Upotolo wa simu yangu

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,579
Reaction score
161,432
Simu yangu ni utopolo mtupu, unaweza ukawa uko kwenye application nyingine kabisa ie uko kwenye chrome, mara ghafla unakuta simu inajipiga yenyewe kwa namba yoyote ya kwenye phone book.

Ukiiweka mfukoni unakuta imejirekodi mavideo na imejipiga mapicha zaidi ya buku.

Betri inapata moto sana kiasi kwamba kama simu iko mfukoni inakuunguza kabisa. Inabidi uizime na uiache ipoe.

Simu hii ikiwa mfukoni unakuta imejituma meseji ya ajabu na inajituma kwa mtu yoyote, na muhanga mkubwa ni baba mkwe.

Kuna siku ilijituma SMS kuwa ninaomba hela ya kula, na kuna siku ikajituma sms kwa ex-girlfriend wangu kuwa I love you, without you I am nothing.

Pia hi simu haikai kabisa na chaji. Ikiwa full charge, baada ya masaa matatu Inakubudi uiweke Tena chaji.

Simu iko slow, ukifungua browser, unaweza kukaa dakika sita huoni herufi

Hii simu nimeinunua kwenye duka la Tigo, mwishoni mwa mwezi wa sita. Aina ya simu ni tecno S3
Ndugu zetu TECNO Tanzania 🇹🇿 ongeeni na Wachina wenu waboreshe bidhaa.
 
hebu weka hapa hayo mapicha na mavideo inayojipia tu ovyo ovyo!
 
Mimi juzi nimekoma na tecno, nimetoa line,kwenye simu nikaweka kwenye simu ingine,ila ukipiga inaita kwenye simu ileile niliyotoa line
ha ha ha ha ha hiyo imeshindikana boss!
 
Hii hii unayotumia humu JF mkuu? Kama ni hiyo amini ni nzima mkuu.

Kuna moja wakati smart zinatoka ilikuwa ni M3, ilkuwa inajifungua saiti za porn tu, na kuitoa sasa hiyo sehemu haitoki mpaka uzime.
Hapana mzee, huwezi hate ku type, ukiandika Mama inaweza kukugharimu zaidi ya sekunde ishirini, simu imeganda tu hewani. Ikija kuandika inaandika neno inaloamua yenyewe
 
Dah leo umeua kabisa, yaani ata watumia techno feki hawapati huo usumbufu,

Usiitupe hiyo simu kuna siku utakuta imeshinda tatu mzuka, sport pesa milion 500, utashangaa inakuombea u DAS, DC kwa JPM,

Bahati mbaya TALA hawapo tena duniani
 
Dah leo umeua kabisa, yaani ata watumia techno feki hawapati huo usumbufu,

Usiitupe hiyo simu kuna siku utakuta imeshinda tatu mzuka, sport pesa milion 500, utashangaa inakuombea u DAS, DC kwa JPM,

Bahati mbaya TALA hawapo tena duniani
Hahaha
 
Hiyo ni Hali ya kawaida kwa sisi watumiaji nguli wa tecno, tunao elewa maana ya tecno huwa hatukai na simu zaid ya mwaka 1 tunauza ikafie kwa mtu mwngne
 
Naweza ifananisha na hii yangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…