Nimrod Mkono alitaka tatizo kati ya Tanesco na IPTL lidumu milele ili afaidike. Kumbukeni alichokifanyia BOT kwenye kesi ya Valambhia.
Naomba kutoa ufafanuzi kidogoNimeupenda uchambuzi wako. Nakubaliana no isipokuwa nadhani kuna makosa machache umefanya, labda sikuelewa vizuri nieleweshe zaidi.
Kama Tanesco hawakupeleka VAT, TRA waibane Tanesco sio IPTL
Nadhani hapa umechanganya mambo. Unazungumzia umeme unaouzwa na Tanesco au umeme unaouzwa na IPTL? Swala lililopo ni umeme unaouzwa na IPTL, Tanesco akiwa mnunuzi.
Kama unazungumzia umeme unaouzwa na IPTL basi kwa msimamo huo, kama Tanesco watakuja kwako kununua nguzo za umeme, na wewe ukawacharge VAT kama utashindwa kuwasilisha hivyo VAT basi wadaiwe Tanesco. Nikija mimi kununua mbao kwako ukanicharge VAT lakini ukashindwa kuwasilisha basi ni mimi wa kudaiwa? Wataniona wapi? Kuna wangapi wanaokuja kununua vitu kwako kwa siku moja - itakuwa rahii kuwafuatilia?
Vile vile sikubaliani na wewe kwenye sentensi ifuatayo: Naamini Tanesco walikuwa wanatenga hii pesa baada ya kupokea Tax invoices toka IPTL. Kwa kuwa mnunuaji siyo anayepeleka VAT bali muuzaji(mfanyabiashara, yaani ni IPTL)
Nakubaliana na wewe hapa:
basi hakuna tatizo lolote kulipa IPTL pesa yote bila kupunguza kodi yeyote, laba ka TRA waliiagiza Tanesco kuwa wakara wa kuikusanyia kodi zote za IPTL, vinginevyo hakuna kosa.
Ndugu watanzania wote (in the voice of profesa Muhongo)
Tuache Jaziba, tuache kulazimisha mapenzi yetu kutimia,tuwe na subra, tujipe nafasi ya kutafakari na kupima mambo haya, tujiweke katika nafasi ya kuwatendea maadui zetu vile ambavyo sisi tungependa kutendewa.
Na zaidi, tufuate ushauri alioutoa Mheshimwa Lusinde jana jioni bungeni, kwamba, "TUSEME KWELI ILI TUFANYE MAAMUZI YA HAKI"
KUHUSU PESA ZA ESCROW KUWA NI ZA UMA ETI KWA SABABU KULIKUWA NA KODI YA VAT NDANI YAKE
Ndugu watanzania wote.
Huu ni upotoshaji, ni uongo na uzushi ambao tunapaswa kuukataa, jambo lolote linalofanywa kwa uovu mwisho wake huwa sio mwema.
Report iliyowasilishwa na PAC katika bunge letu, japo ilitegemewa kuwa msingi wa kulipatia haki Taifa letu, imekuwa ni chanzo cha aibu kwa Taifa zima, hutuwezi kupigania maslahi ya Taifa letu kwa kusema uongo, kuficha ukweli kwa wingi wa meneno yaliyopindishwa pindishwa na kupambwa kwa lugha za ghirba.
UKWELI NI HUU
Kama ambavyo mahusiano ya IPTL na TANESCO yanajurikana, hawa walikuwa na bado wanaendelea kufanya biashara pamoja, IPTL akiwa muuzaji na TANESCO Mnunuzi.
Bila kuzingatia namna wanavyofikia bei ya bidhaa husika, ni wazi IPTL imekuwa ikiipatia INVOICES Tanesco, Ili Tanesco Iilipe IPTL.
Sheria yetu ya kodi ya VAT ya mwaka 1997, imetoa maelekezo yanayowapa wafanyabishara FURSA ya kukusanya kodi ya VAT kutoka kwa wanunuzi wa bidhaa zao, kwa niaba ya TRA.
Kutokana na vigezo vilivyowekwa katika sheria husika, IPTL nao ni wakara wa TRA katika kukusanya kodi ya VAT kutoka Tanesco.
Kutokana na mahusiano ya kibishara kati ya TANESCO NA IPTL, TANESCO Haina mamlaka mpaka leo ya kuchukua maamuzi ya kutoilipa IPTL VAT eti ipeleke VAT hiyo TRA yenyewe.
Hivyo basi, hata katika PESA zilizokuwa kwenye ACCOUNT YA ESCROW, TANESCO walitekeleza wajibu wao wa kisheria na kibiasha kuziweka hela hizo kwenye account hiyo zote za IPTL pamoja na VAT (Ambazo kimsingi zote ni za IPTL), Na wakati malipo yanafanyika kutoka account hiyo, YALIFANYIKA KWA USAHIHI KABISA Kwa PESA zote KULIPWA kwa IPTL. Kwa sababu ni wajibu wa IPTL kukusanya VAT kutoka Tanesco.
