Tetesi: Uonevu wa wakulima wa cocoa halmashauri ya Mlimba

Tetesi: Uonevu wa wakulima wa cocoa halmashauri ya Mlimba

Pax Vobiscum

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
455
Reaction score
764
Salaam wakuu,
Uongozi wa Halmashauri ya Mlimba umetangaza kuanza kuwaandikisha na kuwasajili wakulima wa zao la kokoa,
Hii inafikirisha sanaaa, je Nia yao Nini hasa?

Kwanini waje na huo Mpango kwa wakulima wa kokoa tu? Kwanini wasifanye kwa wakulima wote wa mpunga, mawese, mahindi, matikiti n.k?

Kwanini wakulima wa kokoa wanasumbuliwa sumbuliwa?

Mtu ahangaike kulima akianza kuvuna wao wanakuja na mikakati kibao, kujifanya kumsaidia mkulima.

Kwa ufupi inaonekana Kuna shida sehem, Kuna mipango ovu na isiyo na Nia njema kwa wakulima wa kokoa.

Tunaomba huo Mpango wao waachane nao, watu hawataki mambo ya kusumbuana ktk kilimo na mazao yao.

Kama wanataka kusajili basi wasajili wakulima woteeeeeee, siyo kujichagulia zao Fulani hivi, zao hili vile.
 

Attachments

  • IMG_20250929_214952_353.jpg
    IMG_20250929_214952_353.jpg
    365.1 KB · Views: 15
Inatakiwa muaulize ofisi ya kijiji madhumuni ya mkakati huo ni nini
 
Back
Top Bottom