Upepo wa Membe mtaani usipime

Chonde chonde watanzania,2020 twende na Membe,kwa maslahi yetu na vizazi vijavyo...
Sisi wengine hatumjui vizuri Membe. Hebu nisaidie kujua Utofauti wa Membe na Magu kulingana na Impact zao. Magu anamapungufu gani na Membe anasifa zipi kumzidi mwenzake angalau nasisi tusiofuatilia siasa kwa undani tuelewe kwann Membe na si Magufuli wakati wote ni CCM
 
Naona unajitahidi kuwa mfalme njozi! Kwa kazi nzuri anayoifanya JPM ya kurudisha nidhamu kwa Chama na Serikali ,hatotokea mtu wa kumpinga huyo Membe wenu sio tu hawezi kuchukua form bali hata kwenye geti la White House pale Dodoma hawezi kuvuka! JPM 2020!
 
Nyie watoto wa membe acheni uzushi
 
halafu taarifa zisizo rasmi zinasema Dr slaa anachukua fomu upande wa cdm,sasa patakuwa moto kweli kweli,
Haiwezekani kama.hujua mambo ya nchi kaa kimya, Dr Slaa ameshazimwa kwa kukubali unalozi, kwanza umri ineshaenda purukushani za kupambana na polis hana tena. Pili ukiwa balozi lazima umesaini mkataba wa mizimu( usiniulize) na kamwe huwezi kuwa mpinzani tena muulize Balozi Juma Mwapachu kule zanzibar.
 
Uchaguzi uwe huru Membe akichukua fomu ndn ya chama apewe maana raia ndy tunamchagua tutakae mtaka na ndiye tunamtaka Membe tuongozwe na katiba ya nchi si chama,Membe juuuuuuuuuuuu 2020/2025
Membemania ndiyo tatizo lako kuu!

Ni ugonjwa hauna chanjo ktk dhahanati Zetu nchini!
 
Nyie ndo mnamjua magufuli,lakin kwa hali iliyopo mtaani Magufuli 10% hapati
 
Time will tell! Kumbuka kuwa ushindi ni kuanzia 50.1%
 
Nani wa kushindana nae wataje, membe, January, wote aliwashinda 2015 kwenye kura huru za ccm, wataweza kumshinda 2020? hebu tueni mature kidogo tuache kujipa matumaini hewa. Ninacho jua mimi utendaji wa Magufuli huwezi kuulinganisha na makada wote ccm , wengi wao ni midomo tu utendaji ni zero, hao wenyewe video zao zimetolewa hewani kwani wamechukua hatua gani ? kama ni fighter's wangekuwa wako upinzani au waanzishe chama washindane na magufuli ili wamshinde ? kwani wana wafuasi wengi nbona kuogopa? hapo ndo huwa najua matanzania kwa kuongea tuko wazima sana action ndio shida, heri ya Magufuli walau anafanya kwa vitendo sio hizi ngonjela.
 
Watoto wa mjini walizoea kitonga (mteremko), nchi imerudi kwa wamiliki wenyewe.
 
Shibuda kalikuwa kakifaranga. Huyu si amepewa cheo cha jasusi mbobezi? Ngoja tuone!
Alishindwa kuongoza kwenye tano bora 2015 ,alisafishiwa njia na the big boy ila wapi. 2020 ndo ataweza ?
 
Alishindwa kuongoza kwenye tano bora 2015 ,alisafishiwa njia na the big boy ila wapi. 2020 ndo ataweza ?
Tatizo big boy walimchukia huko CCM sasa na dogo naye akajionyesha wazi wazi kuwa maadui wa big boy ni wake na ole wao aingie majuu. Ila kwa sasa maadui wameshikana baada ya Jiwe kuharibu haribu. Labda ana nguvu maana siyo kwa kujiamini huko Unajua alivyojitokeza na kukiri kuwa ile sauti ni yake huku akiongea kwa kibri cha kujiamini inaonekana kuna nguvu nyuma yake. Dah hata ingekuwa ni big boy amedukuliwa sidhani kama angejitokeza kwa kujiamini hivyo. Jamaa anajiamini hadi namuogopa na ukizingatia yupo nje ya system kabisa!
 
mmm! asante kwa taarifa. tatizo hapa ni kutumika kwa wanaharakati huru na hili kundi la watu wasiojulikana ''Giving a shield to the so called unknown criminals a.k.a watu wasiojulikana''
 
Hizi ndio zinaitwa mada za kumkimbiza Sungura
 
Wapinzani wanapenda sana kuyumbishwa, utafikiri migomba.

Mpaka pale watakapoacha kuimba nyimbo za CCM angalau kutakuwa na matumaini ya kushinda.

Ama kweli CCM ni baba lao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…