Upinzani hawajui jinsi ya kushirikiana na serikali na viongozi wake kuleta maendeleo

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,908
51,904
Katika vitu ambavyo kwa utafiti nimevigundua ni kuwa viongozi wa upinzani hawajui namna ya kufanya kazi na viongozi wa serikali kwenye maeneo yao ili kuleta maendeleo eneo husika.Unakuta mtu kachaguliwa kuwa diwani,mbunge au meya anaota mapembe anajiona kama vile yeye ni raisi wa eneo husika na hana haja ya kushirikiana na kiongozi yeyote wa serikali kwa lolote awe wa wilaya,mji,jiji,mkoa ,wizara nk.

Hawaelewi kuwa hata ukipata pesa za msaada wa kufanya kitu katika eneo lazima ushirikishe serikali kwanza kabla ya kufanya huo mradi hata kama unataka kuufanya kwa pesa zako.MFANO MTU UKIWA meya umepewa pesa za msaada wa kujenga hospitali kubwa kama ya muhimbili na wafadhili huwezi ibuka tu ukasema mimi nina pesa zangu najenga sihitaji cha mkuu wa mkoa wala waziri wala nani.

Ukianza process waweza kataliwa na serikali kujenga hiyo hospitali yako.Sababu kubwa ni kuwa misaada nayo huratibiwa.Mfadhili akijenga hilo hospitali na kuweka kila kitu mbeleni nani atagharimia uendeshaji wa hiyo Hospitali? Lazima kieleweke sababu kama baadaye madaktari na gharama zote mradi ukikamilika serikali ndio itawajibika kugharimia

Ina maana huo msaada umekuja kuongeza matumizi ya serikali mbeleni wakati serikali haijajipanga kwenye hilo kwani matumizi kuongezeka ina maana serikali mbeleni itawajibika kuongeza kodi ili ipate pesa za kuendesha hilo hospitali koko la msaada lililokuja ghafla bila kuwekwa kwenye mipango ya maendeleo ya serikali.

Hata ukiwa na pesa za kujenga kituo cha polisi lazima uongee na serikali sababu ijipange kuajiri askari wapya kwa ajili ya hicho kituo na gharama zingine za uendeshaji mbeleni. Tatizo la viongozi wa upinzani waliochaguliwa wanadhani unaweza ishi bila serikali na shughuli zako zikaenda sio kweli kuna maeneo ukifika utakwama.

Wanatakiwa wajitahidi mno kutokuwa na BIFU na serikali.Iwe na polisi au kiongozi yeyote wa serikali kama kweli wamepania kuleta maendeleo kwenye maeneo yao.Kila wanachotaka kufanya washirikishe serikali kuanzia hatua za mwanzo kabisa ili viwekwe kwenye mipango ya maendeleo ya serikali.

Ushauri wangu kama hawajui jinsi ya kufanya kazi na serikali watafute washauri toka nchi zilizoendelea wawashauri.Na wanatakiwa wajue kuwa wamechaguliwa na watu wote sio wa vyama vyao tu.Hivyo wakati wa utumishi wao wasiweke jeuri ya vyama vyao mbele bali maslahi mapana ya walio wengi waliowachagua ambao wengi wao si wanachama wa vyama vyao
 
Mkuu Yehodaya andiko lako limeegemea upande mmoja ,kama ungejitahidi kuwa neutral ingekuwa vyema zaidi.Kwamba pande zote ziweke masilahi ya wananchi mbele mambo ya vyama na vyeo yawekwe kando.
 
Vise versa is true
Mkuu nimeshangaa nilichoandika ndicho ulichoandika. Bila shaka hiyo ni ishara ya kuwepo ukweli kwenye comments zetu. Ukifuatilia malalamiko ya meya wa Kinondoni kuhusu kunyanyapaliwa na kutokupewa ushirikiano na serikali ni wazi kwamba tatizo lipo serikalini na sio kwa CDM. Angalia wakuu wa mikoa na wilaya Arusha na Dar es salaam wanavyolalamikiwa na CDM. Tena kinachoshangaza ni pale mtu ambaye hakuchaguliwa anashindana na madiwani na wabunge!!!!
Vice versa is true.
 
Tena kinachoshangaza ni pale mtu ambaye hakuchaguliwa anashindana na madiwani na wabunge!!!!

Hapa ndipo tatizo la upinzani lilipo.Mtu kuchaguliwa kuwa mwakilishi wa wananchi sio kwamba wamekuchagua wewe kuwa serikali!!!! Umechaguliwa ukawakilishe matatizo ya wananchi serikalini ili serikali ikayafanyie kazi.Hawajakuchagua kuwa mkuu wa wilaya wala mkuu wa mkoa!!! Wamekuchagua kuwa wewe mwakilishi wetu nenda kaongee na mkuu wa wilaya au mkoa kwa niaba yetu kwa kuwa sisi sote hatuwezi kwenda huko.

