Unyanyasaji walimu geita mpaka lini?

ntamaholo

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
12,904
6,904
Wilaya ya GEITA pamoja na kuwa na rasilimali za madini katika ardhi yao, bado maisha na unyanyasaji kwa wananchi na watumishi wa umma uko juu sana kuliko wilaya nyingine za mkoa wa Mwanza.

Kilichonisukuma leo kuwapa taarifa na kutaka maoni yenu ni juu ya Halimashauri ya wilaya ya Geita kuwa na kiburi na kufanya unyanyasaji wa wazi kwa watumishi wake hasa WALIMU.

Kwa walimu walioanza kazi 2010 October, hawakulipwa pesa yao ya kujikimu kwa mda mrefu mpaka walipotaarifiana na kukusanyika HALIMASHAURI na kufanya fujo, uongozi mwovu uliopo ukawaita POLISI na kuwasambaratisha walimu hao waliokuwa wakidai haki zao ambazo walinyimwa na mazingira ya kuwadhulumu yalikuwa wazi.

Aliyezima dhuluma hiyo ni waziri mkuu alipotangaza kwamba wilaya zote zilisha pewa pesa ya waajiriwa wapya kujikimu na kuwataka wakurugenzi kuwalipa watumishi stahili zao mara moja ambapo WALIMU geita walilipwa pesa zao April 2011 badala ya October/November 2010. Hata hivyo hawakulipwa zote, walidhulumiwa pesa hiyo hadi 120,000/= .

Sasa watumishi wa halimashauri hiyo, wameingizwa na kulazimishwa kuhesabu sensa ya watoto tangu tarehe 26-09-2011 mpaka leo wanahesabu sensa hiyo.
Kinachosikitisha, hawalipwi chochote na halimashauri hiyo, waratibu wa elimu wa kata ndio wanaopiga mkwara walimu wao na kuwahimiza kukamilisha zoezi hilo kabla ya kufika kesho ijumaa ya 30.09.2011.

Utata,
1. kwa nini sensa iendeshwe bila bajeti?
2. Kazi ya walimu wawapo kwenye vituo vyao vya kazi ni kuhesabu wa watu wa vijiji wanakofanyia kazi?
3. Je hii sensa ni ya Tanzania nzima au ni maalumu kwa halimashauri ya GEITA na hasa kata ya CHIGUNGA ambapo walimu wa kata hizo wamelazimishwa kuacha kazi yao ya kufundisha na kuwa maafisa wahesabu watu-NGOSWE katika vijiji vyao?
4. Ni haki kwa mfanyakazi kufanya kazi ambayo haimuhusu tena bila kumlipa chochote?

Mwenye majibu ya hili atujuze,
nawasilisha.
 
Mnalalamika nn?ukifika uchaguzi mnawasaidia kuiba kura,nani atawatetea wakati 80% ya madiwani ni magamba wapo kimatumbo yao,tulia mnyolewe ili 2015 mfanye uamuzi sahihi
 
Haki yako idai mwenyewe, Je unataka nani akusaidie kuidai? Tuachane na hii tabia inayendana na kamsemo ka-kisukuma kwamba nyumba ya mtu muoga anayeogopa kutetea haki yake nayo ni nyumba pia [Kaya ya ngwolo nayo kaya]
 
mnalalamika nn?ukifika uchaguzi mnawasaidia kuiba kura,nani atawatetea wakati 80% ya madiwani ni magamba wapo kimatumbo yao,tulia mnyolewe ili 2015 mfanye uamuzi sahihi

walimu wanaweza kusimamia vizuri, lakini linapokuja suala la kutangaza matokeo, polisi wanasimamia kumtangaza ambaye hajashinda. Nani wa kumlaumu?
Walimu ndo wapiga kura?
Mbona wengi wanaichukia ccm?
 
Ninahuzunishwa sana na jinsi ambavyo waalimu wa Tz wasivyojitambua. Waalimu wamesambaa nchi nzima na wamesambaa katika jamii kubwa isiyo na uelewa mkubwa wa yanayoendelea nchini. Waalimu wangekuwa aggressive vya kutosha wana uwezo wa kuamua nani atawale nchi hii. Viongozi wetu wanajua hilo, ndo maana hawawapi mwanya wa kuji-mobilise kiasi hicho. Wamewekewa waalimu wenzao Wilayani kwa ajili ya kuwakandamiza, kwani mnyanyasaji wa mwalimu ni mwalimu mwenzake. Wameanzisha CWT na kuwaweka mamluki wao kuakikisha waalimu hawafurukuti, moja ya mbinu ni kuhakikisha viongozi wao hawawi waalimu wenye taaluma ya juu, wakienda kupiga kura kwenye chama chao wanamchagua mwalimu wa primary kwa kuwa wao ndo wenye uwakilishi mkubwa. Ushauri wangu ni huu ni lazima kila mwalimu mmoja mmoja kujitambua binafsi na kuanza kupinga uonevu na unyanyasaji anaofanyiwa. Wewe uliyeleta hoja hii umechukua initiative gani binafsi kujikwamua na unyanyasaji huo?Pili, CWT inapaswa kufanyiwa revolution ili kuwa ni mikakati mipana na kutetea sio waalimu tu bali wananchi kwa ujumla, kama tutakumbuka vizuri vyama vya wafanyakazi vilikuwa mstari wa mbele kupigania uhuru ktk nchi nyingi za Kiafrika, kwa nini sio CWT? Waondokane na tofauti walizonazo kulingana na elimu au ngazi ya elimu wanyofanyia kazi, kwani zipo tofauti kati ya waalimu wa Primary, sec, vyuo na wale wanaofanya kazi za uongozi.Tatu, CWT wanapaswa kuwaelimisha waalimu kujielewa, wajenge umoja katikati ya wanachama wote, wawe tayari kuwatetea wanachama wao kwa hali na mali. Haya malalamiko unayoleta hapa CWT wanayajua? Wamechukua hatua gani? Kumbuka waalimu karibu wote ni wanachama wa CWT na wanachangia chama hiki kwa fedha nyingi kila mwezi.TAFAKARI NA CHUKUA HATUA sio kulalamika.
 
