UPDATES: Kikao Cha Waziri Mkuu na Madaktari CPL (Central Pathology Laboratory)

Pinda apelekwe The Hague maana tayari kashaua watz wengi kwa kauli za ubabe na aliposahau umuhimu wa diplomasia katika kutatua migogoro.
 
wakuu naweka hii thread ili wale wote walioko kwenye eneo la tukio watupe updates za kikao cha majadiliano kati ya waziri mkuu na madaktari walio kwenye mgomo.nimepata habari hivi punde kuwa mh waziri Pinda ameshaingia hospitali ya taifa muhimbili...........more to come
  • inaelekea serikali inaratibu kila kitu,yaani meza kuu imeanadaliwa kwa ajili ya PM na wakuu wa wizara ya afya.
  • yule hasimu wa mponda dr ulimboka stephene aka 'bwana ulimboka' yupo frontline kwenye kikao hiki.
  • imepita dakika 51 baada ya muda uliopangwa kuanza kwa kikao lakini bado pinda hajaingia CPL,madaktari kwa upande wao wameijaza CPL ile mbaya.
  • kuna taarifa kwamba madaktari bingwa na wafanyakazi wa MNH wamepewa viti vya mbele.sijui ile kamati imepewa nafasi gani?
  • hatimaye mh Pinda na ujumbe wake wameingia CPL ni saa 9:54 asubuhi
updates;mapendekezo ya serikali
  • interns warudi muhimbili
  • madaktari wapewe nyumba na green cards lakini hajasema kivipi
  • call allowance kwa specialists iwe 25000
  • call allowance kwa madaktari wa kawaida 20000
updates
katibu mkuu na chief medical officer OUT!
mponda na Nkya watashughulikiwa na Rais!

Pinda umekula matapishi yako. Ulitishia jamaa wakafanya kweli, Ongereni sana madaktari, muwe na moyo huo huo wa ushirikiano wenu
 
sidhani kama kuna jipya kwani mti ukitaka kuuangusha kata mzizi (shina ) si uanze na matawi maana unaweza kupendeza ukaacha kuukata
 
Pinda bana hovyo kweli huyu mzee..........
Yani buku kumi ndo madaktari walikuwa wanagomea?\
wAKIKUBALI HAYO MANENO YA HOVYO, NITAWASHANGAA SANA!!!
 
Pinda mamlaka ya kumfukuza Nyoni kayapata wapi? kwa Jairo si alisema ni presidential appointee naye hana uwezo huo...?

Halafu eti anapumzishwa kufanya uchunguzi.. ni uchunguzi gani wanaotaka kufanya jamani? mbona tunafanyana mazuzu namna hiii?

Dah! Kweli bana...., alisema hana mamlaka! Hii nchi bana..., ntafurahi siku moja atwangwe hlo swali...,
 
Hao walioachiwa JK awawajibishe yaani waziri na naibu wake, kwa historia ya Jk ilivyo hana ujasiri wa kuwawajibisha japokuwa ndie aliyewateua. Atakwepa kama alivyokwepa kutekeleza maazimio 23 ya Bunge na kusababisha mzozo ndani ya serikali usioisha. Kama huamini maneno yangu subiri ujionee mwenyewe.
.
jk NI KAMA MTOTO MDOGO,
Akiambiwa anatakiwa kufanya jambo fulani, yeye analikimbia..........sasa hivi amekimbia matatizo, ameenda kuchekaceka Finland!!!
 
Heshima ya taaluma inarejea taratibu. Professional pushed to the periphery na politishun, only to be 'retrived' taifa likitumbukia katika crisis. Big up dr.
 
Kauli za Huyu mtoto wa mkulima huwa hazina Mashiko, Kumbuka wakati wa Jairo alisema kama angelikuwa na uwezo angechukua hatua ila akamgojea mkuu wa Kaya, matokeo yake tunayajua mpaka jamaa kastaafu kwa heshima.
Sitaona ajabu Waziri na Naibu wake wanapewa heshima ya kuwa mabalozi kwenye nchi fulani.
Hii nchi yetu sijui nani alitupa ujasiri wa Kondoo kila wakati kuwa KAFARA.
Jambo lingine utujuze Huyu mtoto wa Mkulima anahutubia kwa staili ya MBWEMBWE au amekuwa na Nidhamu ya kawaida.
Pia Katibu Mkuu na Chief Medical watashtakiwa au nao wanapewa heshima kama Jairo? Amefafanua au anataka kupigiwa makofi tu? Hapa hatufanyi siasa wakati wenzetu wamepoteza maisha, naye amejiweka kundi lipi kwa jeuri aliyoonyesha awali?

Mkuu mimi bado siridhiki,maana hata Pinda ni mtuhumiwa kwa kushindwa kumaliza mgogoro huu ambapo tayari umesababisha kupoteza maisha ya watanzania wetu wengi,yeye alishiriki kufikisha hapa huu mgogoro kwa kukurupuka kuwaamuru warudi kazini ama la watakuwa wamejifukuzisha kazi.sijui hii imekaaje!Hata hivyo mnatakiwa kuumuuliza kama haitakuwa kama ya Jairo maana mwisho wa siku amestaafu na mafao yake wakati ni mtuhumiwa na hii imekuwa ni staili ya kuwakingia kifua watuhumiwa,sasa kuwatoa Katibu mkuu na Mganga mkuu ni sawa lakini je lini na wanatokaje?maana wanatuhuma hawa?na tayari wamesababisha kupoteza maisha ya watu,wataondokaje hivi hivi?
 
