Ushauri: Baba mzazi

Ushauri: Baba mzazi

Pole sana kwa masaibu yaliyokukuta, kweli inauma sana kutokumjua baba yako mzazi.
Lakini jaribu kuongea na baba mlezi akusaidie na hata mama lazima anawajua ndugu ya baba yako mzazi na akikuambia hao ndugu hapo ndio pa kuanzia

Lazima wakuelewe kuwa upo kwenye wakati mgumu sana wa kushindwa kujizuia na kumjua baba yako halisi.
Nakuombea kila la kheri umpate hata kumjua tu
Damu nzito sana hata yeye anajutia hilo na hana furaha huko aliko na ninatumaini siku mkikutana atafurahi sana haijalishi ni miaka mingapi
Nakupa pole tena na ujue moja tu kuwa dunia hii ina mambo mengi sana
 
Mdogo wangu nikushauri kitu? Baba yako ni huyo aliyekulea, huyo mwingine si Baba yako ila ni mzazi mwenzie na mama. Angekuwa Baba yako angejali uwepo wako duniani.

Umeishi Kwa Amani na furaha Kwa miaka 24 bila Ku notice tofauti yoyote sasa mazungumzo ya dakika 5 na mama ndio yakukoseshe Raha kiasi hicho?

Usilivalie njuga swala la kumtafuta Baba mzazi. Lisipoteze furaha na Amani yako. Mtafute pole pole Tu wala si Kwa pressure, ikiwa ukamuona Sawa usipomuona Sawa pia.

Nakushauri Sana mshirikishe huyo Baba mlezi kila hatua unayochukua kumtafuta Baba yako. Ikiwa hatopenda Jambo Hilo (kitu ambacho sidhani) basi chukua tahadhari Sana ikiwezekana achana nalo.
 
Ongea na mzee hapo home akupe ushauri pia....
 
Sidhani kama iko haja ya wewe kuwa na msukumo mkubwa namna hiyo wa kumtafuta huyo baba yako mzazi. Unachotakiwa kufanya, ni kutuliza akili na kuacha mwaka mmoja upite ndipo uanze mchakato wako.
Ukianza mapema namna hiyo, huyo mlezi wako atapunguza upendo na kusitisha mipango aliyonayo kwako. Tulia kijana kwani utakuwa na muda mwingi wa kumtafuta na kumpata mshua.
 
Hili suala usilichukulie poa sana. Tuliza akili zako kabisa. Usije ukabadili taswira ya malezi yako kutoka kwa baba yako mlezi. Utamvunja moyo baba yako aliyekulea toka utotoni mwako, usipokuwa makini.

Fikiria, baba mlezi alimkubali mama yako bila kujali ni single mother, tena aliyekuwa tayari ameshaolewa akaachika na bado akakubali kukulea hadi sasa 24 yrs! Na bado hakuweza kukutenga wala kwa chochote.

Utakapojitegemea utaanza hizo harakati zako kijana.

Fikiri kabla ya kutenda.
 
Hili suala usilichukulie poa sana. Tuliza akili zako kabisa. Usije ukabadili taswira ya malezi yako kutoka kwa baba yako mlezi. Utamvunja moyo baba yako aliyekulea toka utotoni mwako, usipokuwa makini.

Fikiria, baba mlezi alimkubali mama yako bila kujali ni single mother, tena aliyekuwa tayari ameshaolewa akaachika na bado akakubali kukulea hadi sasa 24 yrs! Na bado hakuweza kukutenga wala kwa chochote.

Utakapojitegemea utaanza hizo harakati zako kijana.

Fikiri kabla ya kutenda.
Ushauri makini sana.
 
Wanasemaga mtoto wa mwenzio mbebe akiwa kalala akiamka atamtafuta mzazi wake....
Kwa busara ongea na baba kaa nae mzungumze kiume, ila sijui hata atalipokeaje pole sana.

naanza kuelewa kwanini kina mama wengine huwa hawataki kusema ukweli kwa situation kama hii naona inaleta vurugu tu na kuondoa amani iliotawala kipindi chote cha kupiga kimya.
 
Wanasemaga mtoto wa mwenzio mbebe akiwa kalala akiamka atamtafuta mzazi wake....
Kwa busara ongea na baba kaa nae mzungumze kiume, ila sijui hata atalipokeaje pole sana.

naanza kuelewa kwanini kina mama wengine huwa hawataki kusema ukweli kwa situation kama hii naona inaleta vurugu tu na kuondoa amani iliotawala kipindi chote cha kupiga kimya.
Kweli kabisa

Naamini dogo asipotumia busara na akili ataivuruga amani iliyopo.
 
Tulia kabisa usiwe na papara fanya kama hakuna ulichokijua ipo siku mama yako atakwambia tu fanya kila hali hakikisha una maisha yako hutegemei wazazi mana kuna uwezekano ukavuruga kila kitu
 
Waliokushauri hapo juu imetosha kabsa unaweza ukaufuta uzi kabsa
 
Kwanza ulivyosimulia nimejifunza mama ako hana roho mbaya maana ungekuwa na wamama wengine ungekuwa unamchukia baba yako kwa chuki za kupandikizwa na mama yako..

Pili,Dogo tafuta maisha kwanza baba ako atakutafuta mwenyewe Ni ushauri wa kijinga ila case nyingi sana wazee wanawafuata watoto maisha yao yakiwa mazuri.
 
Kumjua tu sioni tatizo.... Mtafute tu umjue
 
Mkuu fuata ushaur wa wadau huko juu nafikir wameongea mengi but kuna mdau kasema utapofanikiwa tu baba yako atakutafuta mwenyewe mfano kiba diamond, ommy dimpoz na wengine wengi sana
 
Back
Top Bottom