Mimi nimelelewa na mama wa kambo 3 ..nimeanza kuishi na mama wa kambo nikiwa na miaka 7.. Miaka 3 baadae baba aliacha akaoa mwingine,,yule wa kwanza hakuwa mbaya ,,,labda alikuwa kipindi nipo mdogo sana,,,alizaa nae watoto 2 , ,,waliachana na baba ,,baadae aliondoka na mtoto mmoja,,mwingine alimwacha pale kwa baba,, mama wa pili alikaa na baba kwa miaka 2 naye alipata mtoto mmoja ,,, baadae baba akawa Mara harudi Mara week hatumuoni,,pale NYUMBANI nilibaki Mimi,,na ndugu yangu mtoto wa mama yangu yule wa kwnza,,,,huyu mama wa pili nae hakuwa mbaya, alikuwa akitupenda tu..sana hakuwa na shida... Siku moja baba alirudi akatuchukuwa mimi na mdogo wangu ,,,akatupeleka mahali Fulani,,si mbali sana na NYUMBANI,, kufika tukapokelewa vizuri sana,,akatwambiya kuanzia Leo mtaishi hapa,,,na hyu ndy mama YENU mpya,,,kipindi hicho nipo darasa la 5 .. HAPO NDY MAISHA HALISI YA MAMA WA KAMBO NIKAYAPATA...pale NYUMBANI Tulikuta yule mama ana watoto wake 2 WASICHANA wakubwa tu zaidi yetu..na tayari walikuwa wameshazalishwa,,,baada ya miezi Kama 2 yule mama yangu wa kambo wa pili nae akaja kumleta MWANAE pale kwa baba ,,,akamtelekeza pale,, yule mama hajarudi kutafuta MWANAE hadi Leo...hyo ILIKUWA mwaka 1988....mdogo wangu alikuwa na mwaka mmoja tu...BASI maisha yalikuwa ya taabu sana pale,,,nyumbani, Kwanza KUTUMWA BILA KIPIMO...Kanunuwe mkaa,,dk kumi unarudishwa tena GENGENI kanunuwe mafuta , hujakaa sawa tena nenda kanunuwe chumvi,,,na ukisema utoke ukacheze ukirudi hakuna chakula,,,MTEMBEZI HULA MIGUU YAKE...HUYU MAMA NI HATARI SANA,,,,kulikuwa na house girl lakini nikiwepo Mimi yeye hatumwi...sometimes NARUDI nataka niende tuition naambiwa NIENDE MASHINE,, KUKOBOA MAHINDI..nikifika nakuta foleni kubwa sana,,kuna mashine ILIKUWA pale TRAVETINE MAGOMENI..basi nikishakoboa NARUDI HOME wanapeta mahindi NARUDI KUSAGA TENA. ,..mimi natoka MBALI KUFATA MASHINE...ilikuwa ni UMBALI MREFU SANA,,,,kwa kifupi ILIKUWA ni kama kunifanya nisiende tuition...mdogo wangu akijisaidia basi haoshwi hadi nirudi mimi SHULE,, baba yangu hakuwahi kunipiga hata Kofi,,lakini kwa mama huyu ilikuwa ni makofi kila siku,,maana kila siku kesi za kusingiziwa,,,CHOO CHENYEWE MLANGO WA GUNIA,,,MTU ANAOGA ukipita anasema mwanao ananichungulia CHOONI,,CHAKULA kwenye kisahani cha chai,,kwa kweli huyu mama alikuwa MIYAYUSHO SANA,,,nikipofika STD 7 ..MUNGU ALIJAALIA NILICHAGULIWA KUJIUNGA NA AZANIA SEC SCHOOL...aisee,,yule mama ilimuuma sana,,na pale ilikuwa tunaishi kwenye nyumba ya yule mama,,lilikuwa banda Fulani bovu,,baba aliitengeneza ikawa inatizamika,,,sijuwi alipatwa na NINI MZEE wangu,, yule mama akamwambiya baba yangu hataki Mimi niishi pale tena ,,aondoke yeye ,au niondoke Mimi,, basi baba akaniondoa kwa shingo upande,, akanipeleka kwa mjomba wake niishi....kwakweli story ni ndefu sana...naomba niishie hapa MKUU... nitaleta tena maisha ya kwa mjomba wa baba SIKU ingine..LAKINI kwa kifupi mama wa kambo kumpata aliyekuwa BORA NI BAHATI SANA,,WENGI wao wana pretend.... KUTENGENEZA MAPENZI BAINA YAKE NA MUME,, ,mwisho wa siku mama anatia sumu kwa baba ili awachukie watoto wake... Nakusihi kama una UWEZO Lea wanao PEKE YAKO NA HOUSE GIRL,, ukipata MWANAMKE malizana nae HUKO HUKO NJE..au mpangie sehem ingine,,nakuhakikishia UTAKUWA LULU KWA WATOTO WAKO....kukaribisha mama wa kambo ni KUTOA SADAKA MAPENZI YAKO NA WATOTO WAKO..na hata JITAHIDI KUISHI NA MKEO VYEMA ili mlee watoto wenu pamoja....hata huko kwa mjomba wa baba pia nilipatwa na VISANGA VINGI SANA , LAKINI VILINIFANYA NIWE STRONG BOY...na KUINGIA kwenye maisha ya UBAHARIA HADI SASA.... hii ni TRUE STORY OF MY LIFE....
Sent using
Jamii Forums mobile app