Upuuzi wa TBC1: Rais Kikwete atukanwa 'live'

Hivi hii ni HABARI LEO au habari jana.........??
 
Kwa nini munashambulia gazeti badala ya kujibu hoja kama aliyoyasema huyo mgombea ubunge ni sahihi au siyo katika mila za hapa kwetu Tanzania?

Nadhani haifai kwenda kwenye extreme na kuanza kumsema mama yake fulani hana adabu. Jee ingekuwa ni wewe ungefurahi kutukanwa mama yako kwa kuambiwa hakukufunza?

Wazee wetu lazima tuwaheshimu na inatia uchungu kama mtu atakutukania au kumkejeli mzazi wako.
 
wapinzani ni fotokopi sawsawa? kikwete hajafunzwa na mamaye sawasawa? anayeona katukanwa aende mahakamani.binafsi sipendi matusi awe mdogo au mkubwa ila nasisitiza asiye na adabu afunzwe adabu j"pili.
 
sidhani kama ni matusi ambayo hayawezi kuandikwa ila si kwamba ninasupport maneno hayo laikini nionavyo huyu mwandishi naye ameyakuza sana:bowl:
 
Angalizo:
Dickson Amos Ng'hily alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha CCJ (Bara) kilichokufa na baadaye kuhamia CHADEMA July 2010, Hivyo bado hajakomaa sana ndani ya CHADEMA inabidi tumpige semina na msasa wa namna gani ya kuongea ukiwa mwanasiasa. Maana unaweza kutumia methali nzuri lakini isipostahili na wapinzani wako(CCM) wakaigeuza wanavyotaka wao ieleweke na kuishia kukaangwa na jamii kisiasa.
 
Kuwa mjinga ni kufanywa mjinga, usikubali kuwa mjinga kwa kufanywa mjinga. Haa haaaa mkuu bado unasoma magazeti ya udaku ya ccm pole sana. Ila usiwe unatuletea sisi hapa.
 
Leo katika taarifa ya habari channel ten nimemwona kikwete akisema kwamba ametukanwa na wapinzani wana midomo michafu iliyojaa matusi. baadae wakaonesha kinana akisema kwamba watashtaki tume kuwa wametukanwa.

Halafu sijaona channel ten wakitoa habari za mgombea hata wa cuf au yeyote wa uchaguzi zaidi ya wa ccm. halafu kwenye matangazo ya mapumziko ya habari wanatangaza ccm. sasa najiuliza hawa kweli ndo wale ambao walishikia kidedea kuhusu north mara? mbona wapo sooo pro kikwete badala pro tanzanians?

Kuna haja ya hizi taasisi kushtakiwa baada ya uchaguzi ili wawajibishwe kwa sheria zilizopo kwani mkiwapeleka tume ya mawasiliano wataishia kupewa barua ya onyo tu wala hawatajifunza
 
Nakubaliana asilimia mia moja na wanaopinga alichokifanya huyu Dickson Amos Ng'hily, kwa kweli si uungwana kabisa sababu chama chetu ni cha kiungwana. Huyu jamaa amekosa umakini na hajui matumizi mazuri ya muda. Nafkiri hata kwa waliofuatilia wanaweza kusema kwamba hicho kitendo chake hakikupokelewa vizuri hata na waliokua wakimsikiliza. Kwa nini wameamua kumsimamisha mtu ambaye hajakomaa CHADEMA?

Dkt ni mtu makini sana na naamini wengi wenu mlimuelewa alichokisema mwisho kuhusu nini kifanyike kama ukifanyiwa kitu cha kuudhiwa (Lugha mbaya) na watu wanaoamini chama kingine. Unawedha kufahamu (Kwa mtazamo wangu) Alikua akimfunza Bw. Ng'hily jinsi ya kupambana na wenzetu maana wao wamezoea kufanya hivyo.


