Ushauri: Jinsi ya kuanza maisha ya kujitegemea

Ushauri: Jinsi ya kuanza maisha ya kujitegemea

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
13,726
Reaction score
25,529
Wakuu,

Ndo kwanza naanza maisha mwenzenu, nimepanga chumba kimoja tu lakini changamoto niliyonayo hapa ni nini nianze kununua cha ndani?

Tushauriane wakuu
 
Nunua kile kinachoanza kuja kichwani mwako wakati unawaza

Be patient. The lessons you learn today will benefit you tomorrow.
 
Godoro...tena ununue lile imara maana vijana wakianza maisha huwa linatumika sana
Kweli mkuu
Wakati naanza maisha godoro ndo lilikua ni mahala pa kulalia, kukalia wakija wageni kwa wenyeji na mimi pia lakini pia ndo ilikua sehemu ya kupumzikia muda wote...
Namshukuru Mungu mwezi August linamaliza miaka 7 na bado ni zuriii tu nililihifadhi vizuri baada ya mambo kuanza kunyooka.
 
Chukua mkopo, nunua gari panga gest. hiyo ni mipango baada ya kuoa kwa sasa anza na godoro+mashuka+sufuria+jiko la mchina+ vyombo vya chakula+ndoo
 
Haha! JF taamu. Hata mtu akibanwa na ushuzi atauliza ajambie wapi. Ila wna JF hawana hiyana wanajibu kutokana na swali. Safi sana.
 
Kitanda,meza,tv,radio,
Vingne vtqfuata

[Color= yellow]Triple A[/color]
 
Back
Top Bottom