Ushauri: Kipato changu ni kati ya 700k -1 milioni kwa mwezi

Sio lazima u save,unataka ku save ufanyie nini hiyo Pesa hilo ndio swali la kwanza?

Kama shida yako ni pesa ili ununue kiwanja, nenda kampuni wanazouza viwanja

chukua kiwanja uwe unalipa kila mwisho wa mwezi hela yako yote inaenda huko

ukimaliza deni kiwanja chako unacho! kiwanja kinaweza kua cha thamani hata ya 50m

lakini hujawahi shika 50m ya mara 1, lakini tayari una kiwanja chako.

AU

Unakiwanja unataka kujenga, Ushajua mahtaji ya nyumba yako,nenda hard ware iliyo karibu na site yako

wambie unalipia material then ukshamaliza kila kitu utakuja fata material yako,kila ukilipa unachukua risiti

kila hela unayopata mwisho wa mwezi peleka kwenye ile hardware, material yakitosha chukua gari nenda

kafate material yako yote peleka site Anza ujenzi,material yame cost zaidi ya 20m lakini ki uhalisia wewe bnafsi

hujawahi shka hata 10m ya mara 1,kwa hyo unaweza ukaona namna ya kufanya uka save pesa yako kwa namna hiyo

watu wanaweka hela bank kama hawana chakufanyia wakati huo,watu wana save kama hela haina kazi wakati huo

ila kama unajua una viporo kibao mbele yako,anza kuvipunguza kdg kdg kama nlivyotoa mifano hapo Juu kuja kushtuka

una vitu kibao vya maana na vya gharama lakini haujawahi hata siku 1 kumiliki pesa CASH yenye thamani ya mali unazomiliki.

Njia za ku save zipo nyingi hiyo nliyokupea mfano ndio njia ninayoitumia mimi kufanya maisha yangu,Haijawahi niangusha na wakati wote naonekana na pesa ila lait wangejua ninavyodunduliza,wangeufyata.
Mambo ya kudhurumika vipi
Maana unaweza ukawekeza mwenye store/ supplier/Duka akapata losse akafirisika ktk biashara zake inakula kwako
 
Mambo ya kudhurumika vipi
Maana unaweza ukawekeza mwenye store/ supplier/Duka akapata losse akafirisika ktk biashara zake inakula kwako
Ukiwa unaogopa hayo,Tunza mwenyewe pesa yako

uamuzi ni wako,ufanye hivyo au utunze pesa zako mwenywe

au utafute njia nyingine ya kufanya,hapo n wewe na serikali yako ya kichwa.
 
1. Fungua fixed account au malengo account
2. Kuna viwanja ambavyo wanaruhusu kulipa kidogo kidogo
3. Ingia kwenye kikoba cha kueleweka ambacho kitaku force uweke kiasi flani cha pesa mwisho wa mwezi
4. Fungua liquid account ya UTT
5. Nunua line ya simu mpe mama au mtu unayemuamini akushikie usimpe password uwe unaitumia hela, yani hakikisha io line iko mbali kuifata ni mtihani
6. Download expense manager app, itakusaidia kujua wapi unatumia pesa vibaya
7. Toa sadaka
8.Usikopeshe watu sio roho mbaya sema ukizingua hao hao ndio wa kwanza kukusema
SIjajua una position gani au nature ya industry uliopo ila huo mshahara unatosha sana kuweza kufikia malengo yako ukituliza kichwa.
Assume umepunguziwa mshahara, unalipwa 500K, ili io pesa nyengine inayobaki uweze kuitunza.
Pitia nyuzi zangu upate madini mkuu.
 
Jitahidi kupata mke saafi, ukipata huyo, akakushikia akili zako utatoboa.

Shida ipo kwenye kumpata sasa, hawa viumbe adimu kinoma😂
 
Usiweke kwenye investment account weka kwenye Saving account inayotoa riba kama bonus account then ikiwa nyingi itoe Kawekeze..!!!

#YNWA
Hii naitumia (ga) sana. Tena sikaagi na kadi. Mie niko Njombe, kadi ipo Babati.

Naandika (ga) kwa kidaftari kila niki-deposit.

Naamini kesho itakua poa.
 
Hii naitumia (ga) sana. Tena sikaagi na kadi. Mie niko Njombe, kadi ipo Babati.

Naandika (ga) kwa kidaftari kila niki-deposit.

Naamini kesho itakua poa.
Ikishakua nyingi usiiache bank.
Kawekeze sehemu.
Tena wekeza kwenye hobby yako.
Kama ni dereva chukua Bajaj/boda piga kazi.
Kama ni kilimo LIMA SANAA
Kama ni ..........

Na baada ya kuwekeza, endelea kutafuta elimu juu ya hilo jambo, uelewako usikudanganye kuwa unajua sanaa.

#YNWA

#YNWA
 
Back
Top Bottom