Updates uchaguzi serikali za mitaa - mtaani kwetu

Uchaguzi huu nadhani ulikuwa wa ovyo kimaandalizi kuliko maelezo.

Huwezi amini kwamba viongozi wa nchi hii wanaweza kuandaa uchaguzi na wasiweze kuchapisha karatasi maalumu ambazo si rahisi kugushiwa.

Karatasi zile nilizoona zinatumika hata wewe ungeweza kujitegenezea nyumbani kama una nia mbaya.

Kisha kwa nini ilikuwa mpaka mtu uandike majina badala ya kuweka vema? Watu wengi walikuwa wanafanya vitu vilivyosababisha kura nyingi kuonekana zimeharibika. Nchi hii kwa kweli ni utata mtupu.

Kisha kwa nini waliokuwa wakiandisha wapiga kura ni hao hao viongozi wa Sisi m? Mbona wengi niliona ni viongozi wa kwenye kata na ambao ni wana sisi m vilevile?

Bukoba sisi m imeshinda baadhi ya mitaa na Chadema imeshinda baadhi ya mitaa.

Kuna mtaa mmoja unaitwa Rwagati ulikuwa na mchuano mkali sana! nashangaa hata Karamagi alikuwepo kuongeza nguvu ili mgombea wake wa sisi m apite maana ndio wameshaanza kujiweka tayari kwa ajili ya 2010. Ni kwa nini aliweka kambi pale anajua mwenyewe lakini mwisho wa siku Chadema wameibuka kidedea kwa ushindi wa kishindo.

Ignorance imeonekana wazi kwani wengi hawajui kuandika wala kusoma. Ni ajabu na kweli lakini hiyo ndio hali halisi. Kama uchaguzi wa 2010 nao ukifanyika hivi sijui mambo yatakuwaje.

Kisha matumizi ya pesa kwenye uchaguzi yanatishia usalama wa nchi hii. Kama hakuna ufumbuzi wa jambo hili basi si muda mrefu tutasikia hii wanaita amani na utulivu havipo hata kama polisi wapo.

Siku zote naamini na nitabaki naamini amani haitunzwi na polisi bali watu wenyewe. Nakwambia hata kama utaweka polisi 1000 mahali ambapo watu hawajaamua kutulia na kuwa na amani, basi utawaua wote na bado chaos itakuwepo. Tunao mfano mzuri wa Pemba. Na hii inawezakuwa Tanzania nzima. Tujiepushe na matumizi ya pesa kwenye chaguzi zetu. Polisi wetu wajiepushe na siasa kwenye chaguzi zetu maana haiwezekani mtu anagawa pesa mbele yao na wanaona hawawezi kuchukua hatua. Sijui wako pale kwa maslahi ya nani.

Naishauri serikali na jeshi la polisi kutobweteka kwa hilo la amani na utulivu , labda kama wanahitaji kuwaua wananchi ili wao watawale hapo sina neno. Sijui watakuwa wanatawala miti?
 
habari zilizonifikia sasa hivi zinasema kile kitongoji maarufu cha TABATA mandela road-DAMPO[KULE kwa mafundi garage kule]..kimechukuliwa na CHADEMA.....baada ya mgombea wao HUSEEIN MBEGGA kumuangusha kwa kura nyingi mgombea wa CCM-MASANJA..

VIJANA WA CHADEMA WAMEKESHA HUKO...WANASHANGILIA...
 
Jana nilikwenda kipiga kura saa 3 asubuhi. Kituo kilikuwa hakijafunguliwa na wala hapakuwa na dalili wala taarifa yoyote. Nilisubiri hadi saa 3.30 na baada ya kuona hakuna kinachoendelea nikaondoka kwenda kwenye shughuli zangu. Wakati nikiwa kituoni, walikuja watu wengi na wakaondoka kwa kukata tamaa. Kama hivi ndivyo ndiyo ilivyokuwa sehemu nyingine, bado tuna miaka mingi kufika mwisho wa safari yetu.
 
Mambo si shwari kwa vitongoji vingi vya wilaya ya Mkuranga, Mafia na Kilwa mkoa wa pwani huko CUF wamewanyanyasa CCM si mchezo
 
Licha ya matokeo, ni vyema pia tukajulishana matukio yaliyojitokeza yasiyo ya kawaida katika siku ya j`pili wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa,

Upande wa mbagara Dar, FFU na gari lenye bendela nyekndu utafikiri tuko darfur, yalitisha watu

hali hii ilipelekea sehemu za starehe kama container bar, kingugi pub, kiburugwa inn nk kufunga mapema kuofia usarama.

upande wa matokeo, kingugi ilikuwa inaongozwa na cuf, wamechukua ccm, mtoni ilikuwa ya ccm wamechukua cuf

naomba na wengine mtujuze huko mliko
 
Naombeni wenye matokeo ya moshi vijijini - vunjo ayaweke jamvini hapa nlickia chadema walikua na vitongoji zaidi ya 30 na vijiji zaidi ya 10 kufikia leo mchana
 
Naombeni wenye matokeo ya moshi vijijini - vunjo ayaweke jamvini hapa nlickia chadema walikua na vitongoji zaidi ya 30 na vijiji zaidi ya 10 kufikia leo mchana
 
wakuu,
Kuna maeneo katika uchaguzi wa serikali za mtaa wananchi walishika masanduku ya kura ya ziada yaliyokuwa yametayarishwa yakiwa na kura ndani.

Ningependa kuuliza hivi haya huwa yanafanyika kweli hawa wakurugenzi wa wilaya ambao nadhani ndio returning officers wakiwa hawajui?

Au je wao ndio huwa wanayatoa masanduku hayo ili kufanikisha malengo yao? Maana haya masanduku huwa yako under their custody.

Naanza kukosa imani na watu hawa maana ni wapinga demokrasia wakubwa. Na siku za baadaye watatuletea matatizo hawa.
 
Back
Top Bottom