Usahihi wa tafsiri ya Sheria ya Ardhi na mamlaka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Regnatus Cletus

JF-Expert Member
May 26, 2018
1,114
958
Nimeshawishika kupachika bandiko hili baada ya upotoshaji unaofanywa na mwanajamvi mwenzetu ndugu Barbarosa.

Kama mdau wa sheria, nimeumizwa, na nikapata msukumo wa dhati wa kuliweka jambo hili sawia ili kuzuia udanganyifu wa makusudi.

SHERIA YA ARDHI YA MWAKA 1999, YAANI THE LAND ACT ; KIFUNGU CHA NNE (1) KINASEMA, " ALL LAND IN TANZANIA SHALL CONTINUE TO BE PUBLIC LAND AND REMAIN VESTED IN THE PRESIDENT AS TRUSTEE FOR AND ON BEHALF OF ALL CITIZENS OF TANZANIA.

Kwa lugha ya Kiswahili ni kuwa, "Ardhi yote ya Tanzania itabaki kuwa ardhi ya Umma, na itakabidhiwa kwa Rais kama msimamizi kwa niaba ya watanzania wote.

HIVYO, si kweli kama asemavyo Barbarosa kuwa Ardhi ya Tanzania ni mali ya Rais, na sisi ni wapangaji wake. Rais ni msimamizi wa ardhi yetu watanzania.

KIFUNGU CHA 3 CHA LAND ACQUISITION ACT, YA MWAKA 1967, Kinampa mamlaka Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuichukua ardhi kwa matumizi ya umma.

Na matumizi hayo ya umma yamebainishwa kwa viwango vinavyodhibiti tafsiri yake (it is strictly construed)..... Yaani kuwa matumizi hayo ya umma sharti yawe, aidha kwa shughuli za kiserikali, shughuli za kitaifa, miradi, kilimo, viwanda, biashara, usimikaji wa miundo mbinu, na uchimbaji wa madini.

MATUMIZI YA UMMA SIO TU KWA MATAKWA AU UTASHI BINAFSI KAMA ANAVYOTUELEZA BARBAROSA. MATUMIZI YA UMMA YAMEBAINISHWA KATIKA UTARATIBU WAKE.

IBARA YA 24 (2) YA KATIBA YA JAMUHURI YA TANZANIA INASEMA, "IT SHALL BE UNLAWFUL FOR ANY PERSON TO BE DEPRIVED OF HIS PROPERTY FOR THE PURPOSES OF NATIONALIZATION OR ANY OTHER PURPOSES WITHOUT THE AUTHORITY OF LAW WHICH MAKES PROVISION FOR FAIR AND ADEQUATE COMPENSATION.

Yaani kwa Kiswahili , " ITAKUWA NI KINYUME NA SHERIA, KWA MTU YEYOTE KUNYANG'ANYWA MALI YAKE KWA MALENGO YA UTAIFISHAJI AU MALENGO MENGINE YOYOTE BILA MAMLAKA YA KISHERIA YANAYOWEZESHA FIDIA TOSHELEZI NA YA HAKI".

KIFUNGU CHA 11 CHA "LAND ACQUISITION ACT" YA 1967, KINAMTAKA RAIS AU WAZIRI WA ARDHI KULIPA FIDIA KWA WOTE WALIOCHUKULIWA ARDHI ZAO KWA AJILI YA MATUMIZI YA UMMA. FIDIA HIYO LAZIMA IWE FIDIA TOSHELEZI NA YA HAKI. WATU HAO WANAWEZA KUFIDIWA FEDHA TASLIMU AU KWA KUPATIWA VIPANDE VINGINE VYA ARDHI.

NDUGU WANAJAMVI, TUSIPOTOSHWE NA WATU WACHACHE WENYE MALENGO NA NIA OVU.
 
Bado sheria hizi zinahitaji marekebisho ili kuruhusu urahisi wa uwekezaji mkubwa kwenye miradi mikubwa kama ya Kilimo.
In real sense, nobody will simply trust such kinds of beauracratic land acts in a matter like investing trillions of shillings in lets say irrigated agriculture. Fear comes in where detitling of that established land is done by one person and probably its an overnight decision,and on top of that it may be politically biased.
 
Bado sheria hizi zinahitaji marekebisho ili kuruhusu urahisi wa uwekezaji mkubwa kwenye miradi mikubwa kama ya Kilimo.
In real sense, nobody will simply trust such kinds of beauracratic land acts in a matter like investing trillions of shillings in lets say irrigated agriculture. Fear comes in where detitling of that established land is done by one person and probably its an overnight decision,and on top of that it may be politically biased.
Good point mkuu, heshima yako.
 
