US bombers fly close to North Korea

US bombers fly close to North Korea

Sexer

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2014
Posts
8,504
Reaction score
8,253
US bombers have flown close to North Korea's east coast in a show of force, the Pentagon says.
The move is to demonstrate that President Donald Trump has a "range of military options to defeat any threat", spokeswoman Dana White said.
The US and North Korea have ramped up their rhetoric recently.
At the UN on Tuesday, Mr Trump said that he would "totally destroy" North Korea if the US was forced to defend itself or its allies.
 
Ndege za kijeshi za Marekani zimepaa karibu na pwani ya mashariki ya Korea Kaskazini katika kuonyesha ubabe wa kivita, idara ya ulinzi nchini Marekani pentagon imesema.

''Hatua hiyo ni kuonyesha kuwa rais Trump ana njia tofauti za kijeshi kushinda vitisho vyovyote'' , msemaji Dana White alisema.

Marekani na Korea Kaskazini zimerushiana cheche za maneneo katika kipindi cha hivi majuzi.

Katika Umoja wa mataifa siku ya Jumanne, bwana Trump alisema kuwa ataiangamiza Korea Kaskazini iwapo Marekani italazimika kujitetea na washirika wake.

''Hili ni eneo ambalo jeshi lolote halifai kupitia na ni ndege za kijeshi za Marekani ambazo zimeweza kulifikia katika karne ya 21, licha ya tabia mbaya ya Korea Kaskazini'', alisema Bi White.

Tangazo hili lilijiri muda mfupi kabla ya waziri wa kigeni wa Korea Kaskazini kutoa hotuba yake katika umoja wa mataifa .

Mapema siku ya Jumamosi , tetemeko lenye ukubwa wa 3.4 katika vipimo vya Ritcher lilisikika karibu na kituo cha kujaribia makombora cha Korea Kaskazini na kuzua hofu kwamba taifa hilo huenda lilitekeleza jaribio jingine la kombora lake.

Lakini wataalam wamesema kuwa lilikuwa tetemeko la ardhi.

Source: BBC
 
Mmarekani atachapwa na itakiwa haibu.
Ukizingatia china anapiga jalamba akiwa upande wa Pyongyang.
 
Back
Top Bottom