Katika watu ambao wanafanyakazi kubwa hapo tzdiii ni walimu bt katika watu wanaorudisha nyuma mageuzi na kuzolotesha mabadiriko ni walimu abt 65%
Angalia wananyanyaswa wanataka watu wengine ndo wawatatulie ilo jambo..mh na awa ni certificate,diploma and degree holder Paul Fraire -Education for emancipation!
 
Ninahuzunishwa sana na jinsi ambavyo waalimu wa Tz wasivyojitambua. Waalimu wamesambaa nchi nzima na wamesambaa katika jamii kubwa isiyo na uelewa mkubwa wa yanayoendelea nchini. Waalimu wangekuwa aggressive vya kutosha wana uwezo wa kuamua nani atawale nchi hii. Viongozi wetu wanajua hilo, ndo maana hawawapi mwanya wa kuji-mobilise kiasi hicho. Wamewekewa waalimu wenzao Wilayani kwa ajili ya kuwakandamiza, kwani mnyanyasaji wa mwalimu ni mwalimu mwenzake. Wameanzisha CWT na kuwaweka mamluki wao kuakikisha waalimu hawafurukuti, moja ya mbinu ni kuhakikisha viongozi wao hawawi waalimu wenye taaluma ya juu, wakienda kupiga kura kwenye chama chao wanamchagua mwalimu wa primary kwa kuwa wao ndo wenye uwakilishi mkubwa. Ushauri wangu ni huu ni lazima kila mwalimu mmoja mmoja kujitambua binafsi na kuanza kupinga uonevu na unyanyasaji anaofanyiwa. Wewe uliyeleta hoja hii umechukua initiative gani binafsi kujikwamua na unyanyasaji huo?Pili, CWT inapaswa kufanyiwa revolution ili kuwa ni mikakati mipana na kutetea sio waalimu tu bali wananchi kwa ujumla, kama tutakumbuka vizuri vyama vya wafanyakazi vilikuwa mstari wa mbele kupigania uhuru ktk nchi nyingi za Kiafrika, kwa nini sio CWT? Waondokane na tofauti walizonazo kulingana na elimu au ngazi ya elimu wanyofanyia kazi, kwani zipo tofauti kati ya waalimu wa Primary, sec, vyuo na wale wanaofanya kazi za uongozi.Tatu, CWT wanapaswa kuwaelimisha waalimu kujielewa, wajenge umoja katikati ya wanachama wote, wawe tayari kuwatetea wanachama wao kwa hali na mali. Haya malalamiko unayoleta hapa CWT wanayajua? Wamechukua hatua gani? Kumbuka waalimu karibu wote ni wanachama wa CWT na wanachangia chama hiki kwa fedha nyingi kila mwezi.TAFAKARI NA CHUKUA HATUA sio kulalamika.

Umesema ukweli mtupu. walimu ni ndugu zetu tena ambao wakiamua wana nguvu kubwa sana kuleta mabadiliko nchini. kinachonisikitisha ni kwamba
1. walimu waliowengi yaani wa shule za msingi, ndo hao walionyimwa elimu nzuri na hivyo kwao ualilimu ndo option ya mwisho. katika mazingira haya, hawawezi kusimama kupinga unyonyaji.
2. Walimu kutokupenda kujiendeleza nacho ni kikwazo kikubwa. Hat kujisomea hawataki. Nina rafiki yangu mwl. alikuja kunitembela geto kwangu, wakati anaandaa chakula akataka kuipua sufuria jikoni, hakutaka kutafta mbanio, yeye aliingia kwenye libraary yangu ya magazeti akachana gazeti la mwanahalisi aipulie sufuria jikoni. Alinikera lakini nilimsamehe baada ya kumwelewesha na yeye kukiri amenikosea.
3. Walimu wengi wanatoka katika famila maskini na hivyo kwa yeye kuwa mwalimu, kwa familia yao ndo tajiri. Harakati zozote za kudai haki usimhusishe kwani anaamini atafukuzwa kazi na hivyo kupoteza tittle aliyonayo na kusababisha dhiki zaidi katika familia yao.

WANAHITAJI KUHAMASISHWA ILI TUWE SOTE KATIKA KUDAI DEMOCRASIA ITAKAYOENDANA NA SERIKALI KUWA CHINI YA MAAMUZI YA WAKULIMA NA WAFANYAKAZI
 
Kwa shemu flani ni kweli msemayo,,lakini kumbukeni kwamba walimu wa enzi ya mwito,enzi za mwalimu ndo wanaisha hivyo!Sasa wanakuja walimu wa kizazi kipya,hawa tegemeeni ndio watakaokuwa vinara wa mabadiliko huko tuendako.Ni suala la kusubiri tu!mda utafika mtakubaliana na haya..
 
NTAMAHOLO kindly ni PM tupeane ushauri. hata mi naona kitu should be done
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom