tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 26,021
- 25,423
Tangu zamani Umoja wa Wanawake wa CCM (UWCCM) umekuwa ukijiita Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) kana kwamba wanawake wote nchini Tanzania ni wanachama wa umoja huo.
Imefika wakati sasa matumizi ya jina hili yasitishwe kwani linawapotosha na kuwavuruga wanawake wa Tanzania, hasa wale wa vijijini ambao hawana elimu ya uraia ya kutosha.
Kila chama cha siasa sasa kina umoja wa wanawake kama vile CHADEMA (BAWACHA), CUF (BAWAC), nk. Sio sahihi UWCCM kuendelea kutumia jina la UWT kinyume na maudhumuni ya umoja huo. Mbona UVCCM haiitwi UVT?
UWT ni chama kinachotetea maslahi ya kikundi kidogo cha wanachama ndani ya CCM na sio Tanzania nzima kama jina lake linavyosomeka. Hivyo basi matumizi ya jina la UWT ni batili na upotoshaji wa makusudi.
Umoja unaotetea maslahi ya mafisadi wachache ndani ya nchi hawawezi kujidai kujitwika maslahi ya wanawake wote nchini wakati hawafanyi hivyo. Acheni kutenda kazi kwa misingi ya kilaghai huku mkiwapaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa.
Nawasilisha.
:israel:
Imefika wakati sasa matumizi ya jina hili yasitishwe kwani linawapotosha na kuwavuruga wanawake wa Tanzania, hasa wale wa vijijini ambao hawana elimu ya uraia ya kutosha.
Kila chama cha siasa sasa kina umoja wa wanawake kama vile CHADEMA (BAWACHA), CUF (BAWAC), nk. Sio sahihi UWCCM kuendelea kutumia jina la UWT kinyume na maudhumuni ya umoja huo. Mbona UVCCM haiitwi UVT?
UWT ni chama kinachotetea maslahi ya kikundi kidogo cha wanachama ndani ya CCM na sio Tanzania nzima kama jina lake linavyosomeka. Hivyo basi matumizi ya jina la UWT ni batili na upotoshaji wa makusudi.
Umoja unaotetea maslahi ya mafisadi wachache ndani ya nchi hawawezi kujidai kujitwika maslahi ya wanawake wote nchini wakati hawafanyi hivyo. Acheni kutenda kazi kwa misingi ya kilaghai huku mkiwapaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa.
Nawasilisha.
:israel: