Urais 2015, Rushwa vyaitesa CHADEMA

liwalo na liwe zitto lazima agombee urais na makam wa rais lazima atokee kigoma - kafulila
 
Kama Chadema imegawanyika na itasambaratika soon we kinachokuuma ni nini? Ngoja isambaratike basi ukafanye sherehe!
 
Pumpikin head!
Hollow heads torture m with ignorance.
 
TandaleOne, Tandale pale kwa uwanja wafisi akili lazima iwe ovyo kama wewe vile.Umekubali kutumika kama condom endelea.
 
Last edited by a moderator:
3d za NAPE ukitaka kuzijua ni pale anaposisitiza "Jadili Hoja" huu msemo anaupenda sana kijana pole. Jaribu tena watu tupo kwenye harakati za ukombozi. Hivi viji 3d vyako tunavijua havituumizi.
 

Bahati mbaya moja ya CCM inayowakumba sasa hivi, ni kutumia muda mwingi zaidi kufikiria CHADEMA badala ya kuwajibika. Mnapoteza muda wenu mwingi kweli kweli, kuota ndoto za mchana dhidi ya chama kikuu na mbadala wenu kuchukua dola. Mtasema yote mpaka yataisha maskini nyie, people's power ndo kwanza inasonga mbele kuchukua nafasi yake inayostahili katika jamii ya Watanzania ambayo mnazidi kuipeleka alijojo.

Wajibikeni. Maisha magumu, ufisadi mkubwa, kupanda kwa bei, rushwa ambavyo ni dalili chache tu katika kushindwa kwa CCM na kuendelea kukaribia anguko lake, haziletwi na CHADEMA. Zimesababishwa na uongozi mbovu wa CCM, nothing less, nothing more kaka. Mtaandika sana majungu hapa, mkitaraji mbingu iwe ardhi, haitokeo hivyo!
 

Ukipiga umbea huo, ukimaliza kumbuka hii taarifa hapo chini. Soma kwa makini kwa furaha. Bila shaka utaelewa. Pole. Mengine ya rushwa unajua jinsi mlivyoyalea na kuyafikisha hapa yalipo. Ni moja ya vigezo vya kuwaondoa madarakani.

TAARIFA KWA UMMA






CHADEMA; URAIS UTAAMRIWA KWA MAHITAJI YA UMMA NA SIFA ZA KIONGOZI, SI UTASHI WA WATU/MTU BINAFSI



KUMEKUWEPO taarifa zinazosambazwa kwa umma kupitia njia mbalimbali za upashanaji habari, zikiwa na nia ya kuonesha kuwa kuna mbio za kuwania urais ndani ya chama na kuwa kuna baadhi ya watu wanapewa nafasi kubwa kugombea nafasi hiyo, kiasi kwamba sasa ndani ya CHADEMA "hapatoshi" kwa ajili ya kuwania urais.

Chama kinapenda kutoa taarifa sahihi kwa wanachama, wapenzi, washabiki wake na Watanzania wote kwa ujumla, juu ya suala hili ambalo linaweza kuiweka CHADEMA katika mizania moja vyama vingine au kuwafananisha viongozi wa chama hiki na viongozi wa vyama vingine ambao wamekuwa wakilifanya suala la kugombea nafasi ya urais kuwa linaongozwa na kuamriwa kwa utashi binafsi wa mtu, ukiongozwa na uchu na tamaa ya nafasi ya vyeo.

Kwa sasa ndani ya CHADEMA kitu hicho cha ‘kupamba moto' kwa ajili ya kuwania urais hakipo na wala hakiwezi kuwepo. Hasa kwa sasa ambapo chama kimejikita kuzidi kujijenga kwa kutimiza wajibu wake, kama serikali mbadala inayosubiri kupata ridhaa ya wananchi kuongoza nchi.

Kwa muda huu, kwa CHADEMA suala muhimu ni namna ya kutafuta mizizi au vyanzo vya matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii pana ya Watanzania na kisha kutafuta majawabu au masuluhisho ya kudumu, kwa kushirikiana na Watanzania wote wenye nia njema na nchi yao, kwa ajili ya maendeleo ya watu. Hii ndiyo ajenda muhimu, chama kinasimamia na hakiwezi kutolewa kwenye mstari kwa watu kukimbilia urais.

Kwa CHADEMA, siku zote suala la urais linategemea na kufuata mahitaji mapana ya Watanzania, kamwe haliwezi kuamriwa kwa kufuata matakwa, utashi au uchu wa watu/mtu binafsi. Na katika kufikia hatma ya mahitaji/ maslahi mapana ya wananchi, chama hiki siku zote huamua kwa kufuata na kuzingatia katiba, kanuni na taratibu zake, si vinginevyo.

Ni uwezo na umakini wa kuzingatia mahitaji ya chama na maslahi mapana ya umma katika kuamua masuala mazito kwa mstakabali wa taifa, huku kikifuata katiba yake, kanuni na taratibu, ndiyo umekipambanua CHADEMA kuendelea kuwa chama makini, kinachoaminiwa kwa dhati na Watanzania, na kiupekee kuwa kinastahili kupewa ridhaa ya kuongoza nchi hii.

