Usafiri wa usiku

Usafiri wa usiku

80km/h ya basi ni sawa na 120 km/h ya gari ndogo.
Ha ha ha tycoon nineamini kupata pesa na mali ni tofauti na kupata elimu. Ungeingia darasa la fizikia usinge andika hiki ukichoandika. Ushauri usiwasikilize makenika walio kimbia shule kwenda kutumwa spana. Kumbuka huwezi kutoa usichokua nachacho
 
Usiku wa juzi tulipita sekenke na Takbiir( Wasafi) ya kutokea Dar-Katoro saa tano kasorobo usiku aisee kuna jiwe lilipiga koo karibu na nilipokaa nikaona vumbi kioo kwisha habari yake.Dereva alipangua gia balaa walikagua kioo Igunga.
Nahisi ule uhuni wa zamani unarudi.
Mlikuwa mnamsifia lugola pambanen sasa
 
Zikishaanza kusafiri gari nyingi usiku inamaana njia itakua bize muda wote kwaio hata watekaji hawataweza
 
Hivi hiyo speed 80 unayosema kwa basi unaijua au? Usiwe umekaa kwenye siti unaendeshwa unaona ni speed ndogo, dereva ndiyo anajua timing zote za kukufikisha unapofika, na kwa kukuongezea hiyo speed 80 unayoiona mchana usiku inakuwa mara 2 yake kutokana na nature, (madereva watanielewa zaidi) . Sababu usiku macho yanaona mwisho wa taa zako tu sio zaidi ya hapo.

Mkuu kama niko sahihi siku hizi kuna kitu kinaitwa king’amuzi, so iwe mchana au usiku ukizidisha speed ya 80 KM/hr unakutana na fine /kifungo ila kwa Basi za abiria.
 
Nimesafiri sana usiku, ila kwa sasa nimekuwa mwoga sana, na sijui kwanini naogopa sana kusafiri usiku
 
80km/h ya basi ni sawa na 120 km/h ya gari ndogo.

Mkuu acha kuwa na akili kama za ccm, unaeleww maana ka KM/hr? Nakupa shule ndogo tu ni kwamba km/hr ni kwa gari zote(japo hii siyo tafrisi nzuri) sema utofauti uko kwa stability ya gari. Basi ikifika 120 KM/hr hahahahah lazima upate kitete lakini kwa gari ndogo ni kawaida
 
Miaka ya nyuma kidogo nilianza safari saa sita usiku na Cresta Gx 100 nikitoka Dar kuelekea Arusha...nilipokaribia Wami nikakuta Fuso zinasubiriana kwa ajili ya usalama, nikawona waoga tu hivyo nikaendelea na safari.
Kufika Wami katikati ile kucheck njia yote imefungwa na yale matenga ya nyanya ya mabanzi! Wakati nafikiria cha kufanya ghafla nikaona watu kama ishirini wanakuja na mapanga huku wamebeba tochi na silala mbali mbali wakisema "simama wewee" dah! Ilikuwa noma sana.
Malizia kisa Mzee Baba...inaelekea moyo ulidundia kwenye kioo cha gari cha mbele.
 
Back
Top Bottom