Ushauri: Dada yangu ananiomba sana Pesa

Kama hana chanzo basi wewe ndio chanzo chake
 
Ina maana wanaume wameisha tz? Mambo Mambo gani haya
 
Ndugu huwa wanapenda Sana uwasaidie pindi ukiwa na kipato, ila siku ukiyumba na ukakipoteza kile kinacho kupa kipato haohao ndo huwa wanasema alikua na kazi ila hana cha maana alicho fanya wanasahau wema wote.
Saidia unapoweza tena iwe kwenye mambo ya maana tu,, ukiona msaada unaoutoa unakufanya uumie usisite kuwajibu Sina hela
 
Mmhh acha kumjaza mwenzio upepo .. Kumsaidia mtu anaye jiweza ni baraka au ni kuangushana tu kiuchumi !?
Binafsi ninapomsaidia mtu siangalii anajiweza au hajiwezi natoa msaada pale inapohitajika
 
Wewe binadamu huwajui vizuri
Ndo maana nimekuambia ninamsaidia mtu
pale ninapoona ana sababu za kusaidiwa pasipo kuangalia kama anajiweza au la! Hata hao wanaojiweza kuna wakati wanakwama ile mbaya so siwezi kuacha kumsaidia mtu kwa sababu anajiweza.
Kwangu Mimi kusaidia kuna mibaraka sana
 
Wewe msaidiye tu, ila siku ukikwama ndiyo utamjua vizuri, na siku ukioa ukawa na majukumu yako mengi na kushindwa kumsaidia kama hivi sasa, lazima mkeo wampopoe tu na kumuona mchoyo maana kabla hujamuoa ulikuwa ATM sasa tangia umlete huyo mnyamahanga umebadilika sana.

Hakuna tabia nisiyoipenda kama yakuomba omba hovyo, sasa kama ana Mme na biashara anayo sasa umatonya wanini kwa Kaka yake!
 

Kwel kabisa
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…