babajeska
Senior Member
- Aug 22, 2016
- 157
- 196
Mimi ni mwanachama wa mfuko wa PSSSF niliyechangia miaka kadhaa kabla ya kupoteza ajira kutokana na sababu mbalimbali, mwaka jana (2024) nilifUatilia fao la kukosa ajira nilizungushwa hadi nikaja humu JamiiForums kuleta kilio changu namshukuru Operation Manager alinisaidia.
Pia soma ~ PSSSF Dodoma mama yangu akifa kwa uzembe wa staff wenu hakika jiandaeni kupokea maiti ofisini
Sasa hivi nimekidhi vigezo vya kuhamishiwa uchangiaji wa hiari lakini tangu nianze huo mchakato tangu mwezi wa tano hadi sasa kila siku danadana, kila nikifatilia nauliza labda kuna documents zina mapungufu niambiwe niweke sawa najibiwa hapana, basi nilipeni naambiwa subiri.
PSSSF Kinondoni wananisaidia sana kupush ila tatizo liko Dodoma ndiko kwenye Mungu watu ambao kutimiza majukumu yao hadi wapigiwe simu waombwe wakati ni wajibu wao, yaani kila approve hadi mtu apigiwe simu.
Ukiangalia mabandiko mengi sana humu JamiiForums kuhusu PSSSF tatizo lipo Dodoma, huku kwenye matawi wanajitahidi sana kuwahudumia wateja ila wanakwamishwa na Wadodoma.
Mkurugenzi mpya PSSSF mulika hiyo timu yako ya Dodoma otherwise kila siku malalamiko hayataisha.
Wateja wangapi wanarushwa rushwa hivi? Wastaafu wangapi wanapigwa danadana?
Mtu anayefuatilia mafao yake inamaana amestaafu au bado hana ajira akikamilisha nyaraka zinazotakiwa urasimu wa kufanya malipo unatoka wapi?
Mpeni mtu haki yake akaangalie namna ya kujipambania maisha yake na wategemezi wake. Si busara kila wakati hadi mtu ueleze matatizo yako uhurumiwe ndo upate haki yako.
Ufafanuzi soma hapa ~ PSSSF: Kwa TEHAMA ya PSSSF kila ofisi nchini pote inaweza kumhudumia mteja bila kulazimika kwenda Makao Makuu
Pia soma ~ PSSSF Dodoma mama yangu akifa kwa uzembe wa staff wenu hakika jiandaeni kupokea maiti ofisini
Sasa hivi nimekidhi vigezo vya kuhamishiwa uchangiaji wa hiari lakini tangu nianze huo mchakato tangu mwezi wa tano hadi sasa kila siku danadana, kila nikifatilia nauliza labda kuna documents zina mapungufu niambiwe niweke sawa najibiwa hapana, basi nilipeni naambiwa subiri.
PSSSF Kinondoni wananisaidia sana kupush ila tatizo liko Dodoma ndiko kwenye Mungu watu ambao kutimiza majukumu yao hadi wapigiwe simu waombwe wakati ni wajibu wao, yaani kila approve hadi mtu apigiwe simu.
Ukiangalia mabandiko mengi sana humu JamiiForums kuhusu PSSSF tatizo lipo Dodoma, huku kwenye matawi wanajitahidi sana kuwahudumia wateja ila wanakwamishwa na Wadodoma.
Mkurugenzi mpya PSSSF mulika hiyo timu yako ya Dodoma otherwise kila siku malalamiko hayataisha.
Wateja wangapi wanarushwa rushwa hivi? Wastaafu wangapi wanapigwa danadana?
Mtu anayefuatilia mafao yake inamaana amestaafu au bado hana ajira akikamilisha nyaraka zinazotakiwa urasimu wa kufanya malipo unatoka wapi?
Mpeni mtu haki yake akaangalie namna ya kujipambania maisha yake na wategemezi wake. Si busara kila wakati hadi mtu ueleze matatizo yako uhurumiwe ndo upate haki yako.
Ufafanuzi soma hapa ~ PSSSF: Kwa TEHAMA ya PSSSF kila ofisi nchini pote inaweza kumhudumia mteja bila kulazimika kwenda Makao Makuu