Uongo, Unafiki na Uzandiki wa CCM!

Uongo, Unafiki na Uzandiki wa CCM!

Inasikitisha kuona kwamba CCM wamekuwa mstari wa mbele kuwadanganya wananchi kwamba uendeshaji wa serikali 3 ni ghali kuliko serikali 2 huku wakiwa hawatoi takwimu za kuonesha ughali huo unakujaje. Swali la kujiuliza ni kwamba ikiwa serikali 3 ni ghali na kama kweli CCM wana nia njema ya kupunguza matumizi ya serikali ni kwa nini basi tusiende kwenye serikali 1? Hapo ndipo unapogundua kwamba Dr Antipas Lissu alipowaambia CCM kwamba wamezoea kuishi kwa uongo hakuwa amekosea hata kidogo. Ndivyo CCM walivyozoea kuishi.

Hii hesbau ni rahisi sana. Leo nilikuwa namuuliza mtoto wangu anayesoma chekechea kama 1 na 2 ni ipi kubwa, akaniambia kwamba ni 2! Sasa swali rahisi kama hili kwanini CCM wanashindwa kulitatua wakati mtoto wa chekechea anaweza? Ndani ya CCM kuna maprofesa lukuki lakini wote wameacha taaluma zao na kuchagua kutumikia uongo. Ndugu zangu, wote ni mashahidi na mnafahamu kwamba 1 ni ndogo kuliko 2 ila CCM wameng'ang'ania serikali 2 ambazo ni ghali kuliko serikali 1 kwa sababu zina manufaa kwao kisiasa. Ndio maana wanajenga hoja mufilisi kwamba serikali 3 ni ghali kuliko 2 huku wakisahau kwamba 1 ni nafuu zaidi kuliko 2! Pia serikali 1 zitaimarisha muungano na umoja zaidi kuliko hizi serikali 2 za kulazimishana. Hili hawalioni ila wamebaki kukomaa na serikali 3!

Halafu, ni lini CCM walikuwa na huruma kwa wananchi? Sote tunajua na tunafahamu jinsi pesa za umma zinavyofisidiwa watu wa CCM na kutumiwa na serikali kununua na kuendesha magari ya kifahari huku wananchi wakila majani pamoja na kukosa huduma za kijamii kama matibabu, maji, elimu, miundombinu, nk. Hiyo huruma ya CCM imetoka wapi ghafla hadi wafikirie kupunguza idadi ya serikali kwa manufaa ya wananchi? Hiki ni kichekesho cha mwaka.

Uongo mwingine wa CCM ni dhana potofu kwamba serikali 3 zitavunja muungano. Hii ni hoja ya kitoto na kizezeta kabisa. Kinachosikitisha na kushangaza zaidi ni pale CCM wanapolazimisha na kuwatia hofu wananchi kwa kuwaaminisha kwamba uwepo wa serikali 3 (serikali ya Tanganyika, Zanzibar na MUUNGANO wa Shirikisho) eti ni kuvunja muungano. Muungano utavunjikaje wakati katika hizo serikali 3 imo serikali ya Muungano (Shirikisho)? Hivi hawa INTARAHAMWE hawana haya? Mtaji wa hawa watu ni ujinga watanzania walio wengi. Kuna wajinga wachache ambao wanakubali uongo huu lakini wengi wetu tunaupuuzilia mbali.

Hivi jamani mtu ukiwa na nyumba yako ambayo haikidhi mahitaji, ukiamua kuifanyia renovation au ukaibomoa na kujenga nyumba mpya iliyo kubwa, imara na bora zaidi, tatizo liko wapi? Ni nini hofu ya CCM katika uwepo wa serikali 3 hadi waanze kuwatisha raia kwamba ikiwa serikali 3 zitaruhusiwa jeshi litachukua nchi? Kama ndivyo basi, sisi raia tunaoteseka chini ya utawala wa CCM tunalikaribisha jeshi kwa mikono miwili lije litawale badala ya kuendelea kuishi ndani ya utumwa wa serikali ya CCM.

CCM hawahawa waliwaaminisha watu kwamba vyama vingi vya siasa vikiruhusiwa, nchi itaingia vitani kama ilivyowahi kutokea huko Rwanda. Walifikia hatua ya kutembea nchi nzima wakionyesha video za vita ya Rwanda na intarahamwe ili kuwatisha wananchi kuhusu ujio wa vyama vingi. Ni zaidi ya miaka 20 sasa tangu vyama vingi viruhusiwe nchini lakini hatujawahi kuona nchi ikiingia vitani. Ama kweli CCM wamezoea kuishi kwa UONGO, ukweli hawauwezi! Propaganda zao hizi tumezizoea, hawakuanza leo wala jana.

