Wadau habari,
Mimi ni mgeni kidogo katika hili jukwaa.Kuna rafiki yangu ameoa na kujaliwa kupata watoto wanne,wameishi kwa amani kwa takribani miaka 8.
Sasa miezi kama mitatu iliyopita kuna tabia mke wake kaanzisha ya kuongea na mwanaume mwingine katika simu.Alipokutwa mara ya kwanza alijitetea kwamba ni mtu tu amepiga kwa bahati mbaya yaani kakosea no.
Hivyo akamweleza kuwa yeye kaolewa,cha kushangaza amekwisha kutwa na rafiki yangu zaidi ya mara mbili akiendelea kuwasiliana nae huyo mwanaume.
Mara ya mwisho rafiki yangu alimshirikisha mshenga na mkewe alikili amefanya kosa hivyo kuomba msamaha ila alisisitiza hawana mahusiano ya kimapenzi na huyo bwana.
Siku mbili baadae baada ya kunyang'wa simu amekutwa ameazima simu jirani na anawasiliana na huyo bwana tena.Sasa rafiki yangu ameomba nimpe ushauri kwani yeye anataka amwache huyu mwanamke.
Wadau naomba ushauri ili tunusuru ndoa hii.
Mimi ni mgeni kidogo katika hili jukwaa.Kuna rafiki yangu ameoa na kujaliwa kupata watoto wanne,wameishi kwa amani kwa takribani miaka 8.
Sasa miezi kama mitatu iliyopita kuna tabia mke wake kaanzisha ya kuongea na mwanaume mwingine katika simu.Alipokutwa mara ya kwanza alijitetea kwamba ni mtu tu amepiga kwa bahati mbaya yaani kakosea no.
Hivyo akamweleza kuwa yeye kaolewa,cha kushangaza amekwisha kutwa na rafiki yangu zaidi ya mara mbili akiendelea kuwasiliana nae huyo mwanaume.
Mara ya mwisho rafiki yangu alimshirikisha mshenga na mkewe alikili amefanya kosa hivyo kuomba msamaha ila alisisitiza hawana mahusiano ya kimapenzi na huyo bwana.
Siku mbili baadae baada ya kunyang'wa simu amekutwa ameazima simu jirani na anawasiliana na huyo bwana tena.Sasa rafiki yangu ameomba nimpe ushauri kwani yeye anataka amwache huyu mwanamke.
Wadau naomba ushauri ili tunusuru ndoa hii.