changaule
JF-Expert Member
- Jan 10, 2020
- 5,587
- 9,179
Kukiwa na tuhuma mbali mbali juu ya upangaji wa matokeo, ambapo timu ya Simba ilishapeleka mashitaka yao juu ya tabia ya upangaji wa matokeo ndani ya ligi kuu unafanywa na klabu ya Yanga kupitia kwa mshauri wa klabu bwana Senzo.
Wakati tuhuma hizo zikiwa zinqfanyiwa kazi na vyombo husika, kuna kitendo kimoja ama tabia moja inayofanywa na klabu ya Simba ambayo kimsingi naona kama wanajua kile kinachoenda kutokea uwanjani pindi waendapo mikoani.
1) mechi ya Jkt Tanzania vs Simba
Simba walitangaza kufanyika kwa party ambapo waliita pre match party. Hapa unaona kabisa kuwa Simba walikuwa na uhakika wa kupata furaha iwe isiwe. Na kweli tunaona magoli ya mapema zaidi kufungwa ambapo ndani ya dakika 20 tayari magoli yalikuwa mawili na kipindi cha kwanza Jkt wameshalala goli tatu.
2) mechi ya Prison hakukuwa na party ya After match wala Pre match party na mwisho wake Simba hakupata matokeo ya mvua ya magoli. Hii maanake walishaona kabisa kuwa hakufanikiwa kuwekeza katika rushwa hivyo hakuweza kutangaza shangwe kwa mashabiki kabla ya mpambano.
3) mechi ya Coastal union dhidi ya Simba.
Simba kabla hata ya mechi kuchezwa walishatangaza party. Maanake Simba walishajua na walikuwa wana asilimia mia ya matokeo gani wanaenda kuyapata uwanjani na kutanguliza furaha kwa mashabiki ya kupongezana kwa kuita Party.
Matokeo uwanjani ni kama ilivyokuwa kwa mechi ya Jkt Tanzania, yanapatikana magoli ya mapema zaidi hadi mapumziko magoli matano Simba anaongoza. Uchezaji wa coastal umekuwa wa kujikanyaga kanyaga kama wanajifunza mpira vile.
Kuna dalili ya rushwa na upangaji wa matokeo hata katika timu ya Simba pia.
Wakati tuhuma hizo zikiwa zinqfanyiwa kazi na vyombo husika, kuna kitendo kimoja ama tabia moja inayofanywa na klabu ya Simba ambayo kimsingi naona kama wanajua kile kinachoenda kutokea uwanjani pindi waendapo mikoani.
1) mechi ya Jkt Tanzania vs Simba
Simba walitangaza kufanyika kwa party ambapo waliita pre match party. Hapa unaona kabisa kuwa Simba walikuwa na uhakika wa kupata furaha iwe isiwe. Na kweli tunaona magoli ya mapema zaidi kufungwa ambapo ndani ya dakika 20 tayari magoli yalikuwa mawili na kipindi cha kwanza Jkt wameshalala goli tatu.
2) mechi ya Prison hakukuwa na party ya After match wala Pre match party na mwisho wake Simba hakupata matokeo ya mvua ya magoli. Hii maanake walishaona kabisa kuwa hakufanikiwa kuwekeza katika rushwa hivyo hakuweza kutangaza shangwe kwa mashabiki kabla ya mpambano.
3) mechi ya Coastal union dhidi ya Simba.
Simba kabla hata ya mechi kuchezwa walishatangaza party. Maanake Simba walishajua na walikuwa wana asilimia mia ya matokeo gani wanaenda kuyapata uwanjani na kutanguliza furaha kwa mashabiki ya kupongezana kwa kuita Party.
Matokeo uwanjani ni kama ilivyokuwa kwa mechi ya Jkt Tanzania, yanapatikana magoli ya mapema zaidi hadi mapumziko magoli matano Simba anaongoza. Uchezaji wa coastal umekuwa wa kujikanyaga kanyaga kama wanajifunza mpira vile.
Kuna dalili ya rushwa na upangaji wa matokeo hata katika timu ya Simba pia.