TRA walipaswa kuidai IPTL pesa hiyo ndani ya mwezi mmoja baada ya IPTL kuipatia INVOICES Tanesco, bila kujali kama IPTL wanaubishani na Tanesco juu ya usahihi wa INVOICE AMOUNTS au la?.
Huu ndio utaratibu, sio mpya, na wote tunaufahamu, jana nimetoa mfano ambao haukueleweka, ukienda dukani kununua bidhaa, unaambiwa bei ya bidhaa ambayo ndani yake kuna VAT, ukifanya maamuzi ya kununua unamlipa muuzaji pesa zote, NA KUANZIA HAPO ZINAKUWA ZAKE na wewe bidhaa inakuwa yako rasmi.
Swala la wafanyabishara kutopeleka makusanyo ya VAT TRA ni tatizo lingine.
HIVYO BASI
Kama sababu ya msingi ya kudai kwamba zile pesa ni za UMA ni sababu ya VAT COMPONENT KWA ZILE HELA, HUO NI UONGO NI UPOTOSHAJI.
Nawasilisha.
Naomba kutoa ufafanuzi kidogo
Kama Tanesco hawakupeleka VAT, TRA waibane Tanesco sio IPTL
Kwa mfanyabiashara aliyesajiliwa VAT, anajukumu la kupeleka TRA tofauti kati ya VAT aliyokusanya na VAT aliyolipa au aliyotakiwa kulipa.
Tanesco wakikusanya VAT toka kwetu wanatakiwa wapeleke TRA. Kama katika kufanya biashara yao walilipa gharama zenye VAT ndani yake kama vile capacity charge, wanatakiwa kukokotoa tofauti kati ya waliyopokea na waliyolipa. Kama waliyopokea ni kubwa kuliko waliyolipa, wataipeleka TRA ya juu. Kama waliyopokea ni ndogo kuliko waliyolipa, watatakiwa kuvizia mwezi unaofuata kurecover hiyo deficit kati ya input na output tax. Kwa hiyo kama Tanesco walikuwa wanapata excess ha hawapeleki, wabanwe wao.
Vivyo hivyo na IPTL kama mfanyabiashara mwingine, walitakiwa kila walipopeleka invoice zenye VAT za kuwadai Tanesco, mwisho wa kila mwezi walitakiwa kukokotoa VAT waliyolipia kwenye manunuzi/gharama zao na VAT ya invoice zote walizotoa mwezi husika ikiwa na zile walizopeleka Tanesco. Kama VAT amount ya invoices walizotoa ni kubwa kuliko VAT ya invoices walizolipia gharama, difference walitakiwa wapeleke TRA bila kusubiri eti pesa za Escrow. Kama hawakupeleka, IPTL na TRA wote wawajibishwe. Kama hawakupeleka, na kama TRA walijua, TRA wachinjwe kama hawakuchukua hatua hata ya kukamata mitambo.
Vile vile sikubaliani na wewe kwenye sentensi ifuatayo: Naamini Tanesco walikuwa wanatenga hii pesa baada ya kupokea Tax invoices toka IPTL. Kwa kuwa mnunuaji siyo anayepeleka VAT bali muuzaji (mfanyabiashara, yaani ni IPTL)
Hapa kunielewa. Nilikuwa namaanisha kuwa, Tanesco walikuwa wanapeleka pesa Escrow account baada ya kupokea tax invoice toka IPTL, na hizo zilikuwa na VAT. Tanesco kama mnunuzi, si jukumu lake hapa kuhakikisha VAT ya kwenye invoice zilizoandaliwa na IPTL inalipwa au la. Kama lilivyo jukumu la Tanesco kuwasilisha TRA VAT anayotuchaji sisi kwenye umeme, pia ni jukumu la IPTL kuwasilisha TRA VAT ya kwenye invoices za Tanesco hata kama Tanesco hajalipa au ameweka fedha IPTL.
Itakuwa ni kosa kubwa kwa IPTL na TRA yenyewe kusubiri walipwe fedha za kwenye escrow eti ndio walipe VAT.
Kuna mchangiaji kaongelea suala WITHHOLDING TAX, ambayo ni 5% ya capacity charge before VAT. Hili sasa naliona kuwa tatizo kama halikuzingatiwa haswa na Tanesco wakati wa kupeleka pesa escrow account. Kila walipokuwa wakiandaa malipo ya IPTL invoices na kuhifadhi kwenye escrow account walitakiwa kukata hiyo withholding tax na kuipeleka TRA. Kama hawakufanya hivyo, Tanesco wako liable. Wakati wa kuziiba hizi pesa toka BOT, wezi hawa walitakiwa wacheki na Tanesco kama alikata withholding tax ili kama hakukata, wakate sasa. Kwa wezi hawa alivyo na papara nina wasiwasi kama walicheki na Tanesco.
Mh.ukisoma ulivyo andika, ni kama pacha na nilivo andika. Naona zimeunganishwa.