:yield:

[h=2]Askofu Kakobe kuzungumzia muundo wa Muungano katika Neno la Pasaka 20.4.14[/h]
Taarifa zilizopatikana kutoka kwa waumini wanaosali katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), linaloongozwa na Askofu Mkuu Zachary Kakobe, zinaeleza kwamba, Jumapili iliyopita katika Ibada Kuu ya Kanisa hilo, lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge, Dar-Es-Salaam, karibu na Mlimani City; Mzee wa Kanisa anayehusika na matangazo, alitangaza kwamba, katika Ibada Kuu ya Sikukuu ya Pasaka, Jumapili hii tarehe 20.4.2014, Askofu Kakobe atahubiri Neno la Mungu, ambalo pamoja na mambo mengine ya rohoni, litazungumzia pia juu ya mustakabali wa nchi yetu, hususan kuhusu Bunge Maalum la Katiba, linaloendelea na vikao vyake, mjini Dodoma. Hata hivyo, taarifa za uhakika zilizopatikana jana, kutoka kwa baadhi ya Viongozi wa Kanisa hilo, zinafafanua kwamba, Askofu Kakobe, atachukua muda mrefu zaidi katika mahubiri yake, kuzungumzia juu ya muundo wa Muungano unaoifaa nchi yetu.

Ibada Kuu ya Pasaka katika Kanisa hilo, itaanza saa 3 kamili asubuhi, na kumalizika saa 6.30 mchana. Hata hivyo, kwa kuzingatia Kanuni za Maadili ya Mavazi, za Kanisa hilo; Viongozi hao wa Kanisa, wamewakumbusha watu wote watakaohudhuria, kumheshimu Mungu kwa mavazi watakayoyavaa. Watakaovaa vimini, jeans, milegezo, na nywele bandia; hawataruhusiwa kuingia katika Nyumba hiyo ya Mungu. Vilevile, wanawake hawapaswi kuvaa suruali, na wanatakiwa kufunika vichwa vyao. Vivyo hivyo, wanaume hawakubaliki kuingia Kanisani humo, wakiwa wamevaa kofia.​
 
Mara zote mdomo hauna ushirikiano na maeneo mengine ya mwili. Shauri yako ukipata nafasi tena utakuja omba msamaha hapa.
kamwage hicho kifusi kama kimekuelemea naona unaleta longo longo!
 
Inasikitisha kuona kwamba CCM wamekuwa mstari wa mbele kuwadanganya wananchi kwamba uendeshaji wa serikali 3 ni ghali kuliko serikali 2 huku wakiwa hawatoi takwimu za kuonesha ughali huo unakujaje. Swali la kujiuliza ni kwamba ikiwa serikali 3 ni ghali na kama kweli CCM wana nia njema ya kupunguza matumizi ya serikali ni kwa nini basi tusiende kwenye serikali 1? Hapo ndipo unapogundua kwamba Dr Antipas Lissu alipowaambia CCM kwamba wamezoea kuishi kwa uongo hakuwa amekosea hata kidogo. Ndivyo CCM walivyozoea kuishi.

Hii hesbau ni rahisi sana. Leo nilikuwa namuuliza mtoto wangu anayesoma chekechea kama 1 na 2 ni ipi kubwa, akaniambia kwamba ni 2! Sasa swali rahisi kama hili kwanini CCM wanashindwa kulitatua wakati mtoto wa chekechea anaweza? Ndani ya CCM kuna maprofesa lukuki lakini wote wameacha taaluma zao na kuchagua kutumikia uongo. Ndugu zangu, wote ni mashahidi na mnafahamu kwamba 1 ni ndogo kuliko 2 ila CCM wameng'ang'ania serikali 2 ambazo ni ghali kuliko serikali 1 kwa sababu zina manufaa kwao kisiasa. Ndio maana wanajenga hoja mufilisi kwamba serikali 3 ni ghali kuliko 2 huku wakisahau kwamba 1 ni nafuu zaidi kuliko 2! Pia serikali 1 zitaimarisha muungano na umoja zaidi kuliko hizi serikali 2 za kulazimishana. Hili hawalioni ila wamebaki kukomaa na serikali 3!

Halafu, ni lini CCM walikuwa na huruma kwa wananchi? Sote tunajua na tunafahamu jinsi pesa za umma zinavyofisidiwa watu wa CCM na kutumiwa na serikali kununua na kuendesha magari ya kifahari huku wananchi wakila majani pamoja na kukosa huduma za kijamii kama matibabu, maji, elimu, miundombinu, nk. Hiyo huruma ya CCM imetoka wapi ghafla hadi wafikirie kupunguza idadi ya serikali kwa manufaa ya wananchi? Hiki ni kichekesho cha mwaka.

Uongo mwingine wa CCM ni dhana potofu kwamba serikali 3 zitavunja muungano. Hii ni hoja ya kitoto na kizezeta kabisa. Kinachosikitisha na kushangaza zaidi ni pale CCM wanapolazimisha na kuwatia hofu wananchi kwa kuwaaminisha kwamba uwepo wa serikali 3 (serikali ya Tanganyika, Zanzibar na MUUNGANO wa Shirikisho) eti ni kuvunja muungano. Muungano utavunjikaje wakati katika hizo serikali 3 imo serikali ya Muungano (Shirikisho)? Hivi hawa INTARAHAMWE hawana haya? Mtaji wa hawa watu ni ujinga watanzania walio wengi. Kuna wajinga wachache ambao wanakubali uongo huu lakini wengi wetu tunaupuuzilia mbali.

