ze kokuyo
JF-Expert Member
- Jan 24, 2014
- 7,476
- 9,654
Jeshi la Urusi limefanya mashambulizi dhidi ya ISIS kwa makombora yake mapya Kh-101 strategic cruise missile. Sehemu za kuhifadhia silaha na kituo cha mawasiliano cha kundi hilo la kigaidi viliharibiwa.
Ndege za kijeshi za Urusi Tu-95 ziliruka toka kambi ya jeshi nchini Urusi kuelekea Syria huku zikijazwa mafuta angani kufanya mashambulizi hayo.
Makombora hayo ya Kh-101 yana uwezo wa kwenda hadi umbali wa 4500 km lakini mahali yalipofyatuliwa ni 1000km toka Syria
MY TAKE; Naona Syria imekua ni sehemu ya kila nchi kujaribu silaha zake kuanzia Marekani, Urusi, Israel, Uturuki, Iran, etc, baada ya Urusi sijui nan atafata kwenda kujaribu silaha yake mpya?!