Awali nilizani zoezi la kusajili namba za simu ni kitu serious ambacho kingehitaji watu (wasajili) makini kumbe sivyo! Nimesajili namba 3, za tigo 2 na voda moja. Tigo ya kwanza ingawaje nimesajili zamani kabisa kabla ya foleni, lakini jana naulizia taarifa zangu naambiwa namba yangu haijasajiliwa na hivyo nitume upya jina na namba ya fomu!! Nikafanya hivyo jana, na leo nilipoulizia taarifa hizo,nikapewa jibu lile lile-kwamba sijasajiliwa!!!!! Nilipohitaji taarifa za namba nyingine ya hao hao tigo ambayo nimeisajili majuzi; nikajibiwa nimesajiliwa. Hata hivyo, taarifa nilizotumiwa (jina na namba) ni tofauti kabisa!!!! Kwa maana nyingine, kwa upande wangu ingawaje nimejisajili lakini zoezi hilo lime-fail kwa 100% !!!! Nilihitaji taarifa kutoka Vodacom, wao waliishia tu kusema nimesajiliwa vizuri kabisa lakini bila kunitumia taarifa zangu ambazo ningezihakiki!!!! Sina hakika, labda wasajili wa Vodacom hawakosei!!!!! The question follows, TCRA washasema kwamba wasiosajiliwa namba zao zitafungwa; sasa kwanini mtu kama mimi nifungiwe kwa uzembe wa service provider?! On the otherhand, ile namba ambayo taarifa zake sio sahii,endapo nitaitumia ndivyo isivyo, sio ataingia matatani mtu ambae wao ndie wameandika habari zake wakati sio?! Sasa nini maana ya zoezi zima hili?! Ni nani wa kulaumiwa? Ingawaje zoezi hili linaonekana muhimu lakini hata wasajili tulionao huku uswahilini wala hawaonekani kama ni watu makini!!! USHAURI KWA TCRA; wala msiharakie kufungia namba za watu kabla uhakiki haujafanyika!!!