Countrywide
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 18,190
- 27,237
Habari wanajf, leo kuna jambo moja ambalo nimeona nilizungumzie ili tuweze kukaa sawa na kuweza kushinda mapambano yetu yanayokuja.
Ninaamini kuwa hadi sasa CHADEMA ila ilani nzuri sana ambayo ikitekelezwa italeta manufaa kwa nchi na wananchi kwa ujumla.
Nguvu kubwa tuiweke hapa kwa maana ndio utakuwepo utofauti kati ya Chama tawala na chadema.
Kama tunavyojua mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi na tupo kwenye kampeni kipindi hiki, yes propaganda chafu inaweza kuwa moja ya silaha kubwa kuweza kushinda lakini hizi propaganda chafu ziwe zinakaribiana na ukweli.
Nimejaribu kufikiria mara mbilimbili aina ya maneno/tweets anazotoa mgombea wetu nabaki kukosa majibu na kuhisi pengine chama hakijaweza kukaa naye au kumsaidia kufanya hizi propaganda.
Mgombea uraisi wetu ambae tunahitaji kuwa mbadala wa chama tawala anatakiwa kuwa smart mara mbili kuliko aliyepo madarakani ili uhalali wa yeye kumuondoa uwepo.
Ni lazima kujitofautisha, kama wa chama tawala anafanya mabaya, basi wa kwetu afanye mazuri wananchi wawe na imani nae.
Wapiga kura wapo wa ina nyingi, pia kuna kundi kubwa la wasomi ambao wana uwezo mkubwa sana wa kuchambua yupi ni sahihi na yupi sio. Hapa nazungumzia wale ambao hawana ushabiki.
Tweets za mgombea wetu zinafikirisha sana, unawezaje kutweet jambo ambalo wewe mwenyewe hauna uhakika nalo?
Hebu fikiria siku kadhaa nyuma wakati anahojiwa juu ya kufungiwa kwake alisema mgombea wa CCM anaenda mapumziko ya siku 8 (jambo ambalo sio kweli) na akasema ataanza kampeni tarehe 12(jambo ambalo sio kweli).
Haya maneno mgombea wetu anatakiea kuachana nayo kwa kuwa yanaondoa credibility yake. Haya maneno ni ya kuokoteza mitandaoni wanatakiwa wabaki nayo mashabiki tu wala yasifike kwa mgombea uraisi na kuyazungumza.
Leo mgombea wetu ametweet kuwa wafanyabiashara kariakoo wanalazimishwa kufunga biashaea kwenda uwanjani kwenye kampeni za ccm. Anasema hivi akijua kabisa kuwa ni uongo, watu wapo kkoo na wanaona anayosema, mwisho wa siku nao wanabaki wanajiuliza ni kariakoo ipi hiyo?
Hakuna mfanyabiashara kariakoo anaelazimishwa kwenda uwanjani na haiwezekani, kinachofanyika ni gari ya matangazo kupita na kuwatangazia watu kuwa kuna mkutano uwanja wa taifa ,sasa kwenda au kutokwenda inabaki kuwa uamuzi wako.
Hizi propaganda ashauriwe zibaki kuwa kwa mashabiki tu na sio kwa level yake.
Chadema tujisahihishe hapa, tumsadie na mgombea wetu nae ajisahihishe.
Ninaamini kuwa hadi sasa CHADEMA ila ilani nzuri sana ambayo ikitekelezwa italeta manufaa kwa nchi na wananchi kwa ujumla.
Nguvu kubwa tuiweke hapa kwa maana ndio utakuwepo utofauti kati ya Chama tawala na chadema.
Kama tunavyojua mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi na tupo kwenye kampeni kipindi hiki, yes propaganda chafu inaweza kuwa moja ya silaha kubwa kuweza kushinda lakini hizi propaganda chafu ziwe zinakaribiana na ukweli.
Nimejaribu kufikiria mara mbilimbili aina ya maneno/tweets anazotoa mgombea wetu nabaki kukosa majibu na kuhisi pengine chama hakijaweza kukaa naye au kumsaidia kufanya hizi propaganda.
Mgombea uraisi wetu ambae tunahitaji kuwa mbadala wa chama tawala anatakiwa kuwa smart mara mbili kuliko aliyepo madarakani ili uhalali wa yeye kumuondoa uwepo.
Ni lazima kujitofautisha, kama wa chama tawala anafanya mabaya, basi wa kwetu afanye mazuri wananchi wawe na imani nae.
Wapiga kura wapo wa ina nyingi, pia kuna kundi kubwa la wasomi ambao wana uwezo mkubwa sana wa kuchambua yupi ni sahihi na yupi sio. Hapa nazungumzia wale ambao hawana ushabiki.
Tweets za mgombea wetu zinafikirisha sana, unawezaje kutweet jambo ambalo wewe mwenyewe hauna uhakika nalo?
Hebu fikiria siku kadhaa nyuma wakati anahojiwa juu ya kufungiwa kwake alisema mgombea wa CCM anaenda mapumziko ya siku 8 (jambo ambalo sio kweli) na akasema ataanza kampeni tarehe 12(jambo ambalo sio kweli).
Haya maneno mgombea wetu anatakiea kuachana nayo kwa kuwa yanaondoa credibility yake. Haya maneno ni ya kuokoteza mitandaoni wanatakiwa wabaki nayo mashabiki tu wala yasifike kwa mgombea uraisi na kuyazungumza.
Leo mgombea wetu ametweet kuwa wafanyabiashara kariakoo wanalazimishwa kufunga biashaea kwenda uwanjani kwenye kampeni za ccm. Anasema hivi akijua kabisa kuwa ni uongo, watu wapo kkoo na wanaona anayosema, mwisho wa siku nao wanabaki wanajiuliza ni kariakoo ipi hiyo?
Hakuna mfanyabiashara kariakoo anaelazimishwa kwenda uwanjani na haiwezekani, kinachofanyika ni gari ya matangazo kupita na kuwatangazia watu kuwa kuna mkutano uwanja wa taifa ,sasa kwenda au kutokwenda inabaki kuwa uamuzi wako.
Hizi propaganda ashauriwe zibaki kuwa kwa mashabiki tu na sio kwa level yake.
Chadema tujisahihishe hapa, tumsadie na mgombea wetu nae ajisahihishe.