Ushauri jamani

Yogati

Member
Joined
Jan 1, 2013
Posts
14
Reaction score
1
Wanajf habarini za jioni, naombeni ushauri wenu katika hili please maana sijielewi,
Mimi ni mdada mwenye mchumba na soon this year tunatarajia kufunga ndoa, kabla sijampata huyu mchumba nilikuwa na boyfriend ambaye tuliachana pasipo ugomvi na nadhani hii ilichanngiwa na distance tulokuwa nayo coz yy alikuwa mza kwa mda mrefu nami nikiwa dar chuo. Tulipoteza mawasiliano almost 5 yrs sasa hatujawasiliana. Last week dadangu alinipigia kuniarifu kuwa amekutana na my ex akiwa site kwake nje ya mji kdg ambapo dadangu naye anaishi huko, aliniambia kuwa my ex alimwomba namba yangu coz anataka turudiane na kwamba amenitafuta siku nyingi bila mafanikio but sister aliogopa kumpa coz anajua anaweza kuharibu hii mipango mingine. Tatizo langu ni kwamba tangu niliposikia habari zake nimejikuta kumpenda sana my ex natamani nionane naye yaani mawazo juu yake hayaishi kichwani mwangu najaribu kujisahaulisha but nashindwa. Wanajamii nisaidieni nifanyeje wapendwa?
 
Unampenda mpenzi wako mpya au ex wako? Chagua mmoja unaedhani unampenda zaidi uamue moja.

Sikushauri urudiane na ex wako, muda wake ulishapita na wala kigezo cha kusema mliachana bila ugomvi kisikupe kichwa. Uliamua kupendana na mwingine na hadi kufikia hatua ya kutangaza ndoa kwanini unataka kurudi nyuma?
 
Huna msimamo yaelekea! Mtaka vyote kwa pupa hukosa vyote! Km unategemea kufunga ndoa mwaka huu huyo wa zaman wa nn sasa? Go ahead na ulie naye!
 
Bado mwenye uamuzi ni wewe tu.
::
Je uko tayari kuwa na mume wako huku ukijuta moyoni kwa kumkumbuka ex-wako?
::
Je,ukienda kwa huyo ex wako,ukakuta kuna mwingine anaempenda uko tayari kuwa spare tyre?
::
Utendee haki moyo wako ila ujue kuna maumivu utayaacha kwa wa sasa,,na kuna maumivu ya mabadiliko makubwa utakayoyaona kwa ex wako.
ITS BETTER YOU FORGIVE AND FORGET
=
 
hahahahahahahah....unataka ushauri juu ya kuacha kumuwaza ex wako??..lolz?
Fanya hivi...Usithubutu kurudisha mawasiliano..(jitahidi ujiweke karibu na mumeo mtarajiwa kwa sasa)!
Kinachokusumbua kwa sasa ni 'memories' tu wala sio kwamba unampenda huyo ex...ni kawaida binadamu kukumbukia ya nyuma.....Jitahidi kwenye maisha yako kusonga mbele..ukiendekeza huu mchezo wa kwenda mbele hatua sita na kurudi nyuma hatua kumi hutakaa ufike aisee....Naomba wimbo wa 5 Clock in the morning wa T Pain ft Wiz Khalifa ukuburudishe....
 
Unamuwaza kwa sababu umembiwa na site , kwa hiyo anajenga, hahahahaa .......:becky::confused2:
Yaliyopita si ndwele ...........................!
 
Hapa jamaa anaoa galasa tu, hamna mke hapa. Sijui kwa nini tanzanian women mko pre occupied sana na mambo ya kuolewa. I wonder! mnapenda kuolewa na uzinzi mnautaka. Kwa nini usimalizane na uzinzi alafu uje utulie?
 
simple advice... mwambie huyu wa sasa about your true feelings, anaweza kukusaidia umsahau x wako au akuache ufuate hisia za moyo wako.
 
Hapa jamaa anaoa galasa tu, hamna mke hapa. Sijui kwa nini tanzanian women mko pre occupied sana na mambo ya kuolewa. I wonder! mnapenda kuolewa na uzinzi mnautaka. Kwa nini usimalizane na uzinzi alafu uje utulie?

full double standards alafu ukiwaomba bupa oh umeniona mie malaya
 
alafu inaelekea ex alikugegedaga vizuri na huyo wa sasa unataka kuolewa nae coz ana material things
 
dahhh Pole bana.