Tuwasaidie hawa watu wajikite kwenye namna zilivyotolewa BOT kabla ya kuisha kwa mzozo wa wa capacity charge ambao ndio chanzo cha kufungua account ya escrow. Tuking'ang'ana na kuwa ni za umma au sio za umma, kuna kodi au hakuna kodi hatufika tunakotarajia kufika maana hakuna kodi ya VAT ndani yake. Hat withholding tax, Tanesco walitakiwa wawe wamekata kabla ya kuzipeleka Escrow account
Mgogoro wa Capacity charge kati ya Tanesco na IPTL ulikuwa ni baina yao wawili, maelezo ya Profesa Muhongo jana yanasema Tanesco HAIJAWAHI WAKATI WOWOTE ULE MPAKA WAKATI ULE ANAONGEA BUNGENI, Kufungua kesi mahala popote pale wakilalamikia capacity charges.
Makubaliano ya kuweka hela kwenye Escrow yalikuwa kati ya Tanesco na IPTL, Bot akawa muhifadhi wa fedha, wakakubalina pesa zinatolewa kwa jinsi watakavyokuwa wanakubalina katika ubishani wao.
Tanesco wakakaa kunduchi beach, wakaona walipe tu hizo hela zote.
Mambo ya mahakamani ni uzushi, Mahakamani kulikuwa na kesi ya juu ya kiwango cha uwezekezaji, ni Kwa nini MKONO alikwenda kufungua kesi ya kiwango cha uwekezaji wa IPTL badala ya CAPACITY charge kama alivyoshauri anajua yeye na Tanesco.
Tanesco walikuwa wawakilishi wetu katika hili, na maamuzi yao yote ni kwa niaba yetu, kwamba wanafanyia maamuzi kunduchi au wapi hizo discretion tumewapatia pia.
wewe ngoja nikuache tuh,
maana mara unasema hakuna sehemu tanesco walipofungua kesi mahakamani na tena hapo hapo unasema kesi iliyofunguliwa baina ya tanesco na iptl ni ya kiwango cha uwekezaji sasa ngoja nikuache tu uende zako,
unakanusha kile unachokisema,
sasa nakuuliza,kama kweli unakiri na kukubali kwamba ipo kesi ya msingi mahakamani na bado haijamalizika hao waliokaa kunduchi kuidhinisha pesa itoke walitoa kwa amri ya nani??
then tanesco sio ndiyo ambao walikaa huko kunduchi,hujui unachokiongea,,,
waliokaa huko kunduchi ni hao jamaa zako kina muhongo unaowatetea.
Usilazimishe mambo, haijawahi kuwapo kesi ya capacity charge, au unadhani watu wakipelekana mahakani basi ni kila tofauti zao zinazungumziwa huko.
sasa kama akina muhongo wanahusika na utawala wa tanesco, hautaki wakae vikao, mnataka shirika liongozwe vipi sasa?
Okoanchi CAG alikuwa sahihi. ESCROW haiqualify kuwa asset kwenye financial statements za TANESCO.Kitu ambacho CAG alifanya 2012 ni sahihi. NOTE DISCLOSURE.kwa sababu kuweka escrow kwenye asset position siyo sahihi.Ndugu yangu Fugwe
CAG NAYE AMECHANGIA KUTOBOA TUNDU LA KUDOKOLEA.
Tanesco katika mahesabu yao walikuwa wanaonyesha pesa ya escrow kama ASSET upande mmoja na kama LIABILTY upande mwingine ili kukeep track.
CAG katika Audit ya 2012 aliigaiza Tanesco kutoripoti hivyo na ndipo TUNDU la kudokoa lilipotobolewa.
Okoanchi CAG alikuwa sahihi. ESCROW haiqualify kuwa asset kwenye financial statements za TANESCO.Kitu ambacho CAG alifanya 2012 ni sahihi. NOTE DISCLOSURE.kwa sababu kuweka escrow kwenye asset position siyo sahihi.
Samahani kwa kuchelewa kujibu.Ni kweli huyo UMMA yaani TRA anadai hela nyingi sana. Naomba ujue haidai ESCROW Anamdai IPTL. Pesa ilipokuwa BOT iliwekwa ili kusubiri deni lijulikane na ndipo lilipwe na kama IPTL alikuwa anazisubiri ili akalipie malimbikizo ya kodi, basi angefanya hivyo mara baada ya kulipwa.TRA kama walitambua kuwa wanadai walikuwa na nafasi ya kuiambia BOT kuwa wazuie hizo pesa.TRA nao wana kesi ya kuujibu umma, kwa nini hawakukusanya pesa ya kodi in time?Ndugu Okoachi uchambuzi wako mzuri sana, Hiyo kodi ya TRA ni ya nani? Uliandika vizuri kuwa IPTL ni wakala wa TRA kukusanya VAT kutokana na malipo ya capacity charge, miaka yote hiyo kama hawa kufanya hesabu na VAT ina penalt, huoni huyo TRA(umma) anadai pesa nyingi? Ufafanuzi please!