Hivi jamani mtu ukiwa na nyumba yako ambayo haikidhi mahitaji, ukiamua kuifanyia renovation au ukaibomoa na kujenga nyumba mpya iliyo kubwa, imara na bora zaidi, tatizo liko wapi? Ni nini hofu ya CCM katika uwepo wa serikali 3 hadi waanze kuwatisha raia kwamba ikiwa serikali 3 zitaruhusiwa jeshi litachukua nchi? Kama ndivyo basi, sisi raia tunaoteseka chini ya utawala wa CCM tunalikaribisha jeshi kwa mikono miwili lije litawale badala ya kuendelea kuishi ndani ya utumwa wa serikali ya CCM.

CCM hawahawa waliwaaminisha watu kwamba vyama vingi vya siasa vikiruhusiwa, nchi itaingia vitani kama ilivyowahi kutokea huko Rwanda. Walifikia hatua ya kutembea nchi nzima wakionyesha video za vita ya Rwanda na intarahamwe ili kuwatisha wananchi kuhusu ujio wa vyama vingi. Ni zaidi ya miaka 20 sasa tangu vyama vingi viruhusiwe nchini lakini hatujawahi kuona nchi ikiingia vitani. Ama kweli CCM wamezoea kuishi kwa UONGO, ukweli hawauwezi! Propaganda zao hizi tumezizoea, hawakuanza leo wala jana.

:yield:

hiyo picha ya prof issa shivji --------- ndiyo imenifurahisha!
 
Hakuna wanasiasa wanafiki Tanzania kama wale wanaotokana na CHADEMA, kila mara wamekuwa wakihubiri kile ambacho hawawezi kukitenda!
 
Kwa cc wazee wa bajet serikali 1 ndo itatupunguzia gharama na kwa kuwa CCM leo hii wamegundua ni gharama tunawaomba hivyo bac wapunguze gharama ktk uendeshaji wa miimili yote wabunge wapunguziwe gharama ya mishahara mpaka kufikia laki 300000 km ilivyo kwa walimu na magari ya kifahar wanayotumia wakubal kuyapiga mnada pindi wanapomaliza mchakato huu ili 2jue km kwel wameokoka na wako tayar kuwatumikia watz.
 
...ccm hawafanyi siasa,siku zote wamedumu na kufaidika na ulaghai wa kutumia ujinga wa wananchi. siku zao zinahesabika na mwisho wao upo karibu sana....
 
Mtaji wa ccm si ujinga wa wananchi kwani sasa wengi wameelimika bali mtaji wa ccm ni tume ya uchaguzi (isiyotaka kuboresha daftari)wanasheria(mahakama inayo tafsiri sheria itakavyo) na policcm na usalama wa mafisadi a.k.a. Usalama wa taifa (wanaoshindwa kushugulikia mafisadi )
Mtaji mkubwa ccm ni ujinga wa Wananchi.
 
Ndugu Asamwa, tunahitaji viongozi kama akina Jerry Rawlings wa Ghana.

Mkuu PauliMasao ni nini hasa unapenda kuhusu Jerry Rawlings?! Ni jinsi alivyoingia madarakani kwa kupindua serikali iliyokuwepo ama ni style yake ya uongozi?
 
Hakuna wanasiasa wanafiki Tanzania kama wale wanaotokana na CHADEMA, kila mara wamekuwa wakihubiri kile ambacho hawawezi kukitenda!

Jenga hoja, acha matusi-hayasaidii kitu. Je, ikiwa CCM mnatazama ughali wa serikali kwa kuangalia idadi ya serikali-kwamba serikali 3 ni ghali kuliko 2, je, hamuoni kwamba serikali 1 ni nafuu kuliko serikali 2? Kama ndivyo, kwanini sasa msiende kwenye serikali 1 badala ya serikali 2 (ambazo ni mzigo kwa mwananchi ukilinganisha na serikali 1)? Hapa ndipo unafiki wa CCM unapoonekana wazi. Kama sio wanafiki tuambieni jinsi serikali 2 zilivyo rahisi kuendesha (kigharama) kuliko serikali 1. Sio mnakaa kubwabwaja tu kama bata anayehara bila kutetea hoja iliyopo mezani kwa pointi zinazoeleweka.
 
Mimi nadhani angehubiri mfumo wa uendeshaji wa kanisa lake
 
Mimi nadhani angehubiri mfumo wa uendeshaji wa kanisa lake

alitakiwa aanze samuel 6 kwanza---angewaacha kadinali pengo na mufti simba wahubiri mifumo ya uendeshaji wa dini zao badala ya kwenda kuwarubuni akitaka waiunge mkono ccm ktk hoja ya serikali 3. na pia lukuvi angeacha kutumia mimbari ya kanisa kuwatukana waislamu.
 
Back
Top Bottom