Bado sheria hizi zinahitaji marekebisho ili kuruhusu urahisi wa uwekezaji mkubwa kwenye miradi mikubwa kama ya Kilimo.
In real sense, nobody will simply trust such kinds of beauracratic land acts in a matter like investing trillions of shillings in lets say irrigated agriculture. Fear comes in where detitling of that established land is done by one person and probably its an overnight decision,and on top of that it may be politically biased.

Sheria zimewekwa vizuri sema hazifuatwi. Rais au waziri anapaswa kufuata masharti ya sheria za nchi ila tatizo wanajitwalia twalia tu kinyume na Sheria. Ukitaka kuchukua ardhi ya kijiji lazma ngazi zote zishirikishwe kuanzia chini (Soma VLA)... Tatizo bongo hawafuati sheria. Labda tutunge sheria Ili kulinda sheria zetu, nani atunge? Ccm ya watawala na watawala wa ccm hakuna anayeweza kuleta sheria ya yeye kujisulubu.
 
Ili watawala wafuate sheria, cha kwanza ni kuuondoa katiba ya mwaka77.
Hii katiba imemfanya rais kuwa msaidizi wa karibu wa 'Mungu'.
Yaani msululu wa sheria zooooote then katiba ikaja kumpa mamlaka rais ya kufanya ' jambo lolote bila ya kushauriana na yeyote'... Huu ni msingi wa upuuzi wote. Mahakama hata ifanye nn, hata bunge lifanye nn rahisi kupewa mamlaka ya kutengua. Rejea kusamehe wafungwa anaowataka
 
Nimeshawishika kupachika bandiko hili baada ya upotoshaji unaofanywa na mwanajamvi mwenzetu ndugu Barbarosa.

Kama mdau wa sheria, nimeumizwa, na nikapata msukumo wa dhati wa kuliweka jambo hili sawia ili kuzuia udanganyifu wa makusudi.

SHERIA YA ARDHI YA MWAKA 1999, YAANI THE LAND ACT ; KIFUNGU CHA NNE (1) KINASEMA, " ALL LAND IN TANZANIA SHALL CONTINUE TO BE PUBLIC LAND AND REMAIN VESTED IN THE PRESIDENT AS TRUSTEE FOR AND ON BEHALF OF ALL CITIZENS OF TANZANIA.

Kwa lugha ya Kiswahili ni kuwa, "Ardhi yote ya Tanzania itabaki kuwa ardhi ya Umma, na itakabidhiwa kwa Rais kama msimamizi kwa niaba ya watanzania wote.

HIVYO, si kweli kama asemavyo Barbarosa kuwa Ardhi ya Tanzania ni mali ya Rais, na sisi ni wapangaji wake. Rais ni msimamizi wa ardhi yetu watanzania.

KIFUNGU CHA 3 CHA LAND ACQUISITION ACT, YA MWAKA 1967, Kinampa mamlaka Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuichukua ardhi kwa matumizi ya umma.

Na matumizi hayo ya umma yamebainishwa kwa viwango vinavyodhibiti tafsiri yake (it is strictly construed)..... Yaani kuwa matumizi hayo ya umma sharti yawe, aidha kwa shughuli za kiserikali, shughuli za kitaifa, miradi, kilimo, viwanda, biashara, usimikaji wa miundo mbinu, na uchimbaji wa madini.

MATUMIZI YA UMMA SIO TU KWA MATAKWA AU UTASHI BINAFSI KAMA ANAVYOTUELEZA BARBAROSA. MATUMIZI YA UMMA YAMEBAINISHWA KATIKA UTARATIBU WAKE.

IBARA YA 24 (2) YA KATIBA YA JAMUHURI YA TANZANIA INASEMA, "IT SHALL BE UNLAWFUL FOR ANY PERSON TO BE DEPRIVED OF HIS PROPERTY FOR THE PURPOSES OF NATIONALIZATION OR ANY OTHER PURPOSES WITHOUT THE AUTHORITY OF LAW WHICH MAKES PROVISION FOR FAIR AND ADEQUATE COMPENSATION.

Yaani kwa Kiswahili , " ITAKUWA NI KINYUME NA SHERIA, KWA MTU YEYOTE KUNYANG'ANYWA MALI YAKE KWA MALENGO YA UTAIFISHAJI AU MALENGO MENGINE YOYOTE BILA MAMLAKA YA KISHERIA YANAYOWEZESHA FIDIA TOSHELEZI NA YA HAKI".