Ushauri wangu ni kwamba usije ukafunga pingu za maisha kama huna uhakika.
Kwa sasa huna uhakika na huyo ulie nae na pia ulimpoteza x wako kwa miaka 5.
Hujui alikuwa wapi, hujui alikuwa anafanya nini, hujui historia yake kwa muda wa
miaka 5.

sana sana utaamini tu atakacho kwambia, miaka 5 ni mingi sana na mambo mengi
yamebadilika ndani ya miaka hiyo. Je uko tayari kumuacha ulie nae na kwenda kwa
mtu ambae ulipotezana nae kwa muda wa miaka mitano?

Kingine cha kufikiria ni magonjwa.

usema kweli tutasema na kuandika mengi ila mwisho wa siku haya ni maisha yako
fuata moyo wako. Choose wisely.

Uzuri ni kwamba haya yametokea kabla hujafunga ndoa na wala huna familia na mtu wako wa sasa.

Kila lakheri ......
 

Atakuwa amesikia unaolewa ndio maana anakutafuta akuharibie usirudi nyuma .
 

Kwa maelezo uliyotoa hapo, nakushauri usioane na huyu wa sasa muepushie matatizo, kuoana na mwanamke asiye na msimamo kama wewe ni matatizo makubwa maishani, kwa wengine ndoa ni mara moja tu haturuhusiwi kuoa mara ya pili. Nakushauri rudi tu kwa X wako kwa sababu huyu wa sasa haumpendi na hauko tayari kuishi nae katika ndoa.
 
We kama ulishaamua kuendelea na maisha yako mpaka ukampata mwingine na kupanga nae mipango ya ndoa ni bora tu umsahau huyo X nomatter what good memories you have about him, u have decided to move on then do it never look back cz huyo X unae muwaza possibly si yule uliekua ukimfahamu 5yrs ago mengi kuhusu yeye yatakua yamebadilika na pindi utakapo wasiliana nae na kujikuta upo nae katika mahusiano tena itakua too late to turn back, kwahiyo we fanya mpango umpotezee tu ukutane nae ukiwa ushafunga ndoa na huyo current guy wako atakuheshimu kama rafiki na uondoe hisia zozote za kimapenzi juu yake.
 
Ukitaka kukutana na ex wako uwe tayari kuachana na mchumba wako wa sasa. Ukianzisha mawasiliano na ex wako unategemea kupeleka wapi uhusiano wenu? Hamuwezi kuwa marafiki kama ma-ex bila mchumba wako kufahamu. Mahusiano yenu yaliisha kirahisi sana miaka mitano iliyopita ambayo ni mingi mno. Huyo jamaa muongo hajakutafuta siku nyingi, ni basi tu alikutana na dada yako. Alifanya vizuri kutokumpa namba yako.

Kama bado una second thoughts kuhusu ndoa yako bora umwambie mwenzako kabisa kabla hamjafunga pingu za maisha.
 
Je kuna namna yoyote ufanisi wake hasa site unachangia kujisikia ujisikiavyo? Je umesema yote kuhusiana na hili penzi la ghafla au kuna uliyoficha? Je kama hamkuachana zaidi ya kuishi mbali ilikuwaje ukakubali kuwa na BF mwingine? Je ilikuwaje ukakubali hata kuchumbiwa? Je ikitokea ukaachana na huyu mchumba wako na ukaolewa na huyo BF wako wa zamani na siku moja ukakutana na huyu mchumba wako ukajisikia kama unavyojisikia itakuwaje?Je unaweza kuwa mkweli au tuseme muwazi zaidi? Je unataka tukusaidieje iwapo majibu yote unayo wewe? Je fikiria huyo mchumba wako angekuwa anakufanyia au kukutana na GF wake wa zamani na akajihisi kama unavyojihisi na ukajua ungefanya nini? Je wajua mkuki ni kwa nguruwe? Nadhani uamuzi unao wewe kwa vile yakigarambuka atayeumia ni wewe siyo sisi.
 
Ngoja nikuitie baadhi ya specialists kwenye hiyo sector ya ushauri wa hapa MMU:

gfsonwin
Kaunga
snowhite
Naona ameshapata ushauri mzuri tu toka kwa wadau hapo chini.
Ninachoweza kuongezea tu ni kuwa the devil is at work; na anamtumia huyo ambaye alikuwa too busy to look for you kuharibu familia (kanisa la kwanza) tarajiwa.

Sasa if she want to let the devil win, awasiliane na huyo X; lkn kama anataka kumshinda; basi afunge na kusali hizo nge za kijinga zitayeyuka kama barafu kwenye jua kali la kitropiki.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…