Mahitaji ya chama na ya Watanzania ndiyo yaliyotumika kupata wagombea urais wa CHADEMA katika chaguzi kuu mbili, mwaka 2005 na 2010. kwa kuzingatia mtazamo huo, mara zote hizo mbili, wagombea waliombwa, wala hawakuongozwa na uchu au tamaa ya madaraka.

Hali itakuwa hivyo hivyo wakati ukiwadia wa kumpata mgombea urais wa mwaka 2015, kamwe utashi, uchu au maslahi binafsi ya mtu hayawezi kupata/kupewa nafasi ndani ya CHADEMA.

Kwa CHADEMA, urais si cheo, ni dhamana ya utumishi kwa umma, suala ambalo linazingatia masuala muhimu, ambayo ni mahitaji ya wananchi (nchi) na kisha sifa za mtu husika kuwa kiongozi wa nafasi hiyo.

Kwa sasa CHADEMA na viongozi wake makini hawawezi kuanza mbio za kusaka urais, badala yake, muda wa sasa unatumika kujikita katika kushughulikia na kutafuta ufumbuzi wa vyanzo vya matatizo ya jamii yanayozidi kuongezeka, huku serikali ikiishia kushughulika na dalili/matokeo, hivyo kukosa majawabu ya kudumu na kuishia kutoa lawama kwa wakosoaji wake.

Hivyo kinachopewa umuhimu ni utumishi kwa umma, kwa ajili ya maendeleo ya watu na si mbio za kusaka vyeo. Ni vyema hii dhana ya mtu kufuatwa na kuombwa, mara anapoonekana kuwa anafaa kuongoza, kulingana na mahitaji ya watu na sifa za nafasi hiyo, kama ambavyo imekuwa ikifanyika ndani ya CHADEMA, ikaenziwa na kufanywa kuwa ni namna bora ya kupata viongozi.

Daima, CHADEMA na viongozi wake makini, kitaendelea kuweka mbele kwanza kabla ya kitu kingine chochote, mapambano dhidi ya vyanzo vya matatizo kama vile umaskini (ugumu wa maisha), rushwa na ufisadi mwingine lukuki unaozidi kutafuna na kuangamiza taifa na watu wake, hali inayowafanya Watanzania kuwa katika mtanziko na mkwamo mkubwa kimaendeleo, miaka 50 baada ya uhuru, huku wakiwa ndani ya taifa lenye baraka tele za utajiri wa rasilimali na kila aina ya nyenzo muhimu inayohitajika kwa maendeleo ya watu. Hii ndiyo ajenda ya muhimu kwa sasa.

Imetolewa leo, Januari 8, 2012, Dar es Salaam
Kurugenzi ya Habari na Uenezi,
Makao Makuu ya CHADEMA Taifa
 
Ilazimishe akili yako kufikiri nje ya box ulilomo..,kama hatoamua kushirikisha ubongo wako ipasavyo katika unayoyasema na kuyaamua daima utaishia kuburuzwa.
Unatumia nguvu kubwa bila sababu huku ukitokwa mapovu kutetea upumbavu wako! Sikushangai kwani najua wazi hizo ndio tabia za wapenda majungu na fitina kama wewe.
 
Naamini katika kweli na naandika katika uhalisia..,i always stand on facts and avoid any guess work..,niliyoyaandika ndiyo yaliyopo. Muda ukiwa kwetu utatuthibitishia haya...!
 
Njoo na CD ningine hii naona imechuja kabla ya kuingizwa sokoni,kaa utunge mistari upya,maana kama cd ya ukanda na ukabila hata ya udini zimesahaulika kwa kutopata mafanikio,leo hii mbona naona haina mvuto?

Nape on work!
 
Sema tujadili majungu, maana hakuna hoja hapa!
i like this. hakyanani CDM tumekomaa kimawazo. jamaa anajaribu kupenyeza jungu, lakini kagonga mwamba. duh!!TandaleOne kajipange upya, hili jungu lako limebuma. mambo yetu CDM tutayamalize wenyewe wala usiwashwewashwe kutubunia uozo hapa. KAJIPANGE KIVINGINE MKUU, OVYOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO!!!!!!!!
 
Jadili hoja..,ukishindwa kaa kimya.

Kuna hoja gani mkuu ya kujadil kama siyo umbea tu? Kwa Mfano, Mwenye sired anadai kuwa mikoa ya Katavi na Rukwa ina muunga mkono Zitto, utafiti huo ameufanya wapi? Lini sisi wana Katavi tumetanganza kumuunga mkono Zitto? Hakuna kitu kama hicho, hata kama mimi siyo msemaji wa mkoa, lakini nipo hapa mjini Mpanda, sijasikia kitu kama hicho. UMBEA TU. Hakuna hoja ya kujadili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…