Usafiri bora Dar - Dubai

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,648
Reaction score
10,843
Heshima zenu wasafiri wazoefu!

Ukiacha Shirika letu la ATCL, ni mashirika gani bora ya Ndege, hasa zinazomilikiwa na nchi za Kiafrika, kwa safari ya Dar - Dubai?

Daraja ni la UCHUMI!

Nimeshasikia mashirika yafuatayo yakisifiwa!
1. Kenya Airways(KQ)
2. Ethiopian Air Lines (EAL)
3. RwandAir
4. South African Airways (SAA), ingawa sijui kama yanatoa huduma ya Dar - Dubai

Unalipendekeza shirika lipi kwa mtu anayeenda Dubai kwa mara ya kwanza?

Mtazamo wangu! Kwa kuwa inasemekana ndege za mashirika husika hupitia kwenye nchi zao kabla ya kufika yanakoenda, ninapendekeza kama ifuatavyo:
1. Wakati wa kwenda apande Ethiopian Air Lines ili apate fursa ya kupaona Addis Ababa

2. Wakati wa kurudi apae na SAA ili apitie South Africa japo sijui kama huo mzunguko utawezekana.

Nini ushauri wako?

ANGALIZO: Sina uzoefu na niliyoyaandika! Nisahihishwe kwa manufaa ya wengi!

Asanteni!!!
 
Ticketi za ndege kwenda nchi za watu mara nyingi unakata kwenda na kurudi, na kwa hiyo orodha ya mashirika ya ndege uliyoweka hapo juu kwa kupandia Dar tafuta Ethiopia au Kenya Airline.
 
Ticketi za ndege kwenda nchi za watu mara nyingi unakata kwenda na kurudi, na kwa hiyo orodha ya mashirika ya ndege uliyoweka hapo juu kwa kupandia Dar tafuta Ethiopia au Kenya Airline.
Kuna ulazima wa kukata shirika moja?

What if nitaamua kukata ya kwenda shirika moja na ya kurudi shirika jingine tokea kabla sijaondoka nchini Tanzania, kutakuwepo na vizuizi vyovyote? Kwamba unaondoka nchini ukiwa umeshakata tiketi ya kurudi lakini ya shirika jingine. Kuna shida mtu akiamua kufanya hivyo?
 
Sina uhakika sana lakini nafikiri inawezekana wengi tunapenda kukata shirika moja sababu ya kupunguza gharama za nauli.
 
Mara nyingi ukikata Return ticket unapunguza gharama ya nauli. By the way kwa nini usisafiri na Emirates?
 
Mara nyingi ukikata Return ticket unapunguza gharama ya nauli. By the way kwa nini usisafiri na Emirates?
"Ushamba" tu mkuu! Kwa ambao hatujabahatika kufika kwenye nchi nyingi, unapopata fursa ya kusafiri unatafuta kumaximize uwezekano wa alau kupitia nchi zaidi ya moja.

Nafikiri FLY EMIRATES ni ya Moja kwa moja kutokea Nairobi au Dar(sijui kama ipo Dar) hadi Dubai. Lakini kwa mashirika kama Ethiopian Air Lines ni lazima yapitie kwanza "nyumbani" Addis Ababa kabla ya kuendelea na safari hadi Dubai.

Kwa hiyo pamoja na kwamba RETURN TICKET ni nafuu, lakini nimechagua kutokuichukua hiyo ofa ili kupata nafasi ya "kuosha" macho.

Ndiyo maana ninapendelea mashirika mawili kati ya haya matatu:
1. ETHIOPIAN AIR LINES
2. SOUTH AFRICAN AIR WAYS
3. RWANDAIR
 
Tumeshajua unaenda Dubai
 
Kutoka Dar huwa kuna Emirates na Fly Dubai. Kama hutaki direct from Dar to Dubai basi itabidi uchukue kati ya hizo 2. Ethiopian Airlines au Kenya Airways. Hata hivyo ukiwa on transit utazurula tu airport ya nchi husika kuosha macho.
 
Kutoka Dar huwa kuna Emirates na Fly Dubai. Kama hutaki direct from Dar to Dubai basi itabidi uchukue kati ya hizo 2. Ethiopian Airlines au Kenya Airways. Hata hivyo ukiwa on transit utazurula tu airport ya nchi husika kuosha macho.
Hata hiyo nayo inaweza kuongeza "kaelimu" juu ya nchi za wengine!
 
Hata hiyo nayo inaweza kuongeza "kaelimu" juu ya nchi za wengine!
Of course utaona jinsi airport za wengine zikoje. Sijapita Terminal 3 muda mrefu sana, nilipita wakati imefunguliwa hata kukamilika ilikuwa bado sijui itakuwaje sasa hivi lakini kabla ya hapo ukiangalia Terminal 2 yetu kabla ya hiyo 3 haijajengwa halafu ulinganishe na za wenzetu ilikuwa ni kama airport ya mji mdogo tu kwenye nchi hizo.
 
Atcl wanaenda huko, ukiona Mkenya amepanda Shirika lingine jua chaguo lake la kwanza Kenya airways, amekosa nafasi huko au KQ hawaendi huko...kuwa Mzalendo safiri na ATCL.
 
Sisi tulisafiri kwa Dar Express inapita Great North Road mpaka Kairo kisha unachukua shata bei poa.
 
Atcl wanaenda huko, ukiona Mkenya amepanda Shirika lingine jua chaguo lake la kwanza Kenya airways, amekosa nafasi huko au KQ hawaendi huko...kuwa Mzalendo safiri na ATCL.
Kiongozi, wanaoenda kusoma vyuo vya nje hawajakosa vyuo nchini. Suala hapo si usafiri tu, bali pia na exposure.

Kama hitaji pekee ni kusafiri tu, basi vya "nyumbani" ni bora zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…