Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 42
Baba wa taifa alituachia urithi wa umoja wa kitaifa, lakini JK akiwa kiongozi wa CCM na rais wa nchi ameamua kuubomoa umoja wetu Watanzania ambao ulitupatikia heshima si Afrika tu bali ulimwenguni kote. Ni dhahiri kuwa ubaguzi ni urithi ambao Kikwete anaiachia nchi yetu. Kwanza kuanzia kwenye chama chake, uongozi wake umeleta makundi ya kibaguzi. Pili uongozi wake umesababisha umoja wa nchi yetu kuvunjika kwa kupitia udini ambao pamoja na kuwa ni chama chake kimesaidia kuuongeza kasi yake kwa kuuweka katika ilani yake ya uchaguzi lakini ameamua kuupalilia kwa kukaa kimya kabisa. Baba wa Taifa Nyerere aliujenga umoja huo na alikemea vikali pale anapoona hatari za kibaguzi.
Sasa ni kiongozi gani atatusaidia kurejesha umoja wetu wa kitaifa unaopotea badala ya Kikwete mwaka 2010. Je ni Dk. Slaa, labda, je ni Zitto labda. Je ni Shibuda sijui kwa vile napata mashaka kama kuna mtu wa CCM anayeweza kuurejesha umoja wetu kwa vile tayari, JK ameshapanda mbegu ya ubaguzi hata katika chama chake. Kitu ambacho nina uhakika kwa asilimia 100 ni kuwa Lipumba na Seif hawafai kabisa kuungoza nchi hii kwa sababu ni mashabiki wa siasa za udini zinazobomoa umoja wetu chini ya uongozi wa J.K.
Je JK anafahamu kuwa urithi wake kwa Watanzania ni ubaguzi wa kidini na pia ubaguzi na makundi ndani ya chama chake?
Sasa ni kiongozi gani atatusaidia kurejesha umoja wetu wa kitaifa unaopotea badala ya Kikwete mwaka 2010. Je ni Dk. Slaa, labda, je ni Zitto labda. Je ni Shibuda sijui kwa vile napata mashaka kama kuna mtu wa CCM anayeweza kuurejesha umoja wetu kwa vile tayari, JK ameshapanda mbegu ya ubaguzi hata katika chama chake. Kitu ambacho nina uhakika kwa asilimia 100 ni kuwa Lipumba na Seif hawafai kabisa kuungoza nchi hii kwa sababu ni mashabiki wa siasa za udini zinazobomoa umoja wetu chini ya uongozi wa J.K.
Je JK anafahamu kuwa urithi wake kwa Watanzania ni ubaguzi wa kidini na pia ubaguzi na makundi ndani ya chama chake?