Unyama wa polisi Dodoma

Umkondo wa Swize

JF-Expert Member
Dec 29, 2012
282
89



[h=3]MTU MMOJA APIGWA NA KUUMIZWA VIBAYA NA POLISI[/h]
Kushoto ni kijana ambaye jina halikutambuliwa mara moja akipigwa na polisi.

Kijana ambaye hana shati akichapwa na polisi aliye mbele yake.

Nyuma ya pikipiki ni jana anayeendelea kupigwa na polisi baada ya kuteguliwa mguu na kupasuliwa usoni huku mkono wake ukiwa umechubuka.
=========================================================================
Na Gustav Chahe, Dodoma


Ni nje kidogo na stendi ya daladala ziendazo Chuo cha Pipango na Nanenane, Polisi walipomkamata kijana mmoja ambaye jina lake halikutambuliwa mara moja mbele yangu na kuanza kumpiga.


Wakati wanaendelea kumpa kichapo, wananchi walitaka kujua kosa la huyo kijana ni nini ndipo alipojitokeza askari mmoja na kusema ni mlevi.


Wakati hayo yakiendelea nikashuhudia kwa macho yangu askati aliyekua amevaa mavazi ya kiraia akiwa na boriti na kuanza kumpiga kijana huyo miguuni, mgongoni hata mikononi na kumpasua usoni na kumtegua mguu.


Hali hiyo ilinisukuma kuchomoa kamera katika mkoba wangu na kuanza kupoga picha kwa kiicho japo watu walikuwa wengi iawa ni shida kupata picha lakini nilijitahidi kupata picha Fulani.


Nikaona haitoshi nikaamua kumsogelea askari mmoja na kunza kumuuliza ni kosa gain kijana amelikosa kiasi cha kuchapwa kama mnyama.


Wakati nikiuliza hivyo askari huyo akwaita wenzake na kusema huyu ni mwandishi anatafuta nini hapa.


Kibao kilinigeukia nikaoneshwa bunduki ndipo nilipofanikiwa kujichanganya na watu nikakimbia na ananchi wasamaria wema wakaamua kunificha.


Zilisikika sauti za wananchi wakisema “mlindeni mwandishi huyo ili akafikishe hayo kwa taifa zima ili watu waone unyama wanaotufanyia polisi”.


Muda mfupi walitokea askari wa kikosi cha kutuliza ghasia na kufukuza wananchi kwa kuwatishia bunduki jambo lililowasononesha watu kuwa hawana uhuru.


“Akionekana mtu hapa tunamuwasha. Ondokeni hapa mara moja hatuwataki hapa. Jitieni na kimbelembele chenu muone. Potea” alisema askari.


Wakati hayo yakitendeka ikatokea gari ya polisi na kumtupia yule kijana na kuondoka naye huku akiendelea kupigwa kwenye ndani ya gari wakati anapelekwa kituoni.


Source: Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima
 
Hawa polisi kwanini wasiamie bungeni wapambane na wavuta bangi kule
 
Sasa polisi anasoma miez6 atajulia wapi sheria?anaamini kazi ya polisi ni kujeruhi na kuua kwa bunduki.ipo siku wapigwa na waonewa watachoka na muda sio mrefu kwani dalili zisha kua wazi
 
Hizi picha na maelezo yako mbona haviendani. Mbona usiweke picha ya wakati akiwa kavunjika huo mguu na kupasuka kichwa?
 
hamana unyama hapo, picha ya kwanza inaonesha askari akienda kumkamata na sio kumpiga, picha ya pili inaonesha kachero akiwa ameshika radio call akielekeza jambo na picha ya tatu inaonesha askari na kachero wakiwa wameinama kujaribu kunyanyua mtuhumiwa alikuwa amekaa nyuma ya pikipiki na si kama ilivyo andikwa katika caption ya hiyo picha, hakuna sehemu inayoonesha kuwa kuna mtu anapigwa sasa kunaunyama gani? au unatuona sisi sio wataamu wa picha na hatujui kutafsiri picha? labda ni mwizi alikuwa anaokolewa na polisi kwa sababu hakuna sehemu inaonesha kwamba askari anampiga mtuhumiwa.
 
hamana unyama hapo, picha ya kwanza inaonesha askari akienda kumkamata na sio kumpiga, picha ya pili inaonesha kachero akiwa ameshika radio call akielekeza jambo na picha ya tatu inaonesha askari na kachero wakiwa wameinama kujaribu kunyanyua mtuhumiwa alikuwa amekaa nyuma ya pikipiki na si kama ilivyo andikwa katika caption ya hiyo picha, hakuna sehemu inayoonesha kuwa kuna mtu anapigwa sasa kunaunyama gani? au unatuona sisi sio wataamu wa picha na hatujui kutafsiri picha? labda ni mwizi alikuwa anaokolewa na polisi kwa sababu hakuna sehemu inaonesha kwamba askari anampiga mtuhumiwa.

Wewe umeona picha,mwenzako alikuwa eneo la tukio,watetee tu hao jamaa,cku yakikukuta ndyo utaelewa kilichoongelewa
 
Hao askari walikua wanajipendekeza tu kusafisha mji, kwani hapo ni karibu kabisa na bunge.

Mbona hamuwapigi wale mbuzi na kondoo wanaozunguka na kulala barabara ya kuu street?
 
Kutoa taarifa za mashaka mashaka ndo kama ugonjwa wetu hivi sasa Watanzania ,maana serikali ikitoa taarifa hatuziamini, bunge likitoa taarifa hatuamini na sasa hata sisi wananchi tukipeana taarifa hatuaminiani rai yangu TUJITAHIDI KUTOA TAARIFA ZA KWELI na kama kuna ushahidi wa wazi usio na shaka uwekwe lkn hata mimi nikiziangalia hizo picha naona ukamataji usio na ukiukwaji na hata hao askari wa ffu naona wapo wakati ukamataji ukifanyika.
 
Kaona lakini picha na alichosema tofauti! Je niamini yeye kawashinda polisi na kukimbia? Kwa jinsi ulivyozungumzia tukio wewe mwenyewe usingekuwa salama! Ungeonyesha hilo boriti la askari ulosema kavaa kiraia,Ulijuaje kama ni askari ikiwa alikataa kukujibu? Eti ulionyeshwa bunduki ukafanikiwa kujichanganya kwa watu,Kwani ukionyeshwa bunduki unakufa! Tusipotoshe jamii,Hatujafika huko bado, Japo kidogo amani hakuna! Chuo cha Pipango? Kupoga Picha?
 
Back
Top Bottom