KIFUNGU CHA 11 CHA "LAND ACQUISITION ACT" YA 1967, KINAMTAKA RAIS AU WAZIRI WA ARDHI KULIPA FIDIA KWA WOTE WALIOCHUKULIWA ARDHI ZAO KWA AJILI YA MATUMIZI YA UMMA. FIDIA HIYO LAZIMA IWE FIDIA TOSHELEZI NA YA HAKI. WATU HAO WANAWEZA KUFIDIWA FEDHA TASLIMU AU KWA KUPATIWA VIPANDE VINGINE VYA ARDHI.

NDUGU WANAJAMVI, TUSIPOTOSHWE NA WATU WACHACHE WENYE MALENGO NA NIA OVU.
Cletus umefnya vizuri, lkn kwa hawa wa Lumumba achana nao, either ni mbumbumbu au wanafanya makusudi. It is very unfortunate we have a doomed judiciary! haiwezi kutoa hukumu ya haki kuhusu haya mambo kama ikitokea kesi sasa hivi inayohusu haya mambo.
Barbarosa ni mwanamke, nadhani mawazo yake yanatawaliwa na ile kitu.
For reference soma kesi hii ambayo CA ilidefine public interest in land
 

Attachments

  • PUBLIC INTEREST DEFINED BY CA TANZANIA.pdf
    249.1 KB · Views: 23
Cletus umefnya vizuri, lkn kwa hawa wa Lumumba chana nao, either ni mbumbumbu au wanafanya makusudi. It is very unfortunate we have a doomed judiciary! haiwezi kutoa hukumu ya haki kuhusu haya mabo kama ikitokea kesi sasa hivi inayohusu haya mambo.
Barbarosa ni mwanamke, nadhani mawazo yake yanatawaliwa na ile kitu.
For reference soma kesi hii ambayo CA ilidefine public interest in land
Shukrani sana mkuu!!!

Natamani kila mmoja angeweza kuipitia na kuielewa hii kesi!!!
 
Barbarosa maswala usiyoyafahamu ni vyema usiyazungumzie, badala ya kuwalaghai na kuwapotosha watu.
Mkuu,ubarikiwe sana kwa ufafanuzi wako mzuri sana.
Ushauri: Tafadhali nakuomba siku nyingine uwe unatolea ufafanuzi mambo ya kitaalamu kama haya kwa lengo la kutufundisha sisi wenye uhitaji wa kufahamu mambo kadhaa wa kadhaa na si kuwajibu hao akina "vichwa tupu".
 
Mkuu,ubarikiwe sana kwa ufafanuzi wako mzuri sana.
Ushauri: Tafadhali nakuomba siku nyingine uwe unatolea ufafanuzi mambo ya kitaalamu kama haya kwa lengo la kutufundisha sisi wenye uhitaji wa kufahamu mambo kadhaa wa kadhaa na si kuwajibu hao akina "vichwa tupu".
Karibu mkuu.

Hivi punde nitaleta bandiko linalohusu utukufu na mamlaka ya Bunge juu ya Rais wa JMWT!
 
Sheria zimewekwa vizuri sema hazifuatwi. Rais au waziri anapaswa kufuata masharti ya sheria za nchi ila tatizo wanajitwalia twalia tu kinyume na Sheria. Ukitaka kuchukua ardhi ya kijiji lazma ngazi zote zishirikishwe kuanzia chini (Soma VLA)... Tatizo bongo hawafuati sheria. Labda tutunge sheria Ili kulinda sheria zetu, nani atunge? Ccm ya watawala na watawala wa ccm hakuna anayeweza kuleta sheria ya yeye kujisulubu.
Nilisononeka siku moja, mtu mwenye ekari 30, ananyanganywa kuwa hajaendeleza! Cha ajabu tafsiri ya neno "kuendeleza" haikutolewa. Isitoshe,huo uendelezaji haukuwa na statutory time limit kuwa utanyanganywa muda fulani.
Kingine kibaya, tuna maeneo ya Kitaifa,mfano mashamba ya kilimo ya serikali. Mtu mmoja anaamua,mfano shamba la Mbarali kuwa wanakijiji wanaozunguka eneo hilo wagawiwe hiyo ardhi. Je, mwananchi wa Karagwe hana haki nalo kams Mtz? Huo umma ni upi ambao ndo unawakilishwa na single person? Je, mikoa ambayo haikubahatika kuwa na mashamba ya aina hiyo,waNanchi wake watafaidikaje na migawo kama hiyo?
I believe, kama ulivyosema, tukiendekeza sheria hizi kwa kukaa kimya huku tunaona hali halisi ,ardhi yetu itanufaisha baadhi tu.
 
Back
Top Bottom