Sasa tatizo linakuja unakuta huyo mbunge au diwani akivaa ka kaunda suti kake si mbwembwe hizo anatembea kwa mikogo ile ya Kipofu kaona mwezi!! anaanza kufokea mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa kuwa mimi nimechaguliwa!!! Umechaguliwa kitu gani umechaguliwa kuwakilisha matatizo tu ya wananchi serikalini au bungeni .Full stop.

Tabia ya ku-behave kama wao wako juu ya wakuu wa wilaya au mikoa inaonyesha hata hawajielewi wamechaguliwa kwa ajili ya kitu gani hasa! Wao hawana bajeti,serikali ndio yenye bajeti ya wilaya,mikoa au wizara.Sasa ukiamua kumbinulia midomo mkuu wa wilaya au mkoa na kaunda suti yako ya mtumba unamtishia nani nyau? Kinachotakiwa mchaguliwa yeyote awe nba ushirikiano na serikali yenye bajeti ili kutekeleza ahadi alizoahidi alipogombea.

Ukweli wengi hawajielewi wamelewa kura walizopata wanasahau lengo walilopigiwa hizo kura
 
Tatizo lenu kubwa, hamjiamini, mna hofu na kulalamika kila siku. Kila siku sbb tu, mkishindwa kufanya jambo fulani mnasingizia upinzani.
Ajira hakuna mnasingizia uhakiki hewa, tax & vat kubwa mnasingizia upinzani. Km ufisadi na rushwa nyie wenyew meuleta.
Nawachukia sana nyie kijani. Kila siku mnazidi kuharibu tu. Tumekaribia kuwapoteza km KANU. Kila siku nikukimbizana na upinzani tu, eti upinzan unakwamisha maendeleo. Hiki ndicho mlichobakiza na kukifanya kuwa wimbo wenu
.Nasikia ajira mpya nazo upinzani wamekwamisha
Uchumi umedorora
 
Hapa ndipo tatizo la upoinzani lilipo.Mtu kuchaguliwa kuwa mwakilishi wa wananchi sio kwamba wamekuchagua wewe kuwa serikali!!!! Umechaguliwa ukawakilishe matatizo ya wananchi serikalini ili serikali ikayafanyie kazi.Hawajakuchagua kuwa mkuu wa wilaya wala mkuu wa mkoa!!! Wamekuchagua kuwa wewe mwakilishi wetu nenda kaongee na mkuu wa wilaya au mkoa kwa niaba yetu kwa kuwa sisi sote hatuwezi kwenda huko.Sasa tatizo linakuja unakuta huyo mbunge au diwani akivaa ka kaunda suti kake si mbwembwe hizo anatembea kwa mikogo ile ya Kipofu kaona mwezi!! anaanza kufokea mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa kuwa mimi nimechaguliwa!!! Umechaguliwa kitu gani umechaguliwa kuwakilisha matatizo tu ya wananchi serikalini au bungeni .Full stop.

Tabia ya ku-behave kama wao wako juu ya wakuu wa wilaya au mikoa inaonyesha hata hawajielewi wamechaguliwa kwa ajili ya kitu gani hasa! Wao hawana bajeti,serikali ndio yenye bajeti ya wilaya,mikoa au wizara.Sasa ukiamua kumbinulia midomo mkuu wa wilaya au mkoa na kaunda suti yako ya mtumba unamtishia nani nyau? Kinachotakiwa mchaguliwa yeyote awe nba ushirikiano na serikali yenye bajeti ili kutekeleza ahadi alizoahidi alipogombea.

Ukweli wengi hawajielewi wamelewa kura walizopata wanasahau lengo walilopigiwa hizo kura
Jambo la msingi ni kwamba, hao wakuu wa mikoa na wilaya wanakubaliwa na jamii wanayoiongoza? Usitumie nguvu nyingi kutaka kuwaamisha watu kwamba CDM/ukawa ndio kikwazo cha maendeleo wakati watu tuna akili zetu timamu. Leo itokee kuna uchaguzi jimbo la ubungo au kibamba unadhani makonda amaweza kusimama mbele ya makonda au mnyika?

Inaonekana hujui majukumu ya wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na wabunge na madiwani.
 
Jambo la msingi ni kwamba, hao wakuu wa mikoa na wilaya wanakubaliwa na jamii wanayoiongoza?

Mkuu wa wilaya au mkoa sio mwanasiasa.Anapofika mahali haendi kutafuta kupendwa au kutopendwa sababu hana mpango wa kuomba kura.Yeye kaenda pale kuhakikisha barabara zinajengwa,shule zinapata madawati,madaraja yanajengwa ,huduma za jamii za maji,umeme nk zinapatikana hajaenda kuuza sura kwa wapiga kura .Hiyo kazi ya kujipitisha kwa wananchi ni ya wabunge na madiwani.Tatizo lingine wanalokosea upinzani wanadhani mkuu wa wilaya au mkoa ni diwani au mbunge mwenzao!!!! Mkuu wa mkoa na wilaya kazi yake kusimamia mkoa na wilaya hata kama ni wa upinzani wote yeye kazi yake ni kusimamia kazi za serikali katika mkoa husika watu wamtake wasimtake yeye sio mwanasiasa kama mbunge na diwani.
 
Unamtaka mpinzani ashirikiane na serikali katika kuleta maendeleo wakati huohuo hutaki serikali ishirikiane na upinzani katika kutatua kero za wananchi..leo hii mkuu wa wilaya kawa kama mbunge anauwezo wa kumdindia Meya kisa huyo Meya anatoka Upinzani akifanya vitu vyenye tija atakiongezea nguvu chama chake,hivyo anaona bora aharibu tu ila analolitaka yeye anataka hadi mpinzani alifanye wewe kama nani nchi hi? Mtu ameteuliwa na boss wake anaonyesha umwamba badala ya kufanya kazi huku akitaka kujifananisha na mtu aliechaguliwa kwa kula za wananchi.
 
Mkuu wa wilaya au mkoa sio mwanasiasa.Anapofika mahali haendi kutafuta kupendwa au kutopendwa sababu hana mpango wa kuomba kura.Yeye kaenda pale kuhakikisha barabara zinajengwa,shule zinapata madawati,madaraja yanajengwa ,huduma za jamii za maji,umeme nk zinapatikana hajaenda kuuza sura kwa wapiga kura .Hiyo kazi ya kujipitisha kwa wananchi ni ya wabunge na madiwani.Tatizo lingine wanalokosea upinzani wanadhani mkuu wa wilaya ni diwani au mbunge mwenzao!!!! Mkuu wa mkoa na wilaya kazi yake kusimamia mkoa na wilaya hata kama ni wa upinzani wote yeye kazi yake ni kusimamia kazi za serikali katika mkoa husika watu wamtake wasimtake yeye sio mwanasiasa kama mbunge na diwani.

Hilo umelisema wewe. Siku hizi watu wamesoma na kuelimika. Ukimwambia mtu kwamba makonda au gambo sio wanasiasa atakudharau na kukuona huna akili. Nitajie wakuu wa mikoa au wilaya ambao sio wanasiasa tukiachana na wale wanajeshi walioteuliwa kwa ajili ya mikoa ya mipakani.
 
Mtu ameteuliwa na boss wake anaonyesha umwamba badala ya kufanya kazi huku akitaka kujifananisha na mtu aliechaguliwa kwa kula za wananchi.

Ameteuliwa na bosi yupi? BOSI aliyemteua kapewa ridhaa na wananchi nchi nzima kwa kura za kishindo ateue watu wa kufanya naye kazi.Kura za kishindo za WANANCHI NA katiba vimempa hayo mamlaka ya kuteua.Huyo aliyeteua huwezi kumlingani na vikura vya mtaani alivyopata diwani au mbunge.Aliyemteua ujue ndiye aliyembwaga chini mgombea wenu LOWASA au hilo kichwani limewatoka ghafla.Msilisahau hilo

Huyo aliyeteuliwa kateuliwa kwa mujibu wa katiba ya nchi na sheria.Ndizo zimemuweka madarakani.Kumdharau ni kudharau katiba na sheria iliyomuweka.Hao ni sawa na majaji huwezi dharau jaji kuwa eti kateuliwa asijitutumue kuliko wewe uliyepigiwa kura!
 
Hapa ndipo tatizo la upoinzani lilipo.Mtu kuchaguliwa kuwa mwakilishi wa wananchi sio kwamba wamekuchagua wewe kuwa serikali!!!! Umechaguliwa ukawakilishe matatizo ya wananchi serikalini ili serikali ikayafanyie kazi.Hawajakuchagua kuwa mkuu wa wilaya wala mkuu wa mkoa!!! Wamekuchagua kuwa wewe mwakilishi wetu nenda kaongee na mkuu wa wilaya au mkoa kwa niaba yetu kwa kuwa sisi sote hatuwezi kwenda huko.Sasa tatizo linakuja unakuta huyo mbunge au diwani akivaa ka kaunda suti kake si mbwembwe hizo anatembea kwa mikogo ile ya Kipofu kaona mwezi!! anaanza kufokea mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa kuwa mimi nimechaguliwa!!! Umechaguliwa kitu gani umechaguliwa kuwakilisha matatizo tu ya wananchi serikalini au bungeni .Full stop.

