BungelaKatiba2014tz
JF-Expert Member
- Feb 18, 2014
- 1,231
- 649
Baada ya juhudi za Lowassa na Mbowe kumshawishi Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye ajiunge na CHADEMA kuonekana kutozaa matunda, sasa Mwanasisa huyo mwenye sifa ya kupiga vita ufisadi ameamua kubadilisha uwamuzi wake na kuitikia wito wa Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT), ALEX MALASULA.
Kiongozi huyo wa kiroho amemuomba Sumaye kumuunga mkono Mlutheri mwenzake(Lowassa) katika harakati zake za kuwania nafasi ya kuingia Ikulu baada ya uchaguzi hapo mwezi Oktoba mwaka huu.
Itakumbukwa kuwa 30/12/2013, wakati wa uzinduzi wa Kanisa la LOLE, Usharika wa Mwika katika Diosisi ya Kaskazini, Mwenyekiti wa Chadema , Freeman Mbowe alimuomba SUMAYE ajiunge na Chadema kwa vile yeye ni mpiga vita ufisadi mzuri, vita ambayo kwa wakati huo ndiyo ilikuwa agenga ya CHADEMA.
LEO au siku ya Uzinduzi wa Kampeni za Chadema, Sumaye atatangaza kukihama chama cha Mapinduzi na kujiunga na Chadema. Hata hivyo Sumaye anakwenda CHADEMA, chama ambacho mgombea urais wake alituhumiwa sana na bwana Sumaye kuwa fisadi hadi kufikia hatua ya kufikiria kuchukua maamuzi magumu endapo CCM ingempitisha(LOWASSA) kuwa mgombea urais kupitia chama hicho ambacho kimewalea wote SUMAYE na LOWASSA.
Kiongozi huyo wa kiroho amemuomba Sumaye kumuunga mkono Mlutheri mwenzake(Lowassa) katika harakati zake za kuwania nafasi ya kuingia Ikulu baada ya uchaguzi hapo mwezi Oktoba mwaka huu.
Itakumbukwa kuwa 30/12/2013, wakati wa uzinduzi wa Kanisa la LOLE, Usharika wa Mwika katika Diosisi ya Kaskazini, Mwenyekiti wa Chadema , Freeman Mbowe alimuomba SUMAYE ajiunge na Chadema kwa vile yeye ni mpiga vita ufisadi mzuri, vita ambayo kwa wakati huo ndiyo ilikuwa agenga ya CHADEMA.
LEO au siku ya Uzinduzi wa Kampeni za Chadema, Sumaye atatangaza kukihama chama cha Mapinduzi na kujiunga na Chadema. Hata hivyo Sumaye anakwenda CHADEMA, chama ambacho mgombea urais wake alituhumiwa sana na bwana Sumaye kuwa fisadi hadi kufikia hatua ya kufikiria kuchukua maamuzi magumu endapo CCM ingempitisha(LOWASSA) kuwa mgombea urais kupitia chama hicho ambacho kimewalea wote SUMAYE na LOWASSA.