Ushahidi Watz tuna IQ Ndogo!

Mkuu unachosema ni ukweli..

Hapa TZ sio IQ tu ni tatizo, hata elimu tunayosoma ni ya 20th century, then tunategemea watu wafikiri ki-21st century??...


Our minds are very slowly in process things.. and we are too slowly in understanding issues... Then, what do you expect??
 

Utailaumuje IQ?
Ili iweje?
...
Ivi umeisoma vizuri concept ya IQ?
Kulia lia kwa Wazenji ndio kumekufanya useme wanaIQ kubwa?
...
Na jee unazungumzia nini kuhusu EQ ktk suala zima la maendeleo?
 
Watanzania wote tuna IQ ndogo! Hapo napinga kaka si kweli. Pia ninashaka na takwimu zako kama kweli zanziba inawatu mil. 1! Ninavyojua mimi wanazidi mil moja. Suala la Zanzibar ni gumu, tena usifikiri wakati mwingine viongozi waandamizi kufumba mambo kwa baadhi ya mambo wanayotufanyia wazenji ni wajinga, la hasha! Wanalinda muungano, pia wanawabembeleza wazenji muungano usife kwa sababu ya sababu.
 
Nadhani swali lako la msingi lingekuwa nini "strategic interest" ya Tanzania" huko visiwani. Hata kama ungejiuliza hivyo ningekushangaa kwani suala la Interest hizo limekuwa likizungumziwa kila siku kuanzia enzi ya Baba wa Taifa mpaka sasa. Usidhani wewe peke yako ndo una IQ kubwa kushinda hao walioliona hili na wanaoendelea kupigania hili mpaka sasa. Pili sidhani kama IQ ya Watanzania inapimwa kwa suala hili tu. Mbona umeacha mengi ambayo huenda yakawa mazuri kwako kuliko hili.

 
Ushahidi mwingine hu hapa:-
  1. Pesa za maendeleo nchi hua hazipo lakini linapokuja suala la kujadiri mambo ya siasa pesa hua zipo na kubaki.
  2. Pamoja na madhambi mengi na uongo mwingi hata na ahadi ambazo hua hawatekelezi ccm, bado Watanzania wanawachagua, mfano iliahidiwa kwenye kampeni za Mkapa 1995 kwamba atahakikisha kila wilaya (makao makuu ya wilaya) yatakua na umeme, hadi anaondoka madarakani hilo bado halijatekelezwa hadi leo.
  3. Tunafundisha watoto wetu kua eti makao makuu ya Tanzania yapo Dodoma while serikali yote ipo Dar na watu wote wanajua hivyo but still tunaamini tofauti.
  4. Tuna amini kua Tanzania ni muungano wa nchi 2, Tanganyika na Zanzibar, Zanzibar bado inaishi while Tanganyika imekufa, huyo huyo anaeishi bado anadai haki kwa mfu (though kwa mleta uzi gili haoni kama ni tatizo) hili bado mimi linanisumbua hadi leo.
  5. Mtu anagombea urais, tena ame faight for 10 years halafu akiulizwa kwanini nchi yako ni masikini wakati ina kila kitu na yeye anasema hata yeye haujui lakini akigombea tena, hata waliomsikia akisema kwanini nchi yetu ni masikini bado wanamchagua.
  6. Tuna amini kua, ukiwa na mikoa mingi pamoja na wilaya nyingi ndio kupeleka maendeleo kwa wananchi.
  7. ............
  8. ..........
  9. ............
 

nina wac wac na majbu yako. hng kong watu ml. 7? cna uhakika sana na jbu lako japo nimeish pale mda mrefu ngoja niingie kwenye web yao
 

kijakazi wa II,bila shaka wewe ndio una Iq ndogo.
Nani alikwambia ukubwa wa eneo una guarantee nguvu na hadhi ya nchi husika?
Kama ndivyo,si DRC ndio wangekuwa matajiri kuliko wote Afrika?
 
Last edited by a moderator:

Sijajua upembuzi wako umezingatia nini! Kuhusu aldhi ndogo labda profession yako inakubana, ardhi ina value, inawezekana value ya ardhi ya Zenji ni kubwa! Sijui kama ulizingatia hilo katika kupima IQ! Mbona oysterbay ardhi ni aghali wakati kuna poli kbala ya mikumi ambalo halina mtu,IQ yako ilikupitisha huko?

Kwanini kama Mzanzibari ana uwezo wa kununua na kumiliki ardhi Kariakoo ambako hakuna ardhi, na mTangnyika asinunue na kumiliki huko? IQ imekupitisha huko? Au wazo alako ni kuwa kwakuwa Zanzibar hakuna ardhi ya kutosha basi iwe haki ya Wazanzibari ila huku ambako kuna ardhi ya kutosha iwe yetu wote? IQ yako inakuongoza hivyo? na Kariakoo kusiko na ardhi je? na Tandika? Angalia IQ yako mkuu!
 