Leo katika taarifa ya habari channel ten nimemwona kikwete akisema kwamba ametukanwa na wapinzani wana midomo michafu iliyojaa matusi. baadae wakaonesha kinana akisema kwamba watashtaki tume kuwa wametukanwa.

TBC mkuu wetu kasema wenzie MAJUHA yaani wale waliokutana jana Mwembe Yanga! Pia ametumia matusi, lakini hii inaonesha ni kwa kiasi gani huyu jamaa hastahili kuongezewa miaka mitano ijayo maana anamkimbiza kichaa aliechukua nguo zake wakati yeye anaoga mtoni.
 
:nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono: sijaona tusi,dk slaa yupo sahihi na huyo mbunge yupo sahihi
 
Mbunge yuko sahihi kabisa. Kwani Kikwete alivyosema watu wenye ukimwi wameupata kwa sababu ya kiherehere chako hakua amewakosea adabu hao watu? Kwani Kikwete alivyosema wanafunzi wanaopata mimba wamepata hizo mimba kwa sababu ya kiherehere chako hakua amewakose adabu hao wanafunzi? Kikwete hana adabu tena hana adabu sana tu. Na kama mama yake alimfundisha adabu, sasa mbona hatuoni kama anayo. Kwa baadhi yetu, tunaona kuwa mama yake ka alimfunza adabu hakuielewa au hakumfunza kabisa. Ni wajibu wetu sisi sasa tumfunze hio adabu.
 

Mkuu labda matusi ni kusoma report ya kawambwa ya utekelezaji wa ilani ya CCM bagamoyo ambayo matundu manne ya choo yamejengwa kwa mil 700
 
Sasaungefafanua tusi liko wapi? Hivi wewe unaridhika na CCM inavyoendeshwa kifamilia?Rais kuwasafisha mafisadi ni sawa? Ina maana hana washauri au hasikii la Mtu? Sasaasiyefunzwa na Mamaye ni yupe kama si huyo anayekiuka katiba aliyoapa kuilinda.Fafanua au na wewe tukuone ni haohao.
 
Kwa jinsi JK anavyoendesha CCM ni matusi kwani amewatenga waasisi na kukumbatia mafisadi na wanafamilia/marafiki.
 
Mara nyingi inategemea mlengwa atalichukuliaje neno analoambiwa na mwenzake. Kwa hali hiyo neno lolote ukimwambia mtu mwingine lakini yeye akalitafsiri kimatusi linaweza kuwa ni tusi kwake. Lakini katika hili hakuna tusi, hapa ni kuonyesha umahiri katika lugha yetu ya kiswahili ambayo bahati mbaya sana kwasasa Watanzania wengi inatupiga chenga. Mgombea ubunge jimbo la Temeke kupitia CHADEMA, katika kusisitiza hoja yake alimalizia na methali -"asiyefunzwa na mamaye, hufunzwa na ulimwengu". Hii ni methali nzuri tuu ya kiswahili na wala katika matusi yaliyomo kwenye kamusi haipo. Kama CCM wameshitaki ilhali wao ndio waoongoza kwa kutukana washindani, basi swali kwao ni hili: mkuki kwa nguruwe kwa binaadamu mchungu? au chongo kwa mnyamwezi kwa mzaramo ni kengeza?

"Moringe wote ni wamasai lakini sio kila mmasai ni Moringe"
 
Kama ninavyosema humu wengi ni CHADEMA. Kwangu mkishinda itakuwa heri kwa kuwa yale mnayodhani sio matusi ndiyo tutakayomtamkia DR Slaa atakapokuwa Raisi, tuone kama mtastahimili. Hatahivyo nina uhakika hamtashinda kwa kura kiduchu za humu. TCHAOOOOOO!
 
Nalichukia hili gazeti kwa moyo wangu wote, nawe mhariri mkuu ukae mkao wa kufunga virago nchi itakaporudishwa kwa watanzania wenyewe hapo october 31.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…