Usafiri wa mwendokasi bado ni shida

Usafiri wa mwendokasi bado ni shida

Magita

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2013
Posts
319
Reaction score
144
Wana JF sijawahi kupanda mabus ya mwendokasi kwa kipindi cha asubhi kutoka Mbezi to Kariakoo, sababu siishi maeneo ya njia ile. Ila jana niliutumia usafiri ule nikitokea Mbezi to Kariakoo kwa asbhi ..... jamani nimegundua ule usafiri ni hatari sana, kwanza nimeona magari ni machache watu ni wengi mno, pili nikagundua TB unaweza kuipata kwasababu mjazano ule sijawahi kuuona popote pale, nilishindwa kuvumilia hadi nikashuka Ubungo nikapanda magari nusu susu hadi nikafika kariakoo.
Swali: Kwanini hio kampuni isiyayaongeze hayo mabus yakawa mengi? Maana kwa ujaagi ule hata ikitokea dharula yeyote nimeona risk yake itakuwa 75%, duuu hatari sana,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna usafiri nauchukia km Mwendokasi! Mara 100 upande daladala za kawaida kuliko mwendokasi. Magari ya Kivukoni ndo mtihani zaidi, unaweza kusubiri kituoni nusu saa nzima ndo gari lipite na likipita limejaa hakuna hata pa kuingiza mguu, unaendelea kusubiri lengine kwa mda usojulikana km una haraka unachelewa uendako kwa usafiri huu! Na km unashuka njiani ndo unakoma zaidi kufanikiwa kupita nyomi la watu pale mlangoni... Dah hatari. Naskia kuna mtu ashawahi kuzimia ndani ya mwendokasi wakamshusha Jangwani.
 
mi naishi ubungo ila mwendokasi nakwepa sana kuzipanda.. bora nipande gari za sinza zinazopita mabibo.. nikiwa naenda town au kurudi
 
Mwendokasi ni moja ya miradi iliyopangwa bila kuangalia ongezeko la mahitaji ya watumiaji barabara. Siyo mwendokasi pekee, baki miradi mingi ya ujenzi ipo kwa mahitaji ya sasa tu, siyo ya miaka 50 ijayo.
Ndani ya miaka 20 ijayo, barabara nyingi sada za majiji yetu itabidi zifumuliwe zijengwe upya.
 
Mwendokasi ni moja ya miradi iliyopangwa bila kuangalia ongezeko la mahitaji ya watumiaji barabara. Siyo mwendokasi pekee, baki miradi mingi ya ujenzi ipo kwa mahitaji ya sasa tu, siyo ya miaka 50 ijayo.
Ndani ya miaka 20 ijayo, barabara nyingi sada za majiji yetu itabidi zifumuliwe zijengwe upya.
Hadi jana niliwaonea huruma watu kwa maana ya kwamba kama unaishi kimara ama mbezi na kazi unafanya posta ama kakriakoo nikaona ndani ya miaka 3 ama 5 lazima TB itakuwa yako. Kwanini usafiri wa zamani yani daladala nazo zisiwepo? Kweli kama nchi kuna huruma hapo kwa wananchi wake? Kwa ujaaji ule mara paaaap mmeingia ktk mtaro wangapi wataumia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna usafiri nauchukia km Mwendokasi! Mara 100 upande daladala za kawaida kuliko mwendokasi. Magari ya Kivukoni ndo mtihani zaidi, unaweza kusubiri kituoni nusu saa nzima ndo gari lipite na likipita limejaa hakuna hata pa kuingiza mguu, unaendelea kusubiri lengine kwa mda usojulikana km una haraka unachelewa uendako kwa usafiri huu! Na km unashuka njiani ndo unakoma zaidi kufanikiwa kupita nyomi la watu pale mlangoni... Dah hatari. Naskia kuna mtu ashawahi kuzimia ndani ya mwendokasi wakamshusha Jangwani.
Hivi haujanunua usafiri wako hadi leo
 
ikitokea ebola dar hakuna mtu atapona maana si kwa mgusano ule
 
Wana JF sijawahi kupanda mabus ya mwendokasi kwa kipindi cha asubhi kutoka Mbezi to Kariakoo, sababu siishi maeneo ya njia ile. Ila jana niliutumia usafiri ule nikitokea Mbezi to Kariakoo kwa asbhi ..... jamani nimegundua ule usafiri ni hatari sana, kwanza nimeona magari ni machache watu ni wengi mno, pili nikagundua TB unaweza kuipata kwasababu mjazano ule sijawahi kuuona popote pale, nilishindwa kuvumilia hadi nikashuka Ubungo nikapanda magari nusu susu hadi nikafika kariakoo.
Swali: Kwanini hio kampuni isiyayaongeze hayo mabus yakawa mengi? Maana kwa ujaagi ule hata ikitokea dharula yeyote nimeona risk yake itakuwa 75%, duuu hatari sana,

Sent using Jamii Forums mobile app


Walivyowavivu kufikiri watakuja na ongezeko la nauli ili wasio na uwezo wasipande ionekane tatizo limetatuliwa
 
ebola mbali, kifua kikuu tu kila siku watu wanaambukizana pamoja na magonjwa ya ngozi hasa tetekuwanga.
Viongozi hawalioni hilo wanaloliona kuwa ni gongwa kubwa eti ni HIV tu, lkn TB watu hawawezi kuambukizana, mwanzoni niliwaona hadi white color~wazungu, wa Asia wakipanda ila sasaiv SIJUI KAMA WANAPANDA TENA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwendokasi ni moja ya miradi iliyopangwa bila kuangalia ongezeko la mahitaji ya watumiaji barabara. Siyo mwendokasi pekee, baki miradi mingi ya ujenzi ipo kwa mahitaji ya sasa tu, siyo ya miaka 50 ijayo.
Ndani ya miaka 20 ijayo, barabara nyingi sada za majiji yetu itabidi zifumuliwe zijengwe upya.
mm hata sielewi waliobuni mradi huu walikuwa wanafocus miaka mingapi mbele ! Anyway kwa kusema kweli kabisa hawa watalaam kwa wakati huo wlipokuwa wakibuni mradi huo sijui mwaka gani walikuwa nyuma miaka 30 ndio kinachotugharimu sasa hivi. ukiangalia hata flyover ya mfugale pale tzr itaaleta shida itaja onekana haisaidii kitu miaka kumi ijayo.
 
Ule usafiri una laana . umejaa kero sana watu mnajazana kibao ukifika unakokwenda unanuka jasho mwili mzima si-ajabu unaweza ukazoa magonjwa humo humo .... unaweza kukata ticket sasa hivi gari ukaja kupanda baada ya nusu saa mbaya zaidi kuna wakati magari mengine yana wapita yakiwa empty kabisa na yanapita bila kusimama kituoni ili yaweze kuwachukua watu ambao mme-sha si-mama kiasi ambacho mpaka mnahisi kwamba miguu inataka kuingia tumboni
Hamna usafiri nauchukia km Mwendokasi! Mara 100 upande daladala za kawaida kuliko mwendokasi. Magari ya Kivukoni ndo mtihani zaidi, unaweza kusubiri kituoni nusu saa nzima ndo gari lipite na likipita limejaa hakuna hata pa kuingiza mguu, unaendelea kusubiri lengine kwa mda usojulikana km una haraka unachelewa uendako kwa usafiri huu! Na km unashuka njiani ndo unakoma zaidi kufanikiwa kupita nyomi la watu pale mlangoni... Dah hatari. Naskia kuna mtu ashawahi kuzimia ndani ya mwendokasi wakamshusha Jangwani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom