kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,252
- 16,171
- Thread starter
- #41
wale wenye Faraqi, matalasimu, halubadili na makombe walisoma nini? Kabla ya kufa kuna maisha, vijana wa kiislam wanaadhirika kwa kusosa ajira kutokana na ukosefu wa elimu. Ukienda pale msikitini hata sadaka haitoki na kama ikitoka basi ni sh. 50, 100, 200, 500 tu ambazo hazitoshi kumlipa Imam na matumizi ya msikiti, hawawezi kuchangishana kujenga msikiti ila kwa kuwanategemea wafadhiri wenye rangi zilezile kila siku, hii yote ni kutokana na ukosefu wa kipato. Ninamsifu sana Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi kwa kuwahimiza waislamu wasome zaidi pia elimu ya circular ingawa baadhi yao wanampiga vibao hadharani anapowaambia mambo yanayotokana na kusoma elimu ile ya Uchina aliyoiagiza Bw. Mtume isomwe. Mtume alijua kuwa iko siku jamii itakubwa na maradhi kama UKIMWI ambayo yatahitaji elimu ya Wachina. Hebu ona vijana wa kiislam waliokwenda kuswali lakini bado wanaiba misikitini viatu vizuri vya waumini wenzao wanaoswali wakati wa ibada. Kama ukiangalia viatu vya waumini vilivyovuliwa pale mlangoni msikitini wakati wa kuswali utagundua kuwa hawa waliokondani humo msikitini ni maskini sana, ndala na yeboyebo zilizochoka sana, na wale wenye viatu vizuri inawalazimu kuviingiza msikitini ili visiibiwe. Waumini wamevaa nguo za mitumba zilizokuwa zinavaliwa na wagalatia (wazungu) kutoka ulaya. Hivi vyote ni viashiria vya umaskini ambavyo BAKWATA yetu lazima ijione kuwa ina dhima ya kuwafanyia mageuzi waislamu kuhusu elimu na kazi nyingine za kuinua kipato chao, maana watu wenye kipato hata sadaka na zaka watatoa nyingi kiasi cha kuweza kugharamia kuwatuza masheikh wao, kuwalipa walimu wa madrasa na kuwatunzi mayatima vizuri, hivyo kuupeleka mbele uislamu. Wakristo wao wanatoa sadaka na zaka kubwa makanisani hivyo wanamudu kuwatunza wachungaji wao vizuri, sisi tunategemea nyama ya ngamia na tende ziletwe kutoka kulekule. Waislam tusisubiri tukosolewe na watu wengine ili tuwashikie majambia tuwapige, tujisahihishe sisi wenyewe kwa wenyewe ndani kwa ndani. Aliempiga kibao Mzee Mwingi alikosea sana, kwani Bw. Mtume aliposema itafuteni elimu hata mbali na uarabuni ilimaanisha kuje kuwe na watu wa kuyasema kama yale aliyoyasema Mzee Mwinyi kwa waislamu pale siku ile. Mafundisho gani hayo yanayoruhusu kumzaba mzee kama Ali Hassani Mwinyi kama sio laana na bangidini yetu inatutaka kusoma quran na kuiweka kichwani na kuwalazimisha watoto wetu kufanya hivyo kwani Mwenyezi Mungu alishajua kuwa zama za mwisho vitabu vitavamiwa, watu watabadilisha baadhi ya aya as quran kwa manufaa Yao binafsi, hapo kama quran haipo kichwani utaweza kubabaika lkn kama ulibahatika kuisoma na kuihifadhi kichwani huwezi kubabaika. Na Allah anajua zaidi