Ushauri kuhusu makabati ya jikoni.

Ushauri kuhusu makabati ya jikoni.

Udochi

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2015
Posts
1,073
Reaction score
1,576
Habari wakuu.
Baada ya kushindwa kumudu kuweka makabati ya mbao jikoni kutokana na ukubwa gharama,
Pia ya zege kwa kuhofia kutokuwa na mwonekano mzuri,
Nimefikiria ama kutumia materials za
1) MDF au 2) MARINE BOARD.
Ingawa fundi aliniambia kuwa hizo aina mbili za board hazidumu, hasa zikigusa maji.

Kwa waliotumia moja kati ya MDF na Marine boards,
naomba mwongozo wa uimara na changamoto za hizo materials kwa makabati ya jikoni.

Napokea ushauri mwingine wa maboresho.
 
MDF ikipata maji si chaap tu unaitupa? Na jikoni kulivo na mishe za maji??

Heri tu ujibane mdogo mdogo utengeneze mbao imara au hata kabati za kujenga tu kwa cement ukipata fundi mzuri akafanya finishing nzuri yanapendeza.

Ila tu ndani ajengee vizuri, pakiwa ovyo panakua na mchanga tu basi vyombo vinakua kama vipo site.
 
Habari wakuu.
Baada ya kushindwa kumudu kuweka makabati ya mbao jikoni kutokana na ukubwa gharama,
Pia ya zege kwa kuhofia kutokuwa na mwonekano mzuri,
Nimefikiria ama kutumia materials za
1) MDF au 2) MARINE BOARD.
Ingawa fundi aliniambia kuwa hizo aina mbili za board hazidumu, hasa zikigusa maji.

Kwa waliotumia moja kati ya MDF na Marine boards,
naomba mwongozo wa uimara na changamoto za hizo materials kwa makabati ya jikoni.

Napokea ushauri mwingine wa maboresho.
Jitahidi tu Bora hata usubiri kwa muda uweze kumudu hizo gharama kuliko kuweka kitu ambacho Una uhakika baada ya muda utatakiwa kubadilisha. Unless hapo kwako hapana mishe nyingi jikoni ( huna familia au ni ndogo Sana)
 
MDF ikipata maji si chaap tu unaitupa? Na jikoni kulivo na mishe za maji??

Heri tu ujibane mdogo mdogo utengeneze mbao imara au hata kabati za kujenga tu kwa cement ukipata fundi mzuri akafanya finishing nzuri yanapendeza.

Ila tu ndani ajengee vizuri, pakiwa ovyo panakua na mchanga tu basi vyombo vinakua kama vipo site.
mama mwenye nyumba katika moja na mbili.
 
kama una jamaa zako kuanzia goweko, tabora, au hata mpanda ambako mininga, mikurungu na mikongo ni mingi jaribu kuangalia uwezekano wa kuagiza kutokea huko maana bei zake kwa maeneo tajwa ni himilivu na usafiri ukitumia trc ni nafuu sana.
 
Back
Top Bottom