Nsaji Mpoki
JF-Expert Member
- Nov 5, 2007
- 396
- 65
Tumebakiwa na miaka 2 na nusu hivi tuingie kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Tunaziona hatari nyingi ambazo kama hatutaanza mjadala na uchambuzi wa kina mapema tunaweza kujikuta tunamchagua mtu kuwa Rais wakati hana uwezo kabisa. Taifa hili lina hitaji mtu makini, mwadililifu na mzalendo wa kweli. Tunawaomba sana moderators mruhusu mjadala huu uendelee bila kuingilia mawazo na uhuru wa mtu. Mie naanza kwa kusema ukiondoa dr. Slaa na prof. Lipumba naona prof. Makame Mbarawa anafaa kuwa Rais wa Tanzania