Kuleta siasa kwenye utaalamu ndiko kunakodidimiza taifa hili,kilichomfanya atambe kuwa atawaleta madaktari wengine nini?
Madr wakaze hadi Bwana Mponda nae ang'oke ndipo majadiliano yafanyike,wakilegea,hataondoka kamwe na ataanza kuwashughulikia underground
 
Hivi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ni nani vile? Je anapaswa kumrithi Blandina?
 
kwani hao kina mponda na nkya hawaoniaibu tu wao wakaandika barua ya kukaa pembeni?
 
Heading inasema LIVE kikao cha Waziri Mkuu!
MBONA HAKUNA POSTS ZA LIVE?...
Jacbauer vipi mkubwa?
 
Dr.Ulimboka ww ni jembe pamoja na vijembe vyote vya mtoto wa mkulima alivyovitoa bado kakubali kukaa na ww meza moja,ss hapo atakuita tena bwana ulimboka au Dr.?mtu mzima anakula matapishi yake
 
Labda tu nikujuze kidogo.

Kumbuka kuwa duniani kooote hospital za jeshi ndio hospital kuu na mara zote zinakuwa na kila kitu na wataalamu wengi sana na wenye uwezo mkubwa na zinakuwa ni za rufaa. Hata viongozi wa nchi wakiumwa mara zote wanatibiwa katika hospital za kijeshi kutokana na usalama na weledi wa maDr wao.

Nakumbuka hata Tz , Jeshi lilisomesha sana madaktari wake enzi hizo na kuiimarisha hospital yao ya lugalo.

Pasi na shaka yoyote huko Tz lugalo ni hospital ya rufaa pia kijeshi. Hakuna mtu anayeweza kupewa uhamisho toka lugalo kwenda muhimbili kwa matibabu zaidi.

Hata mgomo wa 2003 wa madaktari hao hao wa Lugalo walishika muhimbili na kuiendesha mpaka mgogoro ulipoisha

Chunguza hilo.


Baada ya kukata viuno hapa na vidole juu ndio sasa unataka tujiulize?
 
Mimi nashauri ni lazima waTz murejee katika mila na desturi zenu na kuachana na hizo za kizungu.

Nakumbuka toka zamani kulikuwa na kuto kuelewana kunakoweza kutokea katika jamii mbali mbali mfano wakti nipo Chuo kikuu UDSM tulikuwa tuna mogogoro mara kwa mara na chuo au na Serikali. Lakin mila zenu ilikuwa wanafunzi woote mnakusanyika pale Nkuruma hall na viongozi wanakuja na kukaa kitako kuanza kujadili matatizo yenu mpaka mnafikia kukubaliana na baadae mnarudi darasani.

Siku zote viongozi walikuwa wepesi kufika na kuongea na wanafunzi na kutatua migogoro kwa njia ya majadiliano mezani na sio kuandamana.

naona sasa utamaduni huu huko Tz umepotea kabisa. Viongozi wanajiona ni miungu watu hawataki kabisa kuwasikiliza wanaowaongoza na kupenda kutumia ubabe katika kutatua migogoro.

hakika ubabe na ubinafsi ni sumu sana katika uongozi. Kiongozi kumbuka bila kuwa na unaowaongoza wewe huwezi kuwa kiongozi. Na mnaongozwa acheni lugha za kebehi na kashfa kwa viongozi wenu. Hishma ni muhimu sana na utii wa sharia zenu mlizojitungia.

Nawasihi tena waTz rudini kwenye mila na desturi zenu za kukaa kitako na kujadili matatizo yenu mezani na sio kwa kuandamana na kutusiana.

Loh naifananisha Barza ya JF sawa na Mzee Punch wa Udsm enzi hizo.

Baru, imebidi nitazame maandiko yako sehemu mbalimbali, nimegundua wewe ni mtata sana.
Umesoma UDSM bure kisha ukakimbilia huko uarabuni! Hiyo ni haki yako lakini usikurupuke kushambulia kitu usichokijua.
Kama hili la hospital tuachie wenye fani tukujuze.Usijaribu kutufunza. Tunakupa uzoefu toka kwenye fani unabisha sijui tukueleweje?
Haya sasa unataka kutushauri ati tuachane na mila za wazungu, ina maana kudai haki ni uzungu? Ukimsemesha mtu kwenye mazingira ya amani asiposikia unafanyaje? Kwa taarifa yako, kimila zetu za kiafrika, haki hudaiwa hata ikibidi kwa upinde na ndio maana babu zetu akina Mkwawa na Mirambo walipigana kiume kudai kilicho haki kwao.
 
pinda kasema lolote juu ya ulimboka au bado anakula matapish yake???
 
Back
Top Bottom