Common man
Member
- Mar 10, 2011
- 15
- 0
Ni nani anapaswa kulaumiwa kuhusu uchafu ulivyozagaa katika Jiji? Hivi karibuni nilisafiri na kuingia katika Jiji hili ambalo wengi wanasema ndilo sura halisi ya Tanzania. Kwanza nikiri kuwa nililazimika kununua karanga kwa machinga/mchuuzi. Aliniwekea kweye kifungashio chake. Mara baada ya kula karanga nilikuwa natarajia niikute mahali pakutupa taka ili nitupe kile kifungashio cha ajabu sikupata mahali rasmi pa kutupa.
Kama kweli kuna haja ya kuweka mazingira ya jiji safi basi mbona hakuna sehemu maalum za kutupa taka? Hivi viongozi wa ngazi zote hawawezi kufikiri na kulitatua tatizo hili? Jiji linanuka, linachafua sifa ya nchi.
Kama kweli kuna haja ya kuweka mazingira ya jiji safi basi mbona hakuna sehemu maalum za kutupa taka? Hivi viongozi wa ngazi zote hawawezi kufikiri na kulitatua tatizo hili? Jiji linanuka, linachafua sifa ya nchi.