Una mke wako wa ndoa ya Serikali/Kanisani/Kimila na huenda Mungu amewajalia mukapata mtoto/watoto. Lakini katika ndoa yenu mkeo anataka arudiane na mpenzi wake wa zamani. Unamwambia nikupe Talaka anakataa lakini usiku wewe ukiwa umelala yeye analala sebuleni na anaongea mambo ya kimapenzi na huyo mpenzi wake wa zamani. Mke huyu utamwelewaje? Wazazi wake wamewakalisha kikao pia wakamshauri kama anataka kurudiana na mpenzi wake wa zamani hiyo biashara haipo. Wazazi wanamtambua mume wake wa ndoa na siyo mpenzi wake wa zaman.i Naomba ushauri wana JF.