Ushauri: kuanzishwe idara ya kupendezesha Miji na Majiji

Kamgomoli

JF-Expert Member
May 3, 2018
1,865
3,802
Ukweli ni kwamba miji mingi Tanzania inajegwa bila kuwa na ubunifu wa kuvutia hasa kwenye kudizaini bustani nzuri, minara, miti na maua pembeni mwa barabara nje na ndani ya miji.

Mara ingine mipango miji hupima vizuri na kutenga maeneo kama bustani lakini tatizo linakuja kwenye uendelezaji wa hizo bustani. Utakuta eneo limebaki wazi tu bila ya decorations za maana. Au unakuta barabara zinazotoka na kuingia ndani ya miji ziko tupu bila miti au bustani za maua pembeni mwa barabara.

Hivyo kama idara hii maalumu itaanzishwa jukumu lao kubwa litakua kuwashauri mipango miji, kufuatili maeneo ya wazi na kubuni mapambo ya miji huska, kutengeneza bustani nzuri, pembezo mwa barabara na hata kutengeneza minara ya miji.

Ni vema ukuaji wa majiji yetu ukaendana na uzuri wa madhari na sio kuzagaa kwa nyumba tu!

Hili nalo linahitaji USAIDS?

Haipendezi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unachokisema ni kweli mkuu mfano pale lugalo angalia panavyopendeza.

Bado hatujajua jinsi gani ya kuwatumia wafungwa kwa manufaa, hii ilitakiwa kuwa moja ya kazi zao.
 
Unachokisema ni kweli mkuu mfano pale lugalo angalia panavyopendeza.

Bado hatujajua jinsi gani ya kuwatumia wafungwa kwa manufaa, hii ilitakiwa kuwa moja ya kazi zao.
Kabisa.Mfano watu wenye kesi ndogo ndogo km wizi wa kuku,au simu wangepewa vifungo vya nje huku wakipewa kazi za kupanda miti, kumwagilia bustani n.k kuliko kuwarundika Segelea huku wakila msosi wa buree

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua tatizo tulilonalo na mipango miji mibovu linatokana na desturi zetu waafrika. Huwezi kuamini kwamba wakati wa ukoloni miji yetu ilikuwa mizuri zaidi kuliko ilivyo sasa. Hakukuwa na slums au miji isiyopangwa.

Unahabari kuwa sehemu nyingi za miji yetu zilizopangwa vizuri ni zile zilizopangwa na Wajerumani kabla ya 1920 na baadaye Waingereza kuanzia 1920 had 1961? Baada ya hapo tumebaki tunajenga hovyo hovyo bila mpango ndio matokeo ya kuwa na Manzese, Magomeni, Mbagala, n.k

Usitegemee sana rais aliyezailiwa kwenye kibanda cha nyasi au matope na haendi nje ya nchi kutembea ataweza kuona kwamba tuna tatizo la mipango miji. Yeye anaona kwamba tuna luxury ya ajabu!

Tujifunze kwa wenzetu Ulaya na America au angalua Abuja Nigeria walioanza kujenga mji mkuu mpya mahali ambapo hapakuwa na chochote. Tunavyojenga Dodoma kamwe hautakuwa mji mzuri. Tunahitaji watu kutoka nje watusaidie tuwalipe matrilioni ili kutupangia miji yetu. Hadi tutakapopata akili nzuri, tuendelee kumtukuza magu.
 
Tuna Rais ambaye akiona Machinga wamezagaa kando kando ya barabara et anazani ndo kukua kwa biashara. Vitu vya ajabu kabsa
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuna Rais ambaye akiona Machinga wamezagaa kando kando ya barabara et anazani ndo kukua kwa biashara. Vitu vya ajabu kabsa

Sent using Jamii Forums mobile app
La machinga na wapiga debe ndo linafanya miji iwe ya kiswahili. Sehemu za watembea kwa miguu kumejaa machinga, masoko yetu ya vyakula vizimba vipo ila kwenye maegesho nako mbogamboga zimepangwa chini.
 
Kama ningekuwa na mamlaka,kila mtu nwenye kiwanja mbele ya barabara ningemlazimisha apande miti na maua na avitunze

Kama huwezi achia kiwanja waje wanaoweza kupendezesha mazingira

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mbona hizi idara karibu ktk kila halmashauri wapo watu wa mipango miji........sema tunapuuziaga tu vitu kama mazingira na mipango miji..alafu dunia ya kwanza ndio vitu wanavyovipakipaumbele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…