Upepo wa Membe mtaani usipime

Angalia asije akijakata mwenyewe maana anatakiwa ajibu trilion 2.4 ziko wapi
Watanzania tufike mahali tukubali kumpongeza anayeonyesha moyo angalau wa kutuvusha,
tusitegemee nchi hii iongozwe na malaika asiyekuwa na doa hata kidogo.
Binafsi naona hakuna haja ya kutoa maelezo ya hiyo trioni 2.4
mimi naweza kusema nchi hii ni kubwa kumtegemea mtu mmoja adhibiti mambo yote na pasiwepo upungufu
haiwezekani,huenda hilo pengo kama lipo limesababishwa na wasimamizi wake,maana tunashuhudia
kila mara watu wanatenguliwa na wengine kuwekwa.
 

Upinzani ni neno la kiswahili (lugha ya taifa) mbona wengi tunashindwa kuelewa linamaanisha nini?
 

Trilioni 2.4 ni nyingi kushinda ufisadi wote uliotokea kwenye serikali ya BWM plus ya JK

Unataka tusamehe hivihivi tu mjomba?
 
Trilioni 2.4 ni nyingi kushinda ufisadi wote uliotokea kwenye serikali ya BWM plus ya JK

Unataka tusamehe hivihivi tu mjomba?
kati ya hao ni nani aliwahi hacha kutekeleza,tuongelee kuwaza
kuhamishia ikulu Dodoma,kujenga SGR,kujenga fly overs n.k?
Hatutegemei mtu alowane umande wakati amekaa chumbani kwake tena kwenye kochi.
kitendo cha JPM kuthubutu,kinanifanya nimuunge mkono.
 

Hayo Maji unayokunywa miundo mbinu ilijengwa na JPM?
Hiyo Mwendokasi unayopanda kwenda town/Muhimbili ilijengwa na JPM?
Chuo cha UDOM anachosoma mtoto wa mjomba wako alijenga JPM?
Daraja la Kigamboni wanalopita wauza madafu kutoka Kibada alijenga JPM
Huo umeme unaowasha nchi nzima aliuweka JPM?
Vipi Barabara unazotumia kwenda kwenu huko Bukoba, Mwanza, Kahama, Geita, Mtwara, Simiyu, Katavi?
Babu yako akishikwa ugonjwa wa moyo akatibiwa JK Health Institute, aliijenga JPM?
Hizo shule za kata anazosoma mtoto wa dada yako alizijenga JPM?

Mpaka mwaka wa nne wa utawala wake JK alishajenga shule za Kata nchi nzima na Chuo kikuu cha UDOM plus Kilometa kibao za barabara, Huyu wa sasa mwaka wa nne ndo kwanza anazindua ujenzi wa miradi yake ambayo ni "Legacy projects"

Miradi mingi Mikubwa kama Daraja la Kigamboni, Hospitali ya Mloganzila, Termina 3, Darala lile la Kilombero unayoona anazindua leo Ilianza wakati wa utawala wa JK, Pesa alitafuta JK ila sema tu kwa sababu alikuwa lazima astaafu kwa mujibu wa sheria na katiba imeendelea kujengwa na kumalizika katika utawala wa JPM, kwa hiyo ukiona JPM anazindua basi anazindua tu jasho la mwenzie.

Tungoje miradi ya JPM kama SGR na Stiglers ikamilke naye tumpe ujiko lakini so far mpaka sasa bado anatembelea nyota ya JK kwa sana
 
Benard Membe for presidency.. 2020. WanaCCM wenzangu tusiharibu tena kipenga kikipulizwa. Chama chetu lazima tukisimamishe tena.
 
Mlionaaccess ya kumpata mzee wetu huyu mfikishieni ujumbe wetu Watanzania. Hakuna wakati tunamuhitaji Mh Benard Membe kama 2020. Yeye ndie wakututoa kwenye shimo hili tulilopo sasa.
 
Tunamtaka Lissu, weka Membe pembeni
 
Magufuli hahitaji CCM , ni CCM ndo ina muhitaji Magufuli, Magufuli hata akihamia chauma akampisha membe ccm na membe akaungana na wana cecm wote bado Magufuli atawashinda , huyu jamaa utendaji wake una mbeba sana mazuri ni mengi kuliko mabaya
Vizuri mkuu basi wekeni wagombea wawili katika kinyang'anyiro. Magu na Membe.
 
Mbona unawaza kawaida sana? Unafahamu nini kuhusu nguvu ya chama kwa raisi? Akiachana na chama ameachana na hiyo nguvu unayoiongelea mpaka atakapoipata tena kupitia chama kingine(kama ataipata). Raisi anafanya kazi lakini kumpandisha cheo kuliko chama unajidanganya. Halafu unatakiwa ufahamu pia kuna watu nchini wana nguvu na wafuasi mpaka kwenye majeshi na si maraisi. Ndo maana kuna nchi machafuko na uasi wa jeshi hutokea endapo watu wao wakiguswa.
 
Tunamtaka Lissu, weka Membe pembeni

Tangu mambo ya kutekana tekana, kuuawa kwa baadhi yetu, kuminywa uhuru wetu, etc.. yalipoanza, Watanzania tulishafanya maamuzi ya kumpa kiti cha uRais Mh Benard Membe. #tunamwagapombe
 
Tetea kwa akili basi. Sema hakuna T2.4 iliyopotea, kama haipo kwenye ndege basi ipo kwenye reli au umeme kuna sehemu tu imetumika.
Yaani pengo la pesa yote hiyo ndani ya miaka minne unatetea kuwa ni wasimamizi? Yeye akiwa wapi? Anavyoogopeka nani wa kuchota zote hizo? Unajua hiyo figure ni kubwa kuliko pesa zote zilizopigwa miaka kumi ya aliyepita? Mayb even na ya wa nyuma yake.
 
Anaweza badili katiba , chama kijitenge na serikali kabla ya uchaguzi, na akafanya kampeni kwa makada wote wa ccm kura za ndio zitashinda, nguvu aliyonayo ni kubwa kuliko kijani chenu, yuko hapo mtoeni muone effect yake.
 
Acha kabisa Mkuu hili likitokea la Bugirichato kupigwa chini furaha itakayokuwepo nchi nzima itakuwa haina mfano.

Watanzania wengi watalia machozi ya furaha na wengine walioathiriwa na huyo dhalimu kwa namna mbali mbali yatakuwa machozi ya huzuni.

Nina uhakika kabisa kuwa siku hiyo Bubu Atataka Kusema BAK
 
Mkuu mrija wa trilioni 2.4 mbona haujakatwa???...trioni 2.4 zipo wapi????
 
Wantanzania wengi hatujui thamani ya pesa, tril2.4 itoke wapi? miradi mingi ni makusanyo kidogo na wanatanguliza down payment, 2.4 ni accumulations ya projects zipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…