Usafiri wa usiku

Usafiri wa usiku

Bin Chuma75

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2012
Posts
1,002
Reaction score
1,092
Napenda kushare nanyi jambo moja ambalo ninauzoefu nalo sana, ndugu zangu wenye magari madogo hasa private kwa sasa epukeni safari za usiku kutokana na mabasi kuruhusiwa kutembea masaa 24.

Kutakusaidia kuepukana na ajali zisizo za lazima. Iwapo ukikutana na basi akikuletea upande wako kidogo tu ni rahisi kujiingiza uso kwa uso au kwenda nje mazima, sababu ni vigumu kuchagua pa kupita kwa ghafla maana macho yako yanaishia mwisho wa taa zako tu.

Ninauzoefu wa barabarani kwa magari yote (mabasi, malori, gari dogo) zote hizi nimeendesha kwa miaka mingi ndani na nje ya nchi. Hivyo nimeona nitoe ushauri kidogo kwa wenzangu tunaopenda safari za usiku.
 
Usiku wa juzi tulipita sekenke na Takbiir( Wasafi) ya kutokea Dar-Katoro saa tano kasorobo usiku aisee kuna jiwe lilipiga koo karibu na nilipokaa nikaona vumbi kioo kwisha habari yake.Dereva alipangua gia balaa walikagua kioo Igunga.
Nahisi ule uhuni wa zamani unarudi.
 
Usiku wa juzi tulipita sekenke na Takbiir( Wasafi) ya kutokea Dar-Katoro saa tano kasorobo usiku aisee kuna jiwe lilipiga koo karibu na nilipokaa nikaona vumbi kioo kwisha habari yake.Dereva alipangua gia balaa walikagua kioo Igunga.
Nahisi ule uhuni wa zamani unarudi.
Pole mkuu. Bila ya kufunga kioo siku hiyo, keo usingeandika uzi huu.
 
Pole mkuu
Nmecheka kama mazuri
Usiku wa juzi tulipita sekenke na Takbiir( Wasafi) ya kutokea Dar-Katoro saa tano kasorobo usiku aisee kuna jiwe lilipiga koo karibu na nilipokaa nikaona vumbi kioo kwisha habari yake.Dereva alipangua gia balaa walikagua kioo Igunga.
Nahisi ule uhuni wa zamani unarudi.
 
Watanzania bana daaa.
Tahadhari ni muhimu ila sidhani kama usalama unaosemwa hapa unaakisi kile kilichopo kipindi hiki.

Hakuna basi linalokimbia zaidi ya 80 iwe usiku au mchana sasa ajali ya speed ipi inayotamkwa hapa..?
 
Watanzania bana daaa.
Tahadhari ni muhimu ila sidhani kama usalama unaosemwa hapa unaakisi kile kilichopo kipindi hiki.

Hakuna basi linalokimbia zaidi ya 80 iwe usiku au mchana sasa ajali ya speed ipi inayotamkwa hapa..?
Jamaa umewahi yaona yanvyokwenda ovyoo? Yema asubuhi tuuuu hata misugusugu hayajafika. Nilibahatika kukutana nayo yanavyotanua ovyo, ni balaaa.
 
Hivi hiyo speed 80 unayosema kwa basi unaijua au? Usiwe umekaa kwenye siti unaendeshwa unaona ni speed ndogo, dereva ndiyo anajua timing zote za kukufikisha unapofika, na kwa kukuongezea hiyo speed 80 unayoiona mchana usiku inakuwa mara 2 yake kutokana na nature, (madereva watanielewa zaidi) . Sababu usiku macho yanaona mwisho wa taa zako tu sio zaidi ya hapo.
Watanzania bana daaa.
Tahadhari ni muhimu ila sidhani kama usalama unaosemwa hapa unaakisi kile kilichopo kipindi hiki.

Hakuna basi linalokimbia zaidi ya 80 iwe usiku au mchana sasa ajali ya speed ipi inayotamkwa hapa..?
 
80km/h ya basi ni sawa na 120 km/h ya gari ndogo.
Hivi hiyo speed 80 unayosema kwa basi unaijua au? Usiwe umekaa kwenye siti unaendeshwa unaona ni speed ndogo, dereva ndiyo anajua timing zote za kukufikisha unapofika, na kwa kukuongezea hiyo speed 80 unayoiona mchana usiku inakuwa mara 2 yake kutokana na nature, (madereva watanielewa zaidi) . Sababu usiku macho yanaona mwisho wa taa zako tu sio zaidi ya hapo.
 
Napenda kushare nanyi jambo moja ambalo ninauzoefu nalo sana, ndugu zangu wenye magari madogo hasa private kwa sasa epukeni safari za usiku kutokana na mabasi kuruhusiwa kutembea masaa 24.

Kutakusaidia kuepukana na ajali zisizo za lazima. Iwapo ukikutana na basi akikuletea upande wako kidogo tu ni rahisi kujiingiza uso kwa uso au kwenda nje mazima, sababu ni vigumu kuchagua pa kupita kwa ghafla maana macho yako yanaishia mwisho wa taa zako tu.

Ninauzoefu wa barabarani kwa magari yote (mabasi, malori, gari dogo) zote hizi nimeendesha kwa miaka mingi ndani na nje ya nchi. Hivyo nimeona nitoe ushauri kidogo kwa wenzangu tunaopenda safari za usiku.
Hili suala lingejadiliwa kikamilifu tungekuwa na Bunge.
 
Sitaweza kushindana na comment yako, inaonekana hujui lolote kuhusu mfumo mpya wa mwendo wa mabasi.

POLE SANA.
Hivi hiyo speed 80 unayosema kwa basi unaijua au? Usiwe umekaa kwenye siti unaendeshwa unaona ni speed ndogo, dereva ndiyo anajua timing zote za kukufikisha unapofika, na kwa kukuongezea hiyo speed 80 unayoiona mchana usiku inakuwa mara 2 yake kutokana na nature, (madereva watanielewa zaidi) . Sababu usiku macho yanaona mwisho wa taa zako tu sio zaidi ya hapo.
 
Miaka ya nyuma kidogo nilianza safari saa sita usiku na Cresta Gx 100 nikitoka Dar kuelekea Arusha...nilipokaribia Wami nikakuta Fuso zinasubiriana kwa ajili ya usalama, nikawona waoga tu hivyo nikaendelea na safari.
Kufika Wami katikati ile kucheck njia yote imefungwa na yale matenga ya nyanya ya mabanzi! Wakati nafikiria cha kufanya ghafla nikaona watu kama ishirini wanakuja na mapanga huku wamebeba tochi na silala mbali mbali wakisema "simama wewee" dah! Ilikuwa noma sana.
 
Back
Top Bottom