Usafi tulioufanya leo utamaliza kipindu pindu??

Usafi tulioufanya leo utamaliza kipindu pindu??

niah

R I P
Joined
Sep 26, 2015
Posts
7,018
Reaction score
9,305
Kwanza natanguliza shukrani zangu za dhati kwa Mukulu wetu kutupa hii siku ili tufanye usafi kwenye sehemu zetu za makazi na malazi. Natoa pongezi pia kwa wale wote waliojitoa kwa ihari yao au kutumiwa vimemo jana kuwa waamke kujituma.(Africana area vilikuja vimemo).

Pamoja na shukrani zote naomba madaktari wetu wanisaidie kunipa jibu, je pindua pindua inatoka kwenye taka taka za kwenye mitaro na barabarani na nyasi zisizofyekwa au inatoka vyooni? Kwa ufahamu wangu mdogo najua kuwa pindua hasa inasambazwa na inzi, mikono michafu na maji yenye kinyesi chenye vimelea vya pinduka pinduka.

Mitaro tuliyosafisha leo bila gloves, taka tulizochoma na zina plastics ambazo ni sumu kwenye miili yetu, wengine mitaro ilikuwa na maji ambayo yanatapishwa toka vyooni je si tunaweza tusipate pinduka lakini tukaathirika kwenye mapafu na kupata minyoo??

Mpango huu uliandaliwa mapema almost two weeks ago, kwanini vyombo vya habari hasa radio na tv zisihamasishe wananchi kuandaa zana za kujikinga na vile vile kuwaeleza kuwa wasichome plastics bali wazijaze kwenye viroba ili machinga wanaoziuza wazipitie bila malipo?? Marambo nayo yangekusanywa ili yapelekwe kuchomewa kwenye sehemu ambayo yasingeaffect afya za watu wanaozunguka mahala yalipochomewa? Elimu, elimu elimu ndiyo tulikosa leo ili tuweze kulimaliza hili la leo salama.

Don't take me wrong, nia ya brother mapadlock ilikuwa na ni na itabaki kuwa bye lakini maandalizi na utekelezaji hautamaliza kipindu pindu. Je mabomba yanayopita kwenye maji machafu yamehamishwa leo? Je vyoo visivyofunikwa vimekaguliwa kuwekewa mifuniko? Je baada ya kazi watu walinawa na maji ya moto na sabuni kuepuka kujimbukiza na kuambukizana pindua? Huu ni ugonjwa unaotokana na kinyesi siyo nyasi wala chupa!

Nawasilisha.
 
Lengo KUU ni kusherehekea UHURU DAY kwa aina tofauti na si kumaliza kipindupindu..myMTIZAMO.
 
Attitude attitude attitude.

Huwezi kuwa na hulka ya kunawa mikono au kunywa maji yaliochemshwa kama hapo nje kwako tu umeshindwa kuokota takataka au mtaro umeziba.

Hilo ni somo kutoka kwa Magufuli
 
Magufuli anajaribu kujenga desturi mpya ya kujali usafi kuanzia ndani nyumbani mpaka nje ya nyumbani na kwingineko, ni vyema tuanze kujali usafi polepole tutafika na hata kipindupindu yenyewe itakuwa historia mbele ya safari!
 
Nilitegemea vyombo vya habari vielimishe wananchi kipi cha kuandaa siyo mifagio tu bali vyoo viangaliwe viwekewe hata majivu na iwe kila siku, waandae gloves kwa ajili ya usafi na kuanza kuchemsha maji nje ya vyoo ili kila ukitoka unawe na maji ya moto na sabuni. We unaoanaje? Yale mabomba tuliyoonyeshwa na ITV yanapita kwenye mfereji wa maji taka na vinyesi vikiwemo yangeonyeshwa kuwa yametolewa na kuhamishiwa mahali safi.
 
Nilitegemea vyombo vya habari vielimishe wananchi kipi cha kuandaa siyo mifagio tu bali vyoo viangaliwe viwekewe hata majivu na iwe kila siku, waandae gloves kwa ajili ya usafi na kuanza kuchemsha maji nje ya vyoo ili kila ukitoka unawe na maji ya moto na sabuni. We unaoanaje? Yale mabomba tuliyoonyeshwa na ITV yanapita kwenye mfereji wa maji taka na vinyesi vikiwemo yangeonyeshwa kuwa yametolewa na kuhamishiwa mahali safi.

HAH HAH HAH umenikumbuka mbali tumeweka sana MAJIVU ktk chakula kilichokalibia kuaharibika kinakata harufu na MLO KAMA KAWAIDA.
 
We ulitaja iweje mkuu kwa mtazamo wako
Nilitegemea vyombo vya habari vielimishe wananchi kipi cha kuandaa siyo mifagio tu bali vyoo viangaliwe viwekewe hata majivu na iwe kila siku, waandae gloves kwa ajili ya usafi na kuanza kuchemsha maji nje ya vyoo ili kila ukitoka unawe na maji ya moto na sabuni. We unaoanaje? Yale mabomba tuliyoonyeshwa na ITV yanapita kwenye mfereji wa maji taka na vinyesi vikiwemo yangeonyeshwa kuwa yametolewa na kuhamishiwa mahali safi.
 
Hahahahaaaa idadi ya wagonjwa imeongezeka maana tulikua tunasubiri leo ndio tukishambulie! Sijui akili kweli hizi
 
Uchafu mpaka sasa haujazolewaaaa!

Ovaaaa
 
ina maaana wanasubiri tv ifike kuona kama wamekusanya?
 
Back
Top Bottom