*Askari wamtoboa mvuvi makalio kwa singe, aoza nusu mwili, yuko hoi hospitalini Geita
MVUVI mmoja mkazi wa kijiji cha Mganza Wilaya ya Chato, katika mkoa wa Geita, yuko hoi hospitalini baada ya kushambuliwa kwa kutumia vitako vya bunduki, marungu na kuchomwa singe na misumari matakoni na baadhi ya askari wa hifadhi ya taifa wa kisiwa cha Lubondo, wilayani Geita.
Mvuvi huyo, Benedicto Thomas (31) alikamatwa na askari hao wa kisiwa hicho waliokuwa doria Aprili 18, majira ya usiku na alianza kupatiwa mateso Aprili 19 mwaka huu, siku moja baada ya kukamatwa usawa wa boya za hifadhi hiyo akiwa ameelemewa na upepo wa ziwa.
Kutokana na kipigo hicho, mvuvi huyo ambaye kwa sasa amelazwa wod namba nane katika Hospitali ya Wilaya ya Geita, ngozi ya mwili wake kuanzia miguuni hadi matakoni imeanza kubanduka.
Mvuvi huyo sasa hawezi kutembea, kukaa wala kuongea kwa ufasaha, kwa sababu ngozi yake imejaa maji kutokana na wadudu waliokuwa wameanza kumshambulia baada ya kucheleweshewa matibabu.
Imeelezwa baada ya kukamatwa Aprili 18 majira ya usiku, alipelekwa moja kwa moja hadi ilipo kambi namba moja ya kisiwa hicho iitwayo Mulaga, ambapo siku iliyofuata alipelekwa kwenye kambi nyingine ya Lugeye alikoanza kupatiwa mateso ya kila aina na askari hao kwa muda wa wiki moja kuanzia Aprili 18-25 alipofikishwa katika kituo cha polisi Wilaya ya Geita kwa hatua zaidi.
MVUVI mmoja mkazi wa kijiji cha Mganza Wilaya ya Chato, katika mkoa wa Geita, yuko hoi hospitalini baada ya kushambuliwa kwa kutumia vitako vya bunduki, marungu na kuchomwa singe na misumari matakoni na baadhi ya askari wa hifadhi ya taifa wa kisiwa cha Lubondo, wilayani Geita.
Mvuvi huyo, Benedicto Thomas (31) alikamatwa na askari hao wa kisiwa hicho waliokuwa doria Aprili 18, majira ya usiku na alianza kupatiwa mateso Aprili 19 mwaka huu, siku moja baada ya kukamatwa usawa wa boya za hifadhi hiyo akiwa ameelemewa na upepo wa ziwa.
Kutokana na kipigo hicho, mvuvi huyo ambaye kwa sasa amelazwa wod namba nane katika Hospitali ya Wilaya ya Geita, ngozi ya mwili wake kuanzia miguuni hadi matakoni imeanza kubanduka.
Mvuvi huyo sasa hawezi kutembea, kukaa wala kuongea kwa ufasaha, kwa sababu ngozi yake imejaa maji kutokana na wadudu waliokuwa wameanza kumshambulia baada ya kucheleweshewa matibabu.
Imeelezwa baada ya kukamatwa Aprili 18 majira ya usiku, alipelekwa moja kwa moja hadi ilipo kambi namba moja ya kisiwa hicho iitwayo Mulaga, ambapo siku iliyofuata alipelekwa kwenye kambi nyingine ya Lugeye alikoanza kupatiwa mateso ya kila aina na askari hao kwa muda wa wiki moja kuanzia Aprili 18-25 alipofikishwa katika kituo cha polisi Wilaya ya Geita kwa hatua zaidi.