kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,252
- 16,171
Dunia imegeuka geukieni elimu dunia kwa watoto wenu wa Kiislam kwa vitendo. Geuzeni madrasa zenu kuwa vituo vya elimu ambako watoto wanafunzwa masomo ya dini, hesabu, english, sayansi, historia, na ufundi badala ya kulazimisha watoto wenu wakariri (wahifadhi) Quran pekee wakiwa wadogo sana umri uleule ambao watoto wengine wako bize na kujifunza A B C D na 1, 2, 3,.... Umri mdogo ni muhimu sana kwa watoto kuhamasika kujifunza kitu chochote.
Nimefanya utafiti wangu mdogo kwa watoto wa kiislamu nikagundua kuwa wale wanaoimba taarab, muziki, wakata mkaa, wamachinga, na walinzi wa usiku wengi wao wamepitia madrasa hizi lakini wamekosa elimu, ajira rasmi na mitaji ya kufanya biashara kama wale wenzao waliopitia madrasa pia lakini wana asili ya Asia kama vile waarabu, wahindi, wapemba, nk.
Hii ina maana kuwa elimu ya madrasa haitoi ajira, ujuzi wala mitaji ya biashara kwa watoto wanapokuwa watu wazima hasa kwa watoto ambao hawana asili ya Asia. Yaani waislamu weusi wengi wao wanakosa elimu, ujuzi na mitaji ya biashara wanapofikia umri wa kujitegemea na matokeo yake watanyakazi yoyote bila kujali elimu ya dini waliyoipigania na kuihifadhi vifuani walipokuwa watoto kwenye madrasa hizi.
Hii ni tofauti kabisa na watoto wa kiislamu wenye asili ya Asia ambao watakuwa na elimu ya dini na ujuzi na mitaji ya kufanya biashara. Wengi wao weusi wenye elimu kubwa ya kidini wanaishia kugombania uimamu misikitini na kutupiana majini, kuwa waganga wa kienyeji na wapiga ramli na makafara ili kujipatia riziki.
Wazazi wa Watoto wa kiislamu weusi (Waafrika) lazima wawe makini sana kwenye elimu za watoto wao wakiwa wadogo, maana samaki anakunjwa akiwa mdogo, wapeni watoto elimu zote za dini na dunia kwa wakati mmoja utotoni ili kuwapunguzia adha ya kuwa wazindikizaji wa wenzao kwenye maisha watakapokuwa wakubwa, maana elimu ya dini haitoi ajira ya kutosha kwa vijana wengi.
Nimefanya utafiti wangu mdogo kwa watoto wa kiislamu nikagundua kuwa wale wanaoimba taarab, muziki, wakata mkaa, wamachinga, na walinzi wa usiku wengi wao wamepitia madrasa hizi lakini wamekosa elimu, ajira rasmi na mitaji ya kufanya biashara kama wale wenzao waliopitia madrasa pia lakini wana asili ya Asia kama vile waarabu, wahindi, wapemba, nk.
Hii ina maana kuwa elimu ya madrasa haitoi ajira, ujuzi wala mitaji ya biashara kwa watoto wanapokuwa watu wazima hasa kwa watoto ambao hawana asili ya Asia. Yaani waislamu weusi wengi wao wanakosa elimu, ujuzi na mitaji ya biashara wanapofikia umri wa kujitegemea na matokeo yake watanyakazi yoyote bila kujali elimu ya dini waliyoipigania na kuihifadhi vifuani walipokuwa watoto kwenye madrasa hizi.
Hii ni tofauti kabisa na watoto wa kiislamu wenye asili ya Asia ambao watakuwa na elimu ya dini na ujuzi na mitaji ya kufanya biashara. Wengi wao weusi wenye elimu kubwa ya kidini wanaishia kugombania uimamu misikitini na kutupiana majini, kuwa waganga wa kienyeji na wapiga ramli na makafara ili kujipatia riziki.
Wazazi wa Watoto wa kiislamu weusi (Waafrika) lazima wawe makini sana kwenye elimu za watoto wao wakiwa wadogo, maana samaki anakunjwa akiwa mdogo, wapeni watoto elimu zote za dini na dunia kwa wakati mmoja utotoni ili kuwapunguzia adha ya kuwa wazindikizaji wa wenzao kwenye maisha watakapokuwa wakubwa, maana elimu ya dini haitoi ajira ya kutosha kwa vijana wengi.