7. Tunaamini wawekezaji kutoka nchi za nje kuliko watz wenyewe
 
amekosea kidogo kwa kutolea mfano wa zanzibar na tanganyika, lakini point yake ya kuwa asilimia kubwa ya watanzania tuna IQ ndogo ni ya kweli na kuna research zimefanyika ambazo zinaonyesha kuwa 42% ya watanzania waliwahi kuugua utapiamlo wakati wa utoto wao, harafu kuna wale ambao wametoka kwenye familia zenye uwezo lakini mtoto anakuwa mvuta bangi, petrol, madawa ya kulevya au hata unywaji wa gongo, na kuna wale wanaozaliwa na upungufu wa akili bila kujalisha uwezo wa wazazi wao, sasa hao wote ukiwajumlisha utapata karibia 60% ya watanzania wana uwezo mdogo sana wa kufikiri. ndiyo maana utakuta kiongozi wa ngazi ya juu anaropoka kitu ambacho wewe mwenye akili ukikisikia unabaki kinywa wazi, na usijaribu kumkosoa maana anaweza kukuumiza.
 
@SAIZI YANGU akili yako ni sawa na jamaa anaitwa Olonyoike Ole-Sendeka?
Dunia nzima ni ndugu na Afrika ni moja
kwa nini unaing'angania Zanzibar uitawale? ba kututisha Issue ya Zanzibar sensitive unachoogopa ni nini Obama na Mrusi watatuvamia (akili ya kizamani)
Huwezi linganisha UK na Falkland ya Ajentina kwanini basi usikitawale kisiwa cha Comoro
Km kuungana si tuungane na Rwanda au Burundi maana Watanganyika wengi tuna Nasaba nao
Kilimanjaro mlima wote ulikuwa Kenya, mpaka ilipotokea Wajerumani wakampa Malkia Victoria km zawadi ya Birthday
Hayamabadilishano hayakuishia hapo tu na mwingereza kwani hata Ziwa Nyanza , Bandari ya Mombasa na Tanga vilikuwa katika mvurugano huo
Miaka 50 ya Muungano imetutesa sana na wala hiyo HATI YA MUUNGANO hatujaisoma acheni iwekwe hadharani tuone makosa na kila mtu abaki na Nchi yake.
Watanzania tuna tabia za woga au kushikiwa ndio maana nakubaliana tukiambiwa tuna IQ ndogo
Huko ndani ya CCM ni nani hasa anayeshinikiza kuwa na Serikali 2 maana hata Mwenyekiti alishasema kubalini mabadiliko
RUSSIA imesambaratika
UJERUMANI iligawanyika na sasa nchi moja
KOREA ilikuwa moja ikasambaratika
Wapeni Wazanzibar Nchi yao wajitawale hakuna haja ya Nchi 1 wala 2 wala 3
 
mwenye iq ndogo ni wewe peke yako na wenzako wachache. Kila anaeuliza swali au kubisia kitu fulani ana sababu zake. Cha muhimu jibu na jadili hoja na si watoa hoja. Kwa taarifa yako kuna mtanzania tena mtanganyika wa Lushoto ana iq kubwa kuliko NEWTON,ARISTOTLE,CORPENICUS,ARCHMEDES nk.Ni basi tu wa tz hatujui kusifu kilicho chetu. Anaitwa Erasto Mpemba. Just google:MPEMBA EFFECT.
 
Ujumbe wako ni wa kweli kabisa na hauwezi kupungunga wabunge wetu huchukua siku nzima kujadili kitu kama hicho ni aibu sana mi hufikiri huenda wakipeleka muda ili siku iishe wasaini posho basi maana kiakili haiji kabisa.
 
Kwani wewe unadhani Tanganyika ndiyo inataka Muungano peke yake? Kuna wazanzibari wengi tu wanataka muungano. Umuhimu wa muungano (Bila kujali serikali ngapi) sina haja ya kuuelezea maana dunia nzima sasa ina focus katika kuungana. Usitolee mfano wa USSR, kwani kuna wajanja walitaka kuuza umoja wao kwa kuimaliza USSR. mbona huzungumzii Political federation ya East Africa? mbona huzungumzii issue ukuaji wa NATO, huzungumzii kuziingiza Rwanda na Burundi katika EA? Hayo yote yanatokana na ukweli kuwa wenye kuona mbali wanajua umuhimu wa kutatua matatizo kwa pamoja. Na ieleweke issue siyo kutawala bali ni kuungana. Pili mfano wa Ujerumani unathibitisha dhana ya umuhimu wa umoja kuliko kuwa na nchi mbili kama ilivyokuwa awali.

 
Mzizi wa hoja aliyoitoa ni suala la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sina data za IQ, hivyo siwezi ku-comment chochote.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…