Hata miji hauna unaandaa ugaidi mzee
Kivutio kikubwa duniani ni miji iliyopangwa na kujengwa kwa ufasaha (na siyo wanyama na milima). Kuna jitihada mbalimbali zimefanyika na mipango jiji la DAR ES SALAAM/ZANZIBAR ili kuhakikisha inakuwa kama Dubai lakini tukaambulia kuwa na majengo ya ovyo na kujenga nyumba ndogo ili ipo siku tutabomoa na kujenga Gorofa ambapo kwa uhalisia/kiasi kikubwa tunapoteza sumenti nyingi/mchanga mwingi/Gypsum/mapati (steel), kutokuwa na mifumo ya majitaka/maji safi, kusababisha foleni/uchawi n.k.
Aidha, hali hii inajidhihilisha kwenye majiji yote ya Tanzania (ikiwemo mbeya, Iringa, Arusha) kwa kuwa na vyoo kibao kila nyumba, barabara zisizo tengenezeka wakati tunaweza kutumia zege na kuwa na balabala njema kabisa. Kwa hali inavyokwenda tutafika miaka 100 tukiwa na dreams za kwenda kuangalia miji mizuri na iliyopagwa tutakaposafiri kuelekea ulaya/dubai/china. Bila kujiuliza ilijengwaje?
Kama ukijiuliza hili swali ndipo utakapo jua kuna haja ya watanzania kutenga miezi miwili (happy month) kwa kila mwaka kwa ajili ya watu kufanya mazoezi ya kujenga miji ambayo itahakikisha ramani ya mipango inatekelezwa kikamilifu. Ambapo, Serikali inatenga fungu/fedha za kujenga miji (labda kama mafundi wanataka kuchezea tope milele maana nyumba hazina lifespan) na kila mtu anajua kuwa Serikali haifirisiki kwani ipo vizuri kuzungusha fedha kwa njia ya kodi na tozo na viwanja ni vya Serikali.
Maisha ni mipango miji.