Marco Polo
JF-Expert Member
- Jan 16, 2014
- 13,348
- 21,248
Miezi kama minne iliyopita ni watu wachache sana waliokuwa wakiamini kwamba Dr Magufuli atakuja kuwa Rais wa nchi yetu, Hii ilitokana na mfumo uliokuwepo huko nyuma wa kuchagua mgombea ku-base zaidi kwenye makundi ndani ya Chama na umaarufu wa mgombea.
Kilichomwibua Dr Magufuli ni record yake ya uchapakazi, uadilifu, kutoyumbishwa hovyo hovyo kwa sababu ya kusimamia kile anachokiamini kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla, Hiyo imejidhihirisha zaidi katika wizara zote alizowahi kuziongoza mfano Ujenzi na Miundombinu pamoja na Kilimo na ufugaji.
Fundisho tunalopata hapa ni kwamba usingoje mpaka upewe nafasi kubwa ya utumishi ndio uanze kuonyesha namna ya kuwatumikia wananchi. Piga kazi tu hata kama huna cheo chochote, usingoje mpaka uwe Waziri, Mbunge, M /"kiti serikali ya mtaa, nk
WASIPOKUONA BINADAMU MUNGU ATAKUONA NA KUKUINUA TU.
Kilichomwibua Dr Magufuli ni record yake ya uchapakazi, uadilifu, kutoyumbishwa hovyo hovyo kwa sababu ya kusimamia kile anachokiamini kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla, Hiyo imejidhihirisha zaidi katika wizara zote alizowahi kuziongoza mfano Ujenzi na Miundombinu pamoja na Kilimo na ufugaji.
Fundisho tunalopata hapa ni kwamba usingoje mpaka upewe nafasi kubwa ya utumishi ndio uanze kuonyesha namna ya kuwatumikia wananchi. Piga kazi tu hata kama huna cheo chochote, usingoje mpaka uwe Waziri, Mbunge, M /"kiti serikali ya mtaa, nk
WASIPOKUONA BINADAMU MUNGU ATAKUONA NA KUKUINUA TU.