Tabia ya ku-behave kama wao wako juu ya wakuu wa wilaya au mikoa inaonyesha hata hawajielewi wamechaguliwa kwa ajili ya kitu gani hasa! Wao hawana bajeti,serikali ndio yenye bajeti ya wilaya,mikoa au wizara.Sasa ukiamua kumbinulia midomo mkuu wa wilaya au mkoa na kaunda suti yako ya mtumba unamtishia nani nyau? Kinachotakiwa mchaguliwa yeyote awe nba ushirikiano na serikali yenye bajeti ili kutekeleza ahadi alizoahidi alipogombea.

Ukweli wengi hawajielewi wamelewa kura walizopata wanasahau lengo walilopigiwa hizo kura
Binafisi nimekuelewa kwa maelezo yako murua,serikali itabaki kuwa serika na wawakilishi watabaki kuwa wawakilishi mipaka lazima iwepo.
 
Kwenye serikali yangu,sitaki upinzani kabisa..Unadhani hii kauli inahamasisha ushirikano.
Nimetafuta kauli kama hii, ningekosa ningeipachika mwenyewe....kule Znbar alisema hataki upinzani kwenye serikali yake sasa leo hawa UVCCM wa Lumumba wanakuja kumwombea msaada kwa upinzani baada ya mambo kumshinda.
 
Ameteuliwa na bosi yupi? BOSI aliyemteua kapewa ridhaa na wananchi nchi nzima kwa kura za kishindo ateue watu wa kufanya naye kazi.Kura za kishindo za WANANCHI NA katiba vimempa hayo mamlaka ya kuteua.Huyo aliyeteua huwezi kumlingani na vikura vya mtaani alivyopata diwani au mbunge.Aliyemteua ujue ndiye aliyembwaga chini mgombea wenu LOWASA au hilo kichwani limewatoka ghafla.Msilisahau hilo

Huyo aliyeteuliwa kateuliwa kwa mujibu wa katiba ya nchi na sheria.Ndizo zimemuweka madarakani.Kumdharau ni kudharau katiba na sheria iliyomuweka.Hao ni sawa na majaji huwezi dharau jaji kuwa eti kateuliwa asijitutumue kuliko wewe uliyepigiwa kura!
Kwahiyo kwa vile ameteuliwa na aliechaguliwa na wananchi yupo sahihi kufanya kila anachojisikia na kuukwamisha upinzani kisa kapewa fadhila na boss wake? Huoni kuwa anakuwa anawadharau wananchi waliowachagua viongozi wao kwa kula za kishindo kwa kukwamisha mambo ya maendeleo kwa chuki zake binafsi?
 
Ninakubaliana na wewe kabisa. Ukikutana na kiongozi wa namna hiyo ujue ni mwendo kasi kwa sababu kama nyumbani kwako tu ni vyema kupata ushauri kwa mkeo na wanao, je! kata, tarafa, wilaya, mkoa na hata taifa? Hakuna mwanadamu anayejua kila kitu. Hata wale ma professor utakuta wame specialise kwenye kitengo kimoja. Km prof sarungi yeye ni mtaalamu wa mifupa, wako wa uchumi, mipango nk nk.Haipendezi kuwa na watu wa namna hiyo ktk uongozi wa dunia hii
 
Na mtambo wa kuchakata taka kuwa mbolea nao unahitaji hisani ya serikali kuajiri manesi wa kusomba taka mitaani!
Yaani cku hizi kila kitu mwausingizia upinzani kukwamisha mambo!
 
Nimetafuta kauli kama hii, ningekosa ningeipachika mwenyewe....kule Znbar alisema hataki upinzani kwenye serikali yake sasa leo hawa UVCCM wa Lumumba wanakuja kumwombea msaada kwa upinzani baada ya mambo kumshinda.
Hawa UVCCM huwa ni wepesi sana wa kusahau,mambo yamewaendea vibaya hawana pakushika ila wameanza kuona umhimu wa Wawapinzani.
 
Hawa UVCCM huwa ni wepesi sana wa kusahau,mambo yamewaendea vibaya hawana pakushika ila wameanza kuona umhimu wa Wawapinzani.
Walivyoimba waacheni waisome namba walifikiri number ataisoma Lowassa? namba tunaisoma wote bila kujali itikadi za chama.
 
Back
Top Bottom