Kwa maelezo uliyotoa hapo, nakushauri usioane na huyu wa sasa muepushie matatizo, kuoana na mwanamke asiye na msimamo kama wewe ni matatizo makubwa maishani, kwa wengine ndoa ni mara moja tu haturuhusiwi kuoa mara ya pili. Nakushauri rudi tu kwa X wako kwa sababu huyu wa sasa haumpendi na hauko tayari kuishi nae katika ndoa.
Naona ameshapata ushauri mzuri tu toka kwa wadau hapo chini.
Ninachoweza kuongezea tu ni kuwa the devil is at work; na anamtumia huyo ambaye alikuwa too busy to look for you kuharibu familia (kanisa la kwanza) tarajiwa.
Sasa if she want to let the devil win, awasiliane na huyo X; lkn kama anataka kumshinda; basi afunge na kusali hizo nge za kijinga zitayeyuka kama barafu kwenye jua kali la kitropiki.
Wanajf habarini za jioni, naombeni ushauri wenu katika hili please maana sijielewi,
Mimi ni mdada mwenye mchumba na soon this year tunatarajia kufunga ndoa, kabla sijampata huyu mchumba nilikuwa na boyfriend ambaye tuliachana pasipo ugomvi na nadhani hii ilichanngiwa na distance tulokuwa nayo coz yy alikuwa mza kwa mda mrefu nami nikiwa dar chuo. Tulipoteza mawasiliano almost 5 yrs sasa hatujawasiliana. Last week dadangu alinipigia kuniarifu kuwa amekutana na my ex akiwa site kwake nje ya mji kdg ambapo dadangu naye anaishi huko, aliniambia kuwa my ex alimwomba namba yangu coz anataka turudiane na kwamba amenitafuta siku nyingi bila mafanikio but sister aliogopa kumpa coz anajua anaweza kuharibu hii mipango mingine. Tatizo langu ni kwamba tangu niliposikia habari zake nimejikuta kumpenda sana my ex natamani nionane naye yaani mawazo juu yake hayaishi kichwani mwangu najaribu kujisahaulisha but nashindwa. Wanajamii nisaidieni nifanyeje wapendwa?
Unaonaje akitembelea site ya Ex?
Hata kujuliana hali ni makosa!!
af wewe hebu lini unatembelea site yako!nimekumiss bana upo mtani wangu?
una akili wewe!Ndugu Yogati,
Natofautiana kidogo na baadhi ya wachangiaji kuwa wewe kueleza kuhusu 'site' ya mpenzi wako wa zamani ndiyo sababu tosha ya kukufanya 'umtake'..maana ninaitafsiri(ni ukaribu fulani ndani ya mji mmoja(city) wenye kukufanya utake kumuona kila leo! yaani kuwepo hapo jirani kunakufanya ushawishike zaidi kutaka kumuona kuliko alipokuwa Mwanza kama zamani.
Hata hivyo kuna vitu unapaswa kuzingatia.
1. Kwanini mliachana na huyo mpenzi wako wa zamani?
-Kusema kirahisi tu, kuwa, "tuliachana bila ugomvi" haimaanishi mrudiane!Umesema kuwa 'umbali' ulichangia, ikimaanisha kulikuwa na sababu hasa kuu na si umbali.
2. Hisia zisizoeleweka.
-Kunatofauti kati ya Kupenda , Kutamani, Kukosa(Miss), na kukumbuka.
Sijui unamaanisha nini kati ya hivyo..lakini iwapo utasema kuwa unampenda naomba ujiulize haya,
-Huko 'kupenda' unakosema, kulikuwepo kabla au kumeanza baada ya kuambiwa na dada yako?
-Iwapo ungeletewa taarifa kuwa bado anakupenda tena ukiwa umeshaolewa ungeendelea kumchukulia hivyo?
-Unategemea nini kwa mchumba wako wa sasa iwapo akijua kuwa unataka kuanzisha mahusiano based on hisia usizozielewa tena wakati wa uchumba?.
3. Tabia:
- Je, unajua huyo mpenzi wa zamani alikuwa na mwenendo gani?
-Iwapo anataarifa kuhusu ndoa yako(presuming,since kama anakupenda na kutaka mrudiane ameshakufuatilia na kujua), Unadhani atakuchukuliaje wewe hasa MSIMAMO wako kupitia suala tu la kutaka kuonana kwa haraka namna hiyo?
'Memories'..tulia, tazama unataka nini..kisha chukua uamuzi lakini so far, endelea na mipango yako ya ndoa maana yaliyopita si ndwele! Ukisema kila mtu amrudie mpenzi wake kwa sababu tu hawakuachana kwa ugomvi, kuna watu watamiliki mtaa/vijiji.
Goodluck.
una akili wewe!
unanidai dompo ujue!
Mngoni utamjua tu