomba unisahihishe kama hayo juu sio description nzuri au ina uwalakini...ila kwa kifupi naweza kusema wewe ni Mtanzania wa Asili ya bara gani haswa sijui. Ni muhimu, ni muhimu kwa swali niliokuwa nalo na nitaweza kukuuliza tu iwapo nina jibu
 
Bams uko sahihi mkuu, maana Musiba mbali na hiyo kesi ya Membe lakini pia angekuweza kuwa na kesi ya jjnai na hata kufungwa jela - ni vile basi utawala wa sheria uliwekwa ndani ya jokofu awamu ile.
 
Kweli lazima misiba alipe bilioni 8, tuache unafiki. Member alidharilishwa mkawa mnafurahia, Leo ndio mnajua Dunia inazunguka. Yani uwafanyie wengine ubaya uwachwe kisa Dunia inazunguka?. Alipe pesa za watu huyo chawa.
Hajadhalilishwa isipokuwa mipango yake ya gizani pamoja na wote aliowataja Musiba iliwekwa hadharani. Labda kosa la Musiba ni kuiweka hadharani kinyume Cha Sheria lakini tuhuma zote zilikuwa sahihi Kwa 100%
 
Fisadi tu ilo membe
Hajadhalilishwa isipokuwa mipango yake ya gizani pamoja na wote aliowataja Musiba iliwekwa hadharani. Labda kosa la Musiba ni kuiweka hadharani kinyume Cha Sheria lakini tuhuma zote zilikuwa sahihi Kwa 100%
 
Kuna kelele nyingi za wanafiki kwako Mh. Membe. Lililo jema ni kwamba unaufahamu sana unafiki wao.

Manabii wa kweli wa Mungu, tangu historia, na tangu kale, wanafahamika kwa kusimama na kuusemea ukweli. Hawakujali nini kitawapata kwa kuwa wakweli. Walismama imara hata dhidi ya wafalme wenye nguvu na wenye mamlaka ya kutisha.

Tuwaulize viongozi wetu wa dini, wakati watu wakishambuliwa kwa risasi, wakiuawa, wakitekwa, wakiporwa mali zao, wakibambikiziwa kesi na kutupwa magerezani kwa uonevu, wao waliokuwa wapi? Walisimama upande upi? Walinena nini juu ya uovu ule?

Mungu aendelee kusimama na viongozi wa dini waliokemea na wanaoendelea kukemea uovu, wanaoutumikia ukweli, kwa sababu Mungu wetu ni Mungu wa ukweli, ni Mungu wa haki.

Ushauri wangu kwako Membe, ili usiendelee kusumbuliwa na watu wanafiki wanaojifanya wana hekima leo, lakini walijifanya vipofu na mabubu wakati uovu unatendeka, toa tamko kuwa iwe ni ofisini kwako, nyumbani kwako au mahali pengine popote, hutaki kutembelewa na mtu yeyote mnafiki ambaye anakuja eti kumwombea msamaha Musiba.

Ikikupendeza ruhusu tu kujadiliana na watu wenye hekima, watu ambao maisha yao yamejawa na kusimama katika ukweli bila ya kujali watawala watanena nini.

Lakini ufahamu kuwa ule uchafuzi wa haiba za watu, uhamasishaji wa watu kuuawa na kufungwa ulikuwa ni mradi uliohusisha watu wengi, mbele wakiwa wamemsimamisha Musiba, wao wakiwa nyuma yake. Hao waliokuwa nyuma yake, wengi wao ndio watakuja sasa na kujifanya washauri wa kukutaka umsamehe Musiba. Na wengine kwa vile hawawezi kukyfikia, wanawatumia viongozi wa dini wanaoamini wanaweza kuwatumia.

Ukweli ni kwamba watu hawa hawaombi umsamehe Musiba kama mtu tu, bali umsamehe mwenzao ambaye walimweka mbele na wao wakiwa nyuma yake. Hawa wanataka kujitoa kwenye mazingira ya kulaumiwa na Musiba ambaye anawaona wamemsaliti kwa kutomsaidia nyakati hizi. Ukimwachia huyu mhalifu, hawa wahalifu wenzake watakwenda na kumwambia kuwa tumefanya kazi, tumekusaidia mpaka umekuwa huru sasa. Mbinu yao kubwa waliyoibuni kwa sasa ni kuwatumia viongozi wa dini ambao wwanawafahamu kuwa kwa namna fulani walikuwa nao katika katika hali ile ya kuulinda uovu.

Waliokuwa na Musiba, wamsaidie Musiba kulipia uovu wake, maana wao ni sehemu yake katika uovu wake. Na baadhi ya watu ambao sio waovu, na hawakuwahi kuwa waovu, wawe na hekima siyo kukubali maombi ya watu hovyo hovyo, hata wakaharibiwa heshima zao kutokana na kutumika na hao waovu wa kundi la Musiba.

Mpaka sasa si Musiba binafsi ndiye anayewaona viongozi wa dini kumwombea msamaha Musiba, bali ni watu wale wenzake na Musiba ndio wanaoenda kwa hao viongozi wa dini.

Mh. Membe, ujaliwe hekima katika hili.
Bandiko reefu,kiko wapi sasa?
Acha aende kuzimu huko hatuitaji msamaha wa mfu

Maisha ndo hayahaya
Na malipo ni hapahapa
 
Back
Top Bottom