Watatumia drones,na Uganda watalipa kwa mikataba ya wese.Habari wana JF???
Leo asubuhi vyombo vingi vya habari vimezungumzia habari ya Marekani kupeleka majeshi nchini Uganda kwa minajili ya kumtokomeza kabisa Joseph Kony na kundi lake la Lord Resistance Army!
Marekani yenyewe imesema itatumia vifaa vya hali ya juu vya kujua wapi Kony alipo ili ama auawe au akamatwe!
Je tuseme ndiyo mwisho wake umefikia??? Mchezo mwingine unaanza huo tena East Africa baada ya wa Libya kuonekana unaelekea ukingoni!!!
Nawasilisha
Marekani hawawezi kuachana na mafuta.Ni sawa na mgonjwa mwenye kuhitaji drip halafu unamchomolea.Uchumi wa marekani uliinuliwa na automotive manufacturing/industry.Ndiyo maana sehemu nyingi hawataki kuziendeleza public transportation.Yani wana discourage hayo.Na ikafikia mahali kuwa na gari ni very easy/cheaper,or atleast more people are encouraged to have cars.Shida ni hapo bei ya wese ilipopanda na biashara ya kununua magari ikashuka hence automotive production failure.wamarekani na mafuta ni sawa uji na mgonjwa au mgambo na kirungu au dala dala na konda.............
Huyu kony siyo wa jana wala juzi, siku zote yupo.....si chini ya miaka 25....lakini leo eti obama anakuja kumsaka......m7 na waganda kwa ujumla jamaa ananyemelea wese......mtoeni baru ......
MAZZOUT, ESSENCE
miaka yote kumi aliokuwa wapi ndio leo aje kutoa msaada?
Mafuta ya Uganda yananukia, Ingawa kweli Konyi amefanya uhalifu mwingi, lakini walikuwa wapi siu zote hizo? !
Una akili sana wewe. Hawa LRA walikuwepo kwa miaka mingi sasa lakini Wababe wa dunia hawakuona umuhimu wa kumwaga wanajeshi wao mpaka baada ya mafuta kupatikana kule Uganda si ajabu hii pia ndio itatumia katika kuweka kituo chao kikubwa cha jeshi Afrika pale Uganda. Hawa jamaa wakiingia mahali ambapo wanaona watafaidika basi huwa hawaondoki kabisa.
Wamarekani hawana haja ya kuipeleleza uganda. Museveni anawapa siri zote bila wasiwasi, kama ilivyo kwa nchi nyingi za kiafrica hivi sasa!
Kweli, bana. US wako tayari hata kusaidia ujenzi wa miundo mbinu ya "Northern corridor"
Baada ya ujio wa "washauri" tutasikia Al shabaab wamejiingiza Tanzania na washauri hawa watakuja kutushauri jinsi ya kuwashughulikia "magaidi".
Tembelea hii
BBC News - US to send troops to Uganda to help fight LRA rebels
Increased Regional Trade and Integration | USAID East Africa Regional Mission
The Permanent Secretariat of the Transit Transport Coordination Authority of the Northern Corridor
Where's China?
Kama we ni askari kanzu kweli unajua maana ya askari kanzu.unachofikiria sicho.Mr. Kony now it's your turn to face the wrath of the AntiChrist. Licha ya kuwa "msemaji wa Mungu" sasa Kony upo hatarini kulipuliwa na kereng'ende (drones) za wamarekani. Jasho litakutoka. Umeyataka mwenyewe. Sikuonei huruma!
Nakubaliana na wewe .kwani Kony hajulikani alipo??
mwaka jana tu hapa alikuwa anaugua na kuwa na shida ya chakula na walikuwa wanafanya negociations na Museveni, Museveni akawa anampa chakula.
Hapo ni PETROL tu hakuna kingine.
Mbona wasipeleke wanajeshi Somalia au border ya kKenya na Somalia??
Au wanawaogopa Alshabab??...........wazee wa Sambusa!!!
Wewe ni nani unaefikiria kilicho?Kama we ni askari kanzu kweli unajua maana ya askari kanzu.unachofikiria sicho.
Mkuu jaribu kuangali USA ni polisi wa ulimwengu,UN ni yao.Kazi kwako kuna vitu vingi vya kutafuta kwenye google na Jf ndo tunapo elimishana.
Acha kudanganya watu. Usifikirie sote humu ni zao la shule za kata. Uchambuzi wako hauna mashiko!Nakubaliana na wewe .
Jiulize kwa nini wako Pakistan ili wawe jirani na afganstan.
Kwa nini afganstani ni kuwa jirani na warusi.
Walifanikiwa kuvunja umoja wa urusii kwa nia ya kuweza kutumia nchi mpya zitakazo undwa baada ya ku vunja
Umoja wa nchi za kirasha kama wanavyo tumia Poland sasa hivi kuweka mitambo yao ya kujikinga kama wakishambuliwa na warusi.
Na sasa wamethubutu na wamefanikiwa north Afrika na sasa wanaenda Uganda na wakifika hapo E Afrika iko chini yao na hapo waennda kusini nia yao kubwa ni mugabe na baada ya hapo swazi na afrika ya kusini na wote tutakuwa vibaraka wa USA.
Time will tell mkuu na siyo muda mrefu baada ya USA kuingia UgandaWewe ni nani unaefikiria kilicho?
Nashindwa kuelewa una maana gani kwa sababu unachokisema hakihitaji kueleweshana (sio kitu kipya)!Time will tell mkuu na siyo muda mrefu baada ya